Kwenye gazeti la Mwnanchi la leo lina taarifa hii na naomba kulinukuu gazeri:
Mwanasiasa Mkongwe wa CCM , Kingunge Ngombale Mwiru amemshukia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye kwa kauli zake alizodi zinaminya demokrasia na kwamba CCM haiwezi kusimma wanapopambana wenyewe kwa wenyewe.
Kingunge ambaye hivi maribuni aliweka bayana kumuunga mkono Mbunge wa Monduli , Edward Ngoyayi Lowassa katika harakati zake za kuwania urais , alisema hakubaliani na kauli ya Nape kuwa Wagombea wasioridhika na uamuzi wa Kamati Kuu(CC), hawezi kukata rufaa kwa sababu ya muda kuwa mfupi. Mwisho wa kunukuu.
Sote tunajua Nape ni msemaji wa chama na ni mjumbe wa kamati Kuu na kwa maana hiyo kauli yake inaweza kuwa kauli ya Kamati Kuu na CCM kwa ujumla. Binafsi naamini Kama mwana CCM , kingunge hawezi kumshukia kiongozi wake waziwazi hivyo, anaweza kufanya hivyo kama atasimama kama mtu binafsi na kwa maslahi ya mtu binafsi. Je ameongea kama Team Lowassa? Na kama jibu ni ndiyo je, anajuaje kama Lowassa ndiye atakatwa peke yake? Kingunge anajuaje kama wakikatwa wengi, ni Lowassa pekee ndiye atakayekata rufaa?