Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

Unategemea kauli gani kwa wazee...wanaoshinda kwenye magroup ya whatsap na kupost na facebook
 
Huyu baba akisimama jukwaani ataongea nini neno ufisadi 'conscience ina prick' atamwambia nani acha ufisadi? Sauti itatoka wapi,kama ndani pamesha kufa. Sidhani kama Mwenyezi Mungu ayaruhusu uovu ushinde.
 
Kingunge anusa mchezo mchafu urais ndani ya CCM

Katika Gazeti la Mwananchi la leo, Mzee Kingunge kajitokeza wazi wazi kumpigia debe Ndugu Lowassa, ( Kingunge anusa mchezo mchafu urais ndani ya CCM - Kitaifa , ama kweli saa nyingine huyu babu naona anajichanganya, na anatuhakikishia eti "" Alisema Watanzania wana changamoto nyingi na kwamba tangu mwanzo chama hicho kimekuwa kikilia na umasikini unaolikabili taifa, huku akisisitiza kuwa mwarobaini wa kuondoa hali hiyo ni Lowassa. Kingunge alisema licha ya marais wa awamu zote kufanya mambo mengi, nchi kwa sasa inahitaji kiongozi atakaye ondoa umaskini."" Sijui huyu Babu analysis kama hizi kaziotoa wapi, Mbona huko alikotokea Lowassa MONDULI umasikini umejaa, mbona hakuzitumia hizo mbinu za kuondoa umasikini Jimboni kwake kwanza ndio tujue anauwezo huo, lakini hivi sasa hizo ni porojo. tuu.
one should remember ya kuwa NARENDRA MODI wa India alichaguliwa kupeperusha bendera ya chama chake cha BJP na pia Kuchaguliwa UONGOZI INDIA (PM), baada ya kuweza kuukuza uchumi wa jimbo lake la GUJARATH, ambapo for the period of his tenure the economy grew in double digit and employment increased , NDIPO WANANCHI WAO WAKASEMA HEBU TUMPE NCHI HUENDA AKAIBADILISHA.

NAE LOWASA ASEMA:

“Mimi nitayaleta haya mabadiliko nikiwa ndani ya CCM. Nagombea urais kwa sababu nauchukia umasikini na nitaunda serikali ya kusaidia wanyonge, kuwafukuza machinga, mamantilie na waendesha bodaboda ni upuuzi. Watu wanatafuta riziki tunawafukuza inatakiwa tuwawekee mazingira mazuri,” alisema na kushangiliwa kwa nguvu.

Hilo hapo juu lilosemwa na Lowasa, ningependa wengi wetu tulihifadhi, iwapo huyu Bw Atachaguliwa basi tutaona ya kuwa yeye ndiye wa kwanza atakaye ivunja hiyo ahadi. Sababu kubwa zinazofanya. Nauliza kuna mtu anaependa umasikini, hata masikini haupendi huo umasikini. atueleze atauondowaje, kwa kuwagaia rafiki zake vitalu na miradi yenye mloo mnono

Alisema anauchukia msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na iwapo atakuwa Rais atalimaliza tatizo la foleni katika jijini Dar es Salaam kwa miezi sita.

Kutakuwa na waziri anayeshughulika na jiji la Dar es Salaam tu kama ilivyo kwa nchi jirani ya Kenya. Yeye akiamka tu akili yake yote ni kushughulikia changamoto za jiji hili, MMMM Waziri wa JIJI, Mbona hapo kaongeza wizara zake , kwani MEYA kazi haimudu, si angemuweka Director kuhusika na hayo mambo na mwenye uwezo wa kuchukua maamuzi magumu.

alisema Lowassa ambaye mara kwa mara alikuwa akiwaimbisha wananchi wimbo wa ‘mchakamchaka’, huku akisisitiza kuwa ataiongoza serikali yake kwa mtindo wa mchakamchaka akisema ambaye hataweza atakaa pembeni.


Afananishwa na mtume, Yesu
Akimkaribisha Lowassa Dar es Salaam, Madabida alimfananisha waziri mkuu huyo wa zamani na Mtume Muhammad ambaye alikuwa akitangaza dini lakini alikuwa akipingwa na watu wake wa karibu na kufafanua kuwa kutokana na hali hiyo Mungu alimueleza kuwa hatamuacha na atakuwa pamoja naye.

Sasa huyu anakufuru, Lowassa Afanane na Mtume Muhammad (SAW) au YESU , sasa ukisikia mtu anapandisha damu kichwani na kupat ukichaa ndio huu. Mwanasiasa yoyote yule anakuwa muongo na somehow fisadi tuu, lakini not to be compared with Jesus or Muhammad period.
 
Mpaka walipofikia kumkata Lowassa sijui watatumia mbinu gani; the whole thing is wrong hakuna sababu tena za kumpinga Lowassa wanachama wenyewe awaheshimu contractual obligation zao, Lowassa ana support za wanachama wa level zote.

Sasa unajiuliza hao wanachama wengine awalioni hili la accusation anazopewa huyo mgombea kutokana na sifa sahihi za mgombea yeyote duniani let alone CCM.

Ni hivi uongozi wa CCM auna control tena na discipline ya chama if anything career ya Lowassa wangeiuwa tu wangetaka lakini chama kimekuwa kikilea maovu uwezi kupanda mabua halafu uvune mahindi.

Ao akina Chenge ndio wanaosumbua mahakama, Rostam na genge la matajiri wengine wenye utajiri uliokosa misingi ya mwanzo ndio backers wa Lowassa. Misingi ya chama iko wapi badala ya mawaziri kushughulikia ilani yao na Kinana ku-sort mess za internal culture. Kwa sasa uendeshwaji wasiasa na serikari vitu avieleweki who is responsbile for what mwenyekiti na raisi wa nchi kila siku yuko angani hana habari na afya ya chama kisa muda wake umeisha.

Kila kitu ovyo sijawahi ona serkari na chama kinachoendeshwa hovyo kwa vipimo vya siasa za mataifa ninazofuatulia this is just danger zone even to an amateur kama mimi sioni nationalism propaganda agenda wakati solidarity is at stake, values za taifa azieleweki, moral codes azijulikani, income distribution usio na uwiano sahihi, sheria hazina nguvu, ufiasadi wa hali ya juu; matokeo yake inapelekea kukuza confusion, individualism, udini and anomie.

Lowassa akishinda uchaguzi ujao tutarajie nchi kuvurugika zaidi; its simple atuwezi tena ku-afford raisi asiye jua shughuli yenyewe ugumu wake ikoje, sio hela tu ndio kigezo CCM awaaminiki tena kwenye usimamizi hiki chama kipo kwa sababu ya weak opposition tu; there are 50 million people with different problems and whose contractual relation to their nations are in vague, lack of moral concession and immense poverty all the elements of a failed leadership kwakweli tunahitaji mtu mwenye combination ya mawazo ya vijana na experience ya usalama iliyotukuka na uzalendo usio na mashaka vinginevyo tunakoelekea sio kuzuri.

 
Last edited by a moderator:
Mswahili akipata matako hulia mbwata! hapa ni majungu tu yanapikwa dhidi ya Lowassa baada ya kupanga watoto zao warithi utawala. uzuri mambo yanawaendea kombo katika zengwe lao la kushikisha hatamu watoto wao! Eti hata Ridhiwani na Makamba nao wana mamlaka ya kuamua nani Rais ajaye
 
Hicho kizee kimepoteza heshima,kimefanya kazo na nyerere kinajua miiko aliyoiacha nyerere ambayo imesaidia nchi hii kufaka sasa leo njaa zake na umasiki wake anafata lowasa mwizi na kuwasariti watanzania,kweli njaa mbaya.
 
Katika hotuba yake Songea aliwaambia washabiki wake: ...Nina hakika jina langu halitakatwa......Mimi sitakubali....naamini nanyi hamtakubali............
 
Akili za kingunge na lowasa sawa na inawezekana kingunge anaakili kuriko lowasa maana sisi wasomi tunapojadili hoja na speech yake kidogo inazidi ya mzee wa kubwabwaja,
haya anayoyasema leo mbona hakuyasema 1995 nyerere alipokata jina la lowasa na kuiambia nec ya wachumia tumbo kuwa ccm haitafuti mtu maarufu bali inatafuta mtu safi?
 
katika hotuba yake songea aliwaambia washabiki wake: ...nina hakika jina langu halitakatwa......mimi sitakubali....naamini nanyi hamtakubali............

hana akili ndo maana anaongozwa na akili zaifu kama za kingunge,yeye washabiki aliwatoa wapi?washabiki ni wa ccm ambao aliwaacha nyerere na nyerere alifaliki akawaacha na yeye atawaacha na mwisho wake na genge lake umeishafika,
 
Nimependa sana hapo kwenye MASHNE NA USINGIZI akili safi sana.

Naumia sana kulala wkt mwingine usiku natafuta cha kufanya, kwa nini kusiwe na shift kazini?

nafikiri marais kadhaa watangaza nia wanamajibu
 
Kifo cha nyani miti yote huteleza.mwisho wa utawala wa ccm umeshakaribia wameshaanza kugawana fito .Kingunge huko ccm ana cheo gani .huu ujumbe umfikie pia Pasco kingunge anasema Lowasa akikatwa jina patambika huko ccm.
VOTE FOR UKAWA
 
Last edited by a moderator:
KINABO wewe,,,Kingunge kasema ukweli na ana haki yake kumtaja mtu kwenye mapenzi nae. Bavicha wanavyomtaja Padri kuwa Rais ina maana ndani ya UKAWA kuna wengine kwani ni kosa?
Ya Kaisari muachie Kaisari,,jipangeni ukawa kumpata mgombea msindikizaji dhidi ya Lowassa.
 
Back
Top Bottom