Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

Kingunge akerwa, akemea yanayoendelea ndani ya CCM

kingunge mbele ya lowasa afadhali chama kisambaratike kuliko kumtosa lowasa.

Huyu mzee bure kabisa
Kwa nafasi yake ktk chama hakutakiwa kuwa na upande alitakiwa asiwe na upande wowote,
kwa hali hii anakiua chama.
 
Haujuwi kuwa Kingunge ni Mwenyekiti wa waganga wa kienyeji?

Faiza naona umepania kuvunja mbavu wasomaji kwa kicheko - loh! Kama yeye ni Chairman wa ufundi basi atakuwa Judge, Jury na Executioner all rolled in ONE - hakuna haja tena ya kukata rufaa atayamaliza mwenyewe.
 
Mashabiki, wanazi na watazamaji tumeanza kunawa uso na kuvaa miwani zetu ili tuone vizuri mtifuano wa nani zaidi kati ya CCM Nape na CCM Kingunge (mganga mkuu wa kienyeji) katika kuwania kumpata mgombea wa urais kupitia CCM. Nguvu za CCM Nape ziko kwenye kamati za CCM na nguvu za CCM Kingunge ziko nje ya vikao (wanachama, wapenzi, wananchi, media) rasmi vya chama. Nani atanywea na madhara yake kwa CCM ni jambo la muda tunalolisubiri watazamaji. Nani ataibuka kidedea?
 
Wote kwanza Mzee kingunge na Nape wanavunja kanuni ya chama,Nape amekuwa mropokaji sana bila kuchuja kipi cha kusema na chaku kaa kimya japo ni kazi yake kuzungumza kama msemaji wa chama..na Mzee kingunge yeye ana tetea maslahi yake na watu wake japo anatumia madhaifu ya Nape kufanikisha lengo hilo kufikisha ujumbe kwa wakubwa wengine wa chama.
 
Mashabiki, wanazi na watazamaji tumeanza kunawa uso na kuvaa miwani zetu ili tuone vizuri mtifuano wa nani zaidi kati ya CCM Nape na CCM Kingunge (mganga mkuu wa kienyeji) katika kuwania kumpata mgombea wa urais kupitia CCM. Nguvu za CCM Nape ziko kwenye kamati za CCM na nguvu za CCM Kingunge ziko nje ya vikao (wanachama, wapenzi, wananchi, media) rasmi vya chama. Nani atanywea na madhara yake kwa CCM ni jambo la muda tunalolisubiri watazamaji. Nani ataibuka kidedea?


Mzee Kingunge aliisha jivunjia heshima baada ya kuonyesha ni mfuasi wa fisadi Lowassa
 
Kama unaweza kaa macho kuanzia saa usiku na kuendelea utasikia matokeo ya mnyukano huu. Kimsingi huu ni mnyukano kati ya kingunge na J.K kama alivyosema Nape mwenyewe kwamba kingunge amuulize aliyemtuma kazi nape
 
Tayari Nape Amekubali Nguvu ya umma ... Msome ktk uzi mwingine ... Lowassa ndo Rais wa 2015 - 2020
 
Kingunge atuachie chama chetu. Huyu mzee hana hata haya.
 
Pamoja na kila mmoja kuwa na mfuas wake anaemjua mwenyewe na waliojionesha wazwaz wao ni team nan mfn kingunge lakini nape hana hekima ya mazungumzo kama walivyowasemaj wa klabu flan hapa nchin ..
Anashindwa kuchuja kauli zake anapozungumza mbele ya public anahis kama ni chake pekeyake na ana amri
Lkn nikiangalia nyadhifa aliyokuwa nayo kinana pale ccm ni kubwa kuliko nape lkn kinana yuko smart in talking kuliko huyu nape ...
Haya bhn tupo kufatilia hiz epsodes zao kuelekea uchaguz mkuu hii ndo kwanza epsode 1
 
Lowasa akipata urais Nape itabidi ahame nchi
 
Mzee Kingunge aliisha jivunjia heshima baada ya kuonyesha ni mfuasi wa fisadi Lowassa

Hili ndio kosa la karne alilofanya heshima yake haiwezi rudi kamwe. Mwaka 1995 alisimama kwenye kamati bila kigugumizi na kusema lowasa hafai.
 
Kingunge anatumia nafasi yake ili kushibisha njaa yake. Kwa mzee kama yeye hakutakiwa kuwa na upande. Ila sababu ya njaa zake - na hasira za kunyang'anywa Ubungo Terminals na NPS - ndio maana anamkuwadia Lowassa - ili baadae apate sehemu nyingine ya kuweka mirija yake. Muhimu ajue kuwa watanzania wa siku hizi sio walewale wa zamani ambao unaweza kuwadanganya nao wakakubali kirahisirahisi.
 
Na hapati ng'o labda rais wa masai!

Usiseme hivyo wewe Lowassa yuko kwenye mikono salama ya gwiji (KGB) la kirusi na mganga mkuu wa kienyeji nchini. Usimu-nder rate Kingunge amefanya mengi ndani ya nchi hii, sio wa kubezwa hata kidogo.
 
Kingunge atuachie chama chetu. Huyu mzee hana hata haya.

wewe na kingunge nani mwenye chama? mnajidai chama chenu baada ya kuona ma v8? hawa wamejenga chama kwa kutumia miguu na baiskeli leo mtu kama nape anabwabwaja hovyo hajui chama kimetoka wp? mi nawashangaa sana acha sisi tujenge chadema yetu.
 
KAULI ya mwanasiasa wa zamani Kingunge Ngombale-Mwiru dhidi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye kuhusu maamuzi ya vikao ndani ya chama hicho, imeibua mjadala kutoka kwa wajumbe wa vikao hivyo wanaohoji anachokitetea mzee huyo.

Wakizungumza na FikraPevu kwa nyakati tofauti, wajumbe hao wamehoji kinachomsukuma Kingunge kupigana kufa na kupona kumtetea Lowassa bila kuzingatia maslahi ya chama na Taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Nape alisema Kanuni za Uteuzi wa Wagombea wa CCM kuingia katika Vyombo vya Dola, toleo la Februari 2010 hazitoi nafasi kwa Mgombea wa Nafasi ya Urais kukata rufaa.

Hata hivyo, Kingunge akizungumza na waandishi wa habari alionekana kuwa na msimamo tofauti akisema mgombea anaweza kukata rufaa bila kutoa mifano wala nukuu ya kanuni zinazoruhusu jambo hilo.

Mmoja wa wajumbe wa NEC aliyepo Dodoma, ameifahamisha FikraPevu kuwa mkakati wa baadhi ya wagombea ni kuvuruga vikao baada ya kuanza kukata tamaa.

“Wapo wanachama waliwahi kukata rufaa huko nyuma, akiwemo Lowassa mwenyewe 1995 kupitia makada wengine kina Galus Abeid na Yusuf Makamba, lakini Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere, wakati huo alisema kwamba kazi ya vikao vya maamuzi ni kupunguza idadi ya wagombea si kuongeza majina,” anasema mjumbe huyo na kuongeza;

“Mifano mingine ni mwaka 2005 ambapo Mzee Malecela (John Samwel) alikata rufaa kupinga kuenguliwa katika nafasi ya kuwania urais kupitia CCM na alipoomba kujieleza ndani ya NEC alijibiwa kwa dakika tatu tu kwa Mkapa kuzungumzia mambo mawili tu ikiwamo suala la umri kuwa mkubwa na kukumbushia kukataliwa kwa Malecela na Mwalimu Nyerere.”

Alisema katika mchakato huu unaoendelea, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, alipoingizwa katika kundi la wataka urais sita waliosimamishwa na CCM mwaka 2014, aliamua kukata rufaa kupinga kuhukumiwa bila kuzingatia uzito wa makosa anayotuhumiwa nayo, lakini hadi sasa hakuwahi kujibiwa wala kujadiliwa na badala yake CCM iliendelea na mchakato wake.

Mjumbe huyo mkongwe anasema katika hali ya kawaida, vikao vya maamuzi vinakuwa na ratiba ambayo wakiruhusu kukata rufaa, italazimika kusitisha shughuli zote kwa muda usiojulikana.

“Kinachofanywa na Kingunge ni kutafuta uhalali wa kutata rufaa ili kuvuruga mchakato, ili vikao vya NEC na Mkutano Mkuu usifanyike wakati Kanuni ya tano imekaa kimya kuhusu rufaa katika vikao vya uchujaji na uteuzi,” anasema.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mzee Kingunge akionekana kumtetea Lowassa alitoa mfano wa Mzee Malecela bila kueleza jinsi Mkapa alivyozima hoja ya Malecela alipopewa nafasi ya kuzungumza (si kukata rufaa) ndani ya NEC.

Tayari wafuasi wa Lowassa wanadaiwa kuanza kueneza taarifa kwamba Nape amefukuzwa uongozi na kuvuliwa uanachama kwa kumzibia nafasi mgombea wao na kwamba mapendekezo hayo yametolewa na Kingunge.

FikraPevu imeelezwa kwamba hasira na visasi vya Kingunge vinatokana na migogoro katika kampuni zake za ujenzi na ukusanyaji ushuru katika Kituo cha Mabasi na Maegesho anakodaiwa kuwa alikuwa anainyonya serikali fedha ambazo zingeweza kutumika kulipia mishahara na huduma za hospitali.


Source: FikraPevu

Kauli ya Kingunge yaibua mjadala CCM, wadau wahoji anachokitetea | Fikra Pevu
 
Kingunge naye amebaki ni mchumia tumbo anaejaribu kumpigania mchumia tumbo mwenzake ili akipata aendelee kuchuma zaidi na zaidi.
 
Tatizo la ccm wanaishi maisha kama ya Tom and Jerry hawapendi kuambiwa ukweli
 
Back
Top Bottom