Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

Viongozi wachache tuliowapa madaraka wasije wakajisahau na kusababisha chama chetu kushindwa uchaguzi kwa sababu ya chuki zao binafsi, Wananchi na wanachama walio wengi wasikilizwe wanamtaka nani, na sio viongozi ambao ni wachache!

Umeshaanza kuona chama kinaanguka ehh?

Mtatoka mwaka huu kweli?
 
Mimi mshabiki wa man utd. Hiyo match ya arsenal na Liverpool ninaitizama kwa leisure bila presure.
 
Mungu ambariki Rais Kikwete asimamie haki na uadilifu, hili ni jambo jema ambalo Rais Kikwete atatutendea kama kwaheri ya uongozi wake, nchi kwenda mikononi mwa wezi ni jambo lisilokubalika.

Mungu ambariki Rais Kikwete na ampe ujasiri wa kusimamia lililo jema.

Wana CCM na Watanzania kwa ujumla tutamheshimu kwa kufanya hivyo.

huyo atakuwa mungu wa namna gani,ambariki kikwete kwa lipi kwa haya yote aliyo tutendea.
 
Hivi huyu kiongozi wa wachawi tz ndio a nataka kutuchagulia rais? ???? Abomination!
 
Huyu Mzee heshima yake ndogo iliyokuwa imebakia baada ya kufanya ufisadi wake stendi ya ubongo sasa heshima hiyo anaizika rasmi, hivi huyu Mzee EL asipokuwa Rais atauweka uso wake wapi?Mzee asiyejua taratibu za chama na kutoa kauli kama kijana mdogo asiyejua lolote ni aibu ata kumuweka miongoni mwa wazee wa chama.
Taratibu za chama ni zile zinazolingana na tafasiri binafsi! Hakuna anayeijua CCM zaidi ya huyu mzee. Wanayoyafanya yalifanyika 2005 kwa nini sasa yawe haramu wakati kanuni na taratibu hazijabadilishwa? Ingawa nafikiri Lowassa akikatwa huyu mzee inabidi matabibu wawe karibu na dawa za shinikizo la damu!
 
Pole sana Nape Nnauye naona nyota yako inazidi kufifia, mara nyingi kumekua na taarifa za wewe kushushwa jukwaani na Kinana kutokana na kauli zako, juzi kati hapa ukaja na goli la kidole mara na mkono na sasa umekuja na jipya!

Mzee Kingunge amejitokeza hadharani na kuonya kuwa kauli zako zinakizika chama chako na mimi nasema mfe tu maana tumechoka! Kingunge amethibitisha kuwa huko ndani ya CCM kuna fukuto kubwa na wala sio Demokrasia tena bali ni Domg ghasia ndio iliyojaa huko CCM.

Pumzikeni kwa amani

Safi sana Mzee Kingunge.... Mungu akibariki sana mzee wetu
 
Hivi vyombo vya habari vinaanzaje kumpa airtime kwenye vyombo?
Mzee mwenyewe hata kuona haoni vizuri amefikaje huko?

aka kazee kanatia aibu bure.
 
Kama hakutaja jina na mleta mada kataja jina huku akisema Kingunge amesema basi huo ni upotoshaji either ni directly or indirectly..
gsam
Mleta mada please ukileta habari leta kama ilivyo wenyewe tutatoa tafsiri yetu na sio kuleta tafsiri yako, kama ni mawazo yako basi ni vema utuambia kabisa ni mawazo yako...

Kweli mkuu..asante sana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom