Kinana amburuza Msigwa kortini

Kinana amburuza Msigwa kortini

nia yake si kumfunga msigwa bali anataka haya mambo ya ujangili yasiendelee kuongelewa. mia
Anachokifanya Kinana ni kuwazuia CHADEMA na watetezi wa kuzuia ujangili kuendelea kumtaja kama mmoja wa wahusika wa ujangili ndani na nje ya Bunge kwa kisingizio kuwa shauri liko mahakamani na hivyo kutoingilia uhuru wa mahakama!
 
siku ya kesi watz wote tufurike mahakamani maana ni kwa malsahi ya Taifa hii kesi
 
Safi sana comrade kinana wamezoea uzushi na uongo ila sasa naona wamepata muarobaini wao

mwarobaini wapi weyeeee!!,subiri uone huyo unayemwita kamanda namna atakavuombuliwa!!!,unakumbuka list of shame ya pale mwembe yanga?,unakumbuka ni kesi kesi ngapi hao wanatuumiza sisi walala hoi namna walvoungushwa na CHADEMA?.............watch out!!!.....KINANA kajiumiza,ni khery angekaa kimya!!!
 
Mbona haya ni mambo madogo sana,wala hata hayaitaji Akili nyingi kujua kwamba Kinana Katibu mkuu wa Ccm tuhuma anazotuhumiwa nazo sio za uongo!

Huu sio wakati wa Ujima kutumia Polisi na Mahakama kuwaogopesha watu wasiseme ukweli. Msigwa ana uhakika na anachokisema.
Mzee wa Tanganyika(MTIKILA) aliwahi kushitakiwa kwa kesi ya kumuita Kikwete GAIDI.lakini Mtikila bado alishinda hiyo kesi. Je Kinana ni zaidi ya Kikwete?
WAUE TEMBO WAO HALAFU HAWASHITAKIWI,LAKINI WAKIITWA WAUAJI WAO WANASHITAKI!.


Always the fact will remain constant!! Kati ya Jangili (CCM) na Mchungaji (Mwananchi) tutajua nani mkweli!
 
Peleka mahakamani huyu mchungaji kanjanja.
haitasaidia kuwatua hilo pakacha la mavi ni mapito tu nanyi tunawasubiri pale kisutu kwa kesi ya uhujumu uchumi tarehe 30/3/2015
 
Duh! kumbe nyie mkituhumiwa mnaathirika kisaikolojia na inawauma,vp lwakatare wa watu mliyemhusisha na ugaidi mkamsweka mahabusu.......kuweni na haya ccm.....tembo wetu wanakufa kweli na meli zako ndio zinasafirisha meno ya hao tembo pls!Mr Kinana usinichefue eti umeathirika kisaikolojia.
Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.
 
Kwani hizo pembe zinazokamatwa huko nje ya nchi na tunaambiwa zimetoka TZ nani mhusika? Serikali ya CCM itupe jibu mapema. Wanchi rasilimali zetu zinaporwa na sisi wenyewe i.e walio madarakani kwa kuhusika moja kwa moja au kwa kutoa vibali with 10 percent. Mambo mengi yamefichika ndio yanaanza kusikika kidogo kidogo.
 
Safi sana comrade kinana wamezoea uzushi na uongo ila sasa naona wamepata muarobaini wao
Embu ninong'onezee...""Na wewe unamsaidiaga kupakia hayo majino ya ndovu nii""Mbona unamsapoti kama vile ni halali yeye kuangamiza hawa viumbe!!!??
 
hapo waanze na finger print

Finger Print pamoja na Footprints....

Huyu Kinana hatoki mwaka huu, tutampeleka mahakama ya Afrika Mashariki kama maCCM hayataki kumpeleka mahakamani kwa udhalimu wake na wasomali wenzie kwenye Tembo
 
Peleka mahakamani huyu mchungaji kanjanja.
Yaani siku utakapojishitukia na udini wako basi nafikiri utakuwa na michango mizuri humu JF. Udini unakusumbua sana. Ungekuwa na binti basi naomba mwenyezi Mungu aolewe na Mkristu, hata kama ukikataa, ili ujue udini hausaidii.
 
Mingine yupo humuhumu ndani wanasema mchungaji KANJANJA...Wakati anakashfa na yeye ya madawa ya kulevya tunamnyamazia tuu!!!
 
Kinana andhani akizuia isiongelewe kwa "...kuliweka mahakamani..." kutamsaidia kupata muda wa kipiga bao a la haraka na CCM.Ila hajui kuwa 2015 ni mbali sana kwa hizi kesi kubaki kusaidia...Na tayari jina lake ni kinyaa ktk watanzania.

Kinana hana mvuto kwa watanzania.....alipata umaarufu wa enzi hizo wakati RTD na magazeti mengine yakiwa yanawaandika habari za kupamba..huku waandishi wengine wakija na namna mpya ya kuchagua chohote ktk pumba za maccm ili habari iwe na harufu nzuri.
 
Lazima uwe mpuuzi wa kutupwa na mtu usiyejua hata historia ya huyu mtu. Kinana huyu alihamisha machine ya kufulia nguo iliyoletwa kwa matumizi ya hospitali ya mkoa wa Arusha- Mount Meru Hospital akaipeleka kwenye dry cleaner yake inaitwa Falcon, aweza vipi kuwa msafi? Mtu asiye na huruma hata kwa wagonjwa? Kwa tafsiri rahisi huyu ni muuaji na mbovu mkubwa sana ambaye hana hata sifa moja ya kuwa kiongozi nchi hii.
watanzania tuna matatizo ya akili, watu wanashabikia kuibiwa na kuhujumiwa. kwa kitendo hicho na kitendo cha kampuni yake kusafirisha meno ya tembo, ilitakiwa asiwepo kabisa kwenye safu ya uongozi wowote wa chama/serikali.
 
Tembo + meno ya tembo... Sasa vinaenda kupata suluhisho kupitia mahakama. Tunaomba wadau kama kutakuwepo na uwezekano hii kesi iwe inarushwa live ili watanzania tujue mbivu na mbichi maana tembo kila siku wanapungua wauwaji mkitajwa mnakimbilia mahakani ule wenu ushaidi uje uwasute!!! Haiwezekani wewe kinana meli yako ikamatwe na meno wa tembo wetu alafu wewe unajifanya hujui lolote!! Kukimbilia mahakamani kabla ya kutuomba msamaha kwa uhaini wako ni laana itakayokumaliza mwenyewe na hakika kama umejipanga kuwahonga hao majaji usitegemee ushindi wa mezani kwan siku zote giza na mwanga havichangamani hata siku moja!!
 
nina kila sababu ya kuamini kuwa hii haikuwa the right move kwa mzee wetu Kinana..
nina amini kabisa mchungaji Msigwa hakukurupuka kutoa shutuma nzito vile tena ndani ya bunge!
kwa wale ambao mna access tafuta zile hansard za bunge za siku ile
ilikuwa hivi...
baada ya Msigwa kutoa shutuma zile, mh. William lukuvi alisimama kukanusha vikali shutuma zile... baadae kidogo Msigwa alisimama na kusema kuwa, namnukuu '' ...mheshimiwa spika badala ya kunitukana, kunizomea na kunitaka nikanushe madai yangu kwanini hamniombi nithibitishe madai yangu..''
hii inaonyesha dhahili kuwa mhe. Msigwa anajua anachokifanya na amekuwa anatafuta hii chance ili athibitishie umma wa Watanzania juu ya madai yake..
mzee Kinana anapaswa ajiandae vizuri sana, kwani hata sisi ambao ni wafuatiliaji wa mambo nje ya magazeti na mitandao tunajua udhaifu alionao kimaadili (ya uongozi)..
yataibuka mengi sana katika hii kesi..
tusubiri
 
mbunge anapotoa kauri bungeni,kauri hiyo kisheria haihojiwi mahakamani,labda tu kama ameshitakiwa kwa kusema nje ya bunge
nashangaa hili haramia mambo ya bungeni tangu lini yakaenda mahakamani
 
Mimi nitamtetea Msigwa
Hayo maneno hakuyasema akiwa mzima, alikuwa ameingiwa na pepo mbaya tu
 
Back
Top Bottom