President Samia’s math ain’t mathing 🤔

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,405
114,358
Tuliambiwa kwamba Rais Samia karejesha demokrasia, amani, utulivu, haki, n.k.

Twende mbele mpaka leo hii ambapo kuna watu waliandamana kupinga mkataba wa serikali na kampuni ya DP kutoka Dubai.

Vijana wamejitokeza na mabango yao na wakaingia barabarani ili kuonyesha kutokufurahishwa kwao na matakwa ya huo mkataba.

Hiyo ni haki yao kabisa inayolindwa na katiba. Ni haki yao ya kikatiba.

Lakini cha ajabu, wameishia kuchezea virungu vya polisi wa Samia na wengine wamekamatwa na kupandishwa kwenye Difenda za polisi.

Kosa lao ni lipi? Eti ni kuandamana!

Sielewi! Toka lini haki iliyopo kwenye katiba ikawa ni kosa?

Demokrasia aliyoirejesha Samia ni ipi hasa?

Wakishindwa hoja, wanaanza kutumia mabavu.

Kama huo mkataba hauna ubaya wowote, basi waache kutumia mabavu.

Hoja hujibiwa kwa hoja.

Ukianza kujibu hoja kwa mabavu, basi ni ushashindwa. Unalazimisha tu.
 
Tuliambiwa kwamba Rais Samia karejesha demokrasia, amani, utulivu, haki, n.k.

Twende mbele mpaka leo hii ambapo kuna watu waliandamana kupinga mkataba wa serikali na kampuni ya DP kutoka Dubai....
Demokrasia ya kufanya mikutano ya kisiasa ndio imerejeshwa na Ccm kwa sasa, hiyo ya kuandamana isubiri majadiliano mengine.
 
Hakuna democrasia Tanzania. Hata marekani pia hakuna democrasia ni uhuni tuu.

Jambo likishakuwa la public interest lazima nguvu itumike popote pale.

Hao wamarekani wanaojifanya Baba WA democrasia mbona hawatuachii Uhuru waafrica tuamue tusapoti Nani kwenye mgogoro WA Ukraine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kula chuma iko
IMG-20230619-WA0000.jpg
 
Kwa sababu hajawagusa wanasiasa wakubwa huwezi ona hili likipigiwa kelele. Wale wakubwa wanalamba asali kwa sasa hii si issue kwao.

Na hao wakubwa. Ukitaka Serikali ionekane ya kidikteta iwazibie mirija hawa wakubwa. Kwa wadogo hawa hamna shida. Umesahau walishawahi uawa watu wengi toka miaka ile ya kikwete na wengine kuvunjwa viungo.

Lakini sababu wale wakubwa walikuwa wanakula vizuri haikuwa shida.
 
Hoja zao zimejibiwa lkn wamegoma kuelewa, hatuwezi kukubali wahuni wachache watuharibie nchi, nasema hivi watandikwe tu.
 
Ikumbukwe:
●Hao walioandamana ni raia wa Tanzania wanaolilia urithi wao kwa njia ya amani.
●katiba inawaruhusu kufanya maandamano ya amani
●serikali inapaswa kutoa maelezo ya kinachoendelea kuhusu dp world mpaka pale tutakapoelewa na kuridhika na siyo kutumia nguvu.

Ni aibu kwa nchi inayoaminika kuwa na serikali ya kidemokrasia askari kutumia nguvu kubwa kupambana na raia wanaoandamana kuhoji wanachotaka kueleweshwa

Kwa hili ni wazi kuna agenda ya siri ambayo hatuijui kuhusu mkataba wa dp world na tutapojua huwenda itakuwa too late.
 
Nini kazi ya Polisi zaidi ya kuzuia na kuwakabili hao Vibaka watakaojitokeza?

Maandamano ya amani yanaambatana pia na Polisi kuhakikisha usalama wa raia.
Intelegensia imenusa harufu ya uharifu, wahuni ni wengi kuliko polisi
 
Hakuna democrasia Tanzania. Hata marekani pia hakuna democrasia ni uhuni tuu.

Jambo likishakuwa la public interest lazima nguvu itumike popote pale.

Hao wamarekani wanaojifanya Baba WA democrasia mbona hawatuachii Uhuru waafrica tuamue tusapoti Nani kwenye mgogoro WA Ukraine

Sent using Jamii Forums mobile app
MKATABA ULE....
 
Back
Top Bottom