Kinana amburuza Msigwa kortini

Kinana amburuza Msigwa kortini

Well done kinana,

Hizi sifa za "kitoto" za hawa wabunge wetu lazima ziwatokee puani.


Kinana ni mtu makini sana na kwa muda aliotafakari na wanasheria wake lazima MCHUNGAJI wa chadema atajuta.


Mwigulu Nchemba and Job Ndugai inclusive!!.......

 
Hivi ile kesi ya Riz-1 dhidi ya Dr.Slaa imeishia wapi?.

1.Pesa ya kununua meli kaitoa wapi?
2.Je si ni kweli Meli iliyohusika kubeba pembe za Ndovu yeye anaumiliki, kwa hiyo yeye ni sehemu ya matatizo,suala la ukaguzi unafanywa na mamlaka za Serikali haina mashiko.
3.Si ni kweli kuwa yeye ni Katibu Mkuu wa CCM yenye Serikali anatoa wapi heshima ya kupanda jukwaani na kuwa shawishi wananchi/wapiga kura kuwa Serikali na Chama chake wanafanya kazi nzuri ili hali Ndovu wetu wanaisha kupitia Meli zake na Watumishi ambao Chama chake kinatakiwa kuwasimamia na hiyo ndiyo hoja na kauli ya Mbunge na kazi halisi ya Mbunge.
4.............
5.............yako mengi wengin e wataongezea.





Katika hati ya madai amenukuu baadhi ya kauli za Msigwa, ikiwemo "Kinana (naomba waandishi wa habari mnisikie na nyie Usalama wa Taifa mkapeleke habari) hana sifa za kupita barabarani na kuwaambia Watanzania waiamini CCM. Kinana mikono yake si misafi."

"Hata kwenye Nassaco, Shirika la Meli Tanzania kuna harufu ya ufisadi ndani yake; ajibu hoja...Kinana meli zake ndizo zinazohusika kubeba pembe za ndovu nchini. hajajibu hoja hizo! Kwa siku nchi hii tembo 67 wanauawa. Hao ndio wanaokifadhili Chama Cha Mapinduzi, halafu wanakuja eti kuwashawishi Watanzania muwasikilize na kwamba Chama Cha Mapinduzi eti ni kizuri."

".Haya mambo ninayoongea ni hatari kwa sababu haya yote ni majangili ni organized Crime. Ni mtandao wa Kimafia, uko duniani kote, unaweza ukatuua lakini wabunge tumesimama tunawatetea..."
Anadai kuwa kabla ya tuhuma hizo alikuwa katika hatua za mwisho za mchakato wa mazungumzo ya mradi wa ubia wa kilimo cha mboga na mwekezaji kutoka kampuni ya nje, lakini tuhuma hizo zimesababisha kampuni hiyo kuvunja majadiliano hayo.
 
Peleka mahakamani huyu mchungaji kanjanja.

Kwa hiyo ataendelea kuiambia hata Mahakama kuwa ni kweli meli iliyobeba meno ya tembo na kukamatiwa Hongkong ilikuwa yake lkn meno hayakuwa yake?

Kinana kashauriwa vibaya!
 
mbunge anapotoa kauri bungeni,kauri hiyo kisheria haihojiwi mahakamani,labda tu kama ameshitakiwa kwa kusema nje ya bunge

mkuu, naona wewe kama kama umekurupuka vile. kama umeelewa bandiko hilo, utakumbuka kuwa msigwa amenukuliwa akisema maneno hayo nje ya bunge tarehe 21 Aprili 2013 kule Mbuguni Mwanza. kwa hiyo huko ni Bungeni
 
mzee kinana hapa utakua umepotea njia kabisaa nenda tena kakae chini na hao waliokushauri kufanya hayo uliyokusudia kufanya kwasababu mwisho wa siku mambo yatakapo kuendea kombo wao watakua wanakula bata kama kawaida mzee wangu

subiri mwisho wa hukumu ndo utajua kama kapotea njia au la. chezea kinana weye!
 
Biashara ya bogaboga safi sana Kinana, itaajiri watanzania wengi, italipa kodi. Biashara ya meno siyo nzuri kwani hutoa ajira kwa watu wachache na huwa hailipi kodi. 'Mhudumu naomba NDOVU BARIDI, huelewi nini sasa mpaka niseme KINANA BARIDI mwenzio naogopa kupelekwa mahakamani milioni 350 mlala hoi nazitowa wapi?'
 
Kinana uki declare interest za kuhusika na Natural Resources za tanzania there you are finish.
Hao Tembo ni ushahidi tosha..Wakikuona tu wanasepa images.jpg
 
makubwa kazi ipo pia tuna mawakili waliobobea chadema watasimamia
 
images


Nadhani huyu jamaa punde si punde atajitokeza kutoa tamko kuwa CHADEMA inahujumiwa. hajui kuwa mwanasiasa mjinga huponzwa na mdomo wake
 
unajua msigwa amezoe kuropoka na kutukana watu hovyo na kuzua tuhuma za uongo kwa kutafuta sifa ambazo hazimstahili na anadhani kila mtu anafaaa kuonewa na kuzushiwa halafu akaachwa.
 
Naamini mahakama itatenda haki.

Hata mm naziamini sana Mahakama zetu!

Kwanza wana sheria wa Kinana wamekosea kwenye kiwango cha pesa alicho omba alipwe;Mahakama Tanzania ziliisha weka muongozo wa kuomba malipo kwenye kesi ya kashfa;hela unayoomba isizidi kipato cha mtu anayeombwa kwa mwaka!

Je Msigwa anapata milion 350 na zaidi kwa mwaka?
 
Hapo 'Msomali' kajitia kitanzi mwenyewe!! Tembo wetu watapumua sasa!?
 
Mi nildhani ungeanza na kuishauri serikali yako DHAIFU kumchunguza Kinana....
View attachment 97518
Kinana Strikes Again
"kinana nionee huruma unatumaliza" ni kama alikuwa akiomba msamaha huyo tembo kwa kupiga magoti.....hakika damu za tembo hawa hazitamuacha jangili kinana na masisiem yake!!!Time will tell.....
 
hoja hapa ni kwamba kinana ni jangili,kwahiyo mawakili wake watuambie siyo jangili kwa vielelezo.Hizo habari kwamba kapata hasara na kuchafuliwa ni rubbish.
 
Yesu akasema, chochote kile ambacho unataka watu wakutendee, penda kuwatendea vivyo.
 
Safi Kinana katafute haki mahakamani. Ndugu zetu hawajui kuwa sheria ni msumeno unakata pande zote wao wakishindwa basi wameonewa wakishinda haki imetendeka mh ni binadamu wa ajabu kweli.
 
Back
Top Bottom