Kingunge amekubali kutumiwa na wezi na mafisadi wa nchi hii hivyo akubali kudhalilika uzeeni, amekosa busara na hafai kabisa hata kusimama mbele ya umma na kuongea. Aliamua kujidhalilisha kuanzia siku nyingi ikiwemo kuliibia Taifa kwa kujifanya mkusanya ushuru hapo kituo cha mabasi Ubungo, kuingizwa kwenye Bunge Maalum la Katiba kwa kigezo cha kuwakilisha waganga wa kienyeji kumbe dhamira yake ilikuwa ni kutetea maslahi ya wezi na mafisadi wa Taifa hili na sasa ameamua kusimama kidete kumtetea Lowasa ambaye kila mtua anajua wazi kuwa ameshiriki mambo mengi ya kifisadi ndani ya nchi yetu.
Hivi Mwalimu Nyerere angefufuka leo na kumkuta huyu mzee alivyoamua kuvua utu wake kwa minajili ya kumtetea Lowasa angejisikiaje