voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,552
- 11,891
Umejitokeza kwenye Kongamano linalohusisha ukuaji wa Demokrasia na unasema demokrasia imekua kwa kiwango kikubwa nchini. Je, ni demokrasia ipi unayoiongelea wewe?
Wakili Madereka yuko akishikiliwa na Polisi huko Arusha kisa amekosoa na kupinga Mkataba wa DP-WORLD.
Ni Demokrasia ipi hiyo iliyokua, wakati Dkt. Slaa, Wakili Mwabukusi na Mwanaharakati Mdude Nyagali bado wanasumbuliwa na Polisi kwa sababu wametoa maoni yao na kupinga Mkataba mbovu wa DP-WORLD? Ikafikia mahali hata wanakamatwa kwa mfumo wa "utekaji"!
Hapa tunaandika, wao hata simu na laptop zao bado zimeshikiliwa na Polisi ingawa imeshindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yao na kulazimika kuwaachia baada ya sauti huru kuwazidi nguvu kutoka ndani na nje ya nchi.
Tunayo mifano mingi sana ya kuzuia wananchi kutoa maoni yao. Ila pia unakumbuka ile clip yenu ovu enzi mkiwa benchi?
Mfano halisi ni huu wa sasa ambapo serikali imezuia vyombo vya habari kuchapisha waraka wa maaskofu wa madhehebu ya kikatoliki nchini TEC, kwa kupewa amri na Serikali kupitia Waziri wa habari huyu ambae ni Nape Nnauye.
Kinana hana hata aibu mbele ya watanzania anasimama kuongea pumba. Watanzania wa sasa sio wa jana!
Wakili Madereka yuko akishikiliwa na Polisi huko Arusha kisa amekosoa na kupinga Mkataba wa DP-WORLD.
Ni Demokrasia ipi hiyo iliyokua, wakati Dkt. Slaa, Wakili Mwabukusi na Mwanaharakati Mdude Nyagali bado wanasumbuliwa na Polisi kwa sababu wametoa maoni yao na kupinga Mkataba mbovu wa DP-WORLD? Ikafikia mahali hata wanakamatwa kwa mfumo wa "utekaji"!
Hapa tunaandika, wao hata simu na laptop zao bado zimeshikiliwa na Polisi ingawa imeshindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yao na kulazimika kuwaachia baada ya sauti huru kuwazidi nguvu kutoka ndani na nje ya nchi.
Tunayo mifano mingi sana ya kuzuia wananchi kutoa maoni yao. Ila pia unakumbuka ile clip yenu ovu enzi mkiwa benchi?
Mfano halisi ni huu wa sasa ambapo serikali imezuia vyombo vya habari kuchapisha waraka wa maaskofu wa madhehebu ya kikatoliki nchini TEC, kwa kupewa amri na Serikali kupitia Waziri wa habari huyu ambae ni Nape Nnauye.
Kinana hana hata aibu mbele ya watanzania anasimama kuongea pumba. Watanzania wa sasa sio wa jana!