Basi mleta thread ya kwanza ni mhuni anaamua kudanganya jf halafu yeye anaona bonge la ujanja,yuko milembe day.
Habari za uhakika zilizonifikia ni kwamba, Kinana amepata balaa kubwa baada ya mfanyakazi wake wa ndani kumuibia kiasi cha dola elfu 60, taarifa zinasema kuwa kijana huyo mwenye asili ya mkoa wa iringa yuko sasa hivi ktk kituo cha polisi mabatini, na tayari alikuwa ameshanunua gari moja ain ya vitz na pikipiki 3 na nyumba maeneo ya mbagala, gari na pikipiki bado zinashikiliwa na polisi na nyumba bado muuzaji anatafutwa ili arudishe pesa.
Muuzaji wa nyumba ni kijana wa kichaga na ameapa hawezi kurudisha pesa. Kwanini mtu msomi kama yule aweke kiasi kikubwa cha pesa nyumbani kwake?
Kwa uhakika zaidi juu ya suala hili ampigie mkuu wa kituo cha Mabatini hapo Kijitonyama
Kwa taarifa yako, kijana aliyemuibia anaitwa peter daud, na anashikiliwa na polisi kituo cha mabatini leo ni siku ya sita hajafunguliwa kesi wala kupelekwa mahakani.yaani anabanwa pu.bu tu ili atoe pesa mambo yaishe kimya kimya.sasa uzushi uko wapi?KWA MARA NYINGINE TENA, UZUSHI UNAPOGEUZWA ZANA YA KUPAMBANA KISIASA.
Muda mchache uliopita kumekuwepo na taarifa za kutungwa na uzushi ambao umeanzia hapa JF na kuzungushwa katika mitandao mingine ya kijamii k.v facebook na twitter ambazo zinadai Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahaman Kinana amepatwa na mkasa wa kuibiwa kiasi cha dola za kimarekani elfu sitini na mfanyakazi wake wa ndani.
Taarifa hiyo aina ukweli hata chembe, ni uzushi ambao unalenga katika kumchafua na kumjengea tafsir hasi Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, ndugu Kinana. Hakuna mfanyakazi yeyote wa ndani ama mlinzi ambae ametuhumiwa kuiba si tu kwa Kinana lakini hata sehemu nyingine yeyote. Pia hakuna mtuhumiwa yeyote aliyefikishwa katika kituo cha polisi cha mabatini kwa kuhusishwa na wizi wa pesa kiasi hicho kutoka sehemu yeyote na pia hakuna kesi yeyote ambayo imefunguliwa kwa yeyote kuhusiana na shitaka la namna hiyo.
Huu ni uzushi na unapigiwa chapuo na kuchangiwa na watu wenye nia mbaya na wenye mkakati wa kumshambulia katibu mkuu kwa malengo yao binafsi hasa malengo hayo yakihusiana na dhamana ya cheo alichonacho ndugu Kinana yaani Ukatibu Mkuu wa Cham Cha Mapinduzi, hivyo uzushi na uwongo huu una mlengwa wa kisiasa. Ni aibu kubwa kwa mwanasiasa ama chama cha siasa kutumia uzushi, uzandiki na fitina kama silaha yao na mbinu ya kujijengea umaarufu na kujitangaza kwa wananchi.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Wamrudishie dola zake 60 vinginevyo usalama wa tembo utakuwa hatarini
Hata mimi mbavu sina, ha ha haa!Mkuu umenivunja mbavu. ha ha ha haaa!
Hiyo dola elfu 60 ni pesa kidogo sana. Ni kwa ajili ya matumizi madogo madogo ya mheshimiwa. Matumizi ya laki saba mpaka milioni moja kwa siku kwa mheshimiwa ni jambo la kawaida sana. Sasa mlitaka akae na dola ngapi nyumbani kwake??Acheni kupiga kelele kwa kwaaa kwaaa kwaaa kwaaa kwaaa kama kanga wa porini.
halafu, kiuhalisia, huwezi kupata nyumba mbagala chini ya milioni 70. labda aniambie kuwa amenunua kiwanja na msingi. kama ana taarifa zaidi basi atutajie mbagala ipi nyumba hiyo imeuzwa
Wamrudishie dola zake 60 vinginevyo usalama wa tembo utakuwa hatarini
UKWELI. Kijana aliyechukua pesa anaitwa PETER DAUD, na aliyeuza nyumba anaitwa SHIRIMA huyu aliyeiba yuko kituo cha polisi mabatini kijitonyama na leo ni siku ya 6 hajafunguliwa kesi wala kupelekwa mahakani kwa amri ya mkubwa. tembelea kituoni utaona kuna pkpk 2 mpya hazina namba na gari vitz ina namba. Hatubahatishi kama unavyofikiri.na mhuni ni wewe unayetetea usichokijua kwa ajili tu ya tumbo lako.masburi mkubwa weweBasi mleta thread ya kwanza ni mhuni anaamua kudanganya jf halafu yeye anaona bonge la ujanja,yuko milembe day.
Kijana kachota kidogo tu, zilikuwepo nyingi zaidi ya hizo![/QUOTE Ni kweli kabisa.Kama ameweza kununua hizo raslimali patakuwa zimepita siku toka alipoiba.Hiyo inatoa picha kwamba alichota kidogo kutoka katika mzigo uliokuwepo ndo maana hakugundulika haraka.NI MTIZAMO WANGU LAKINI.