Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

Viongozi wachache tuliowapa madaraka wasije wakajisahau na kusababisha chama chetu kushindwa uchaguzi kwa sababu ya chuki zao binafsi, Wananchi na wanachama walio wengi wasikilizwe wanamtaka nani, na sio viongozi ambao ni wachache!

haa haa kwani kingunge aliwasikiliza lini hao hao wananchi? kingunge kuhangaika kote huko ni kumsemea lowasa hakuna kingine.
 
kingunge anataka lowasa apitishwe na chama chao,Na kikwete anataka membe apitishwe...Akina warioba wanamtaka makongoro apitishwe......karume anamtaka ally karume apitishwe....NI KWELI PATACHIMBIKA
 
Viongozi wachache tuliowapa madaraka wasije wakajisahau na kusababisha chama chetu kushindwa uchaguzi kwa sababu ya chuki zao binafsi, Wananchi na wanachama walio wengi wasikilizwe wanamtaka nani, na sio viongozi ambao ni wachache!

ccm nacho ni chama ama gege la majambazi na wanyonyaji.
 
Hajalipwa hata senti tano, Ila Mzee Kingunge anasimamia maslahi ya CCM.

Kingunge amekubali kutumiwa na wezi na mafisadi wa nchi hii hivyo akubali kudhalilika uzeeni, amekosa busara na hafai kabisa hata kusimama mbele ya umma na kuongea. Aliamua kujidhalilisha kuanzia siku nyingi ikiwemo kuliibia Taifa kwa kujifanya mkusanya ushuru hapo kituo cha mabasi Ubungo, kuingizwa kwenye Bunge Maalum la Katiba kwa kigezo cha kuwakilisha waganga wa kienyeji kumbe dhamira yake ilikuwa ni kutetea maslahi ya wezi na mafisadi wa Taifa hili na sasa ameamua kusimama kidete kumtetea Lowasa ambaye kila mtua anajua wazi kuwa ameshiriki mambo mengi ya kifisadi ndani ya nchi yetu.

Hivi Mwalimu Nyerere angefufuka leo na kumkuta huyu mzee alivyoamua kuvua utu wake kwa minajili ya kumtetea Lowasa angejisikiaje
 
Hivi vyombo vya habari vinaanzaje kumpa airtime kwenye vyombo?
Mzee mwenyewe hata kuona haoni vizuri amefikaje huko?

aka kazee kanatia aibu bure.

Anaona vizuri..Kila siku jioni anakagua hesabu za ushuru wa parking zote za Dar..
 
Watu hawawezi kufuata akili za mzee kingunge.huyu mzee amechanganyikiwa kabisa Na lowasa.hivi haoni kuwa hata yeye hakitendei haki Chama chake kwa kumpigia debe mtu ambaye Si muadilifu? Tanzania ina hasara Sana kuwa na mzee huyu hapa nchini.
 
Ukweli CCM migogoro na hawa wazee wenu inawangusha penda msipende hizo ni dalili ya CCM kufell mwaka huu

Sikio la kufa halisikii dawa na babu seya mwaka hub atakuwa uraiani maana miakamitatu haiendani na bill 11!
 
Viongozi wachache tuliowapa madaraka wasije wakajisahau na kusababisha chama chetu kushindwa uchaguzi kwa sababu ya chuki zao binafsi, Wananchi na wanachama walio wengi wasikilizwe wanamtaka nani, na sio viongozi ambao ni wachache!

Kwa taarifa yako Mimi nafanya tafiti mkimpitisha Lowassa kwa kisingizio cha kupendwa ndani ya chama mmekwisha.
 
Tatizo la ccm mpka viongozi nao wanatimu za wagombea wao sasa nape naye anatumia nafasi ya msemaji Wa chama Kwa maslai ya Kambi yake sipati picha nape atakapotangaza Kwa waandishi Wa habari kamati kuu imemteua lowasa kuwa mgombea
 
Pole sana Nape Nnauye naona nyota yako inazidi kufifia, mara nyingi kumekua na taarifa za wewe kushushwa jukwaani na Kinana kutokana na kauli zako, juzi kati hapa ukaja na goli la kidole mara na mkono na sasa umekuja na jipya!

Mzee Kingunge amejitokeza hadharani na kuonya kuwa kauli zako zinakizika chama chako na mimi nasema mfe tu maana tumechoka! Kingunge amethibitisha kuwa huko ndani ya CCM kuna fukuto kubwa na wala sio Demokrasia tena bali ni Domg ghasia ndio iliyojaa huko CCM.

Pumzikeni kwa amani

CCM IMEFICHWA BAGAMOYO KAZI MNAYO IKOMBOENI SASA!/ii
 
Back
Top Bottom