Kinana aibiwa nyumbani kwake

Kinana aibiwa nyumbani kwake

Hapo ukute lwakatare aliwatuma vijana wake akina sa8 wakamteke wamlishe sumu walipoona dolari wakatoka kwenye lengo
Mkuu hii 'joke' haichekeshi tena. Tafuta nyingine utuvunje mbavu.
 
Jiheshimu wewe kilaza, CHADEMA inahusikaje hapo. Huwezi kukurupuka hapa na kusema tuhuma za wana CHADEMA bila kutueleza ukweli ukoje. Mmezoea kusema hata UJANGILI wa KInana ni tuhuma za kisiasa huku Tembo 30 wanauwawa kila siku. Acheni hizo bana...

kabdulrahmani kinana ni tishio kwa uhai wa chadema. ndo maana wanahangaika sana kumchafua kwa lengo la kupunguza umaarufu wake. hakika huyu jamaa hawamwezi
 
KWA MARA NYINGINE TENA, UZUSHI UNAPOGEUZWA ZANA YA KUPAMBANA KISIASA.

Muda mchache uliopita kumekuwepo na taarifa za kutungwa na uzushi ambao umeanzia hapa JF na kuzungushwa katika mitandao mingine ya kijamii k.v facebook na twitter ambazo zinadai Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahaman Kinana amepatwa na mkasa wa kuibiwa kiasi cha dola za kimarekani elfu sitini na mfanyakazi wake wa ndani.

Taarifa hiyo aina ukweli hata chembe, ni uzushi ambao unalenga katika kumchafua na kumjengea tafsir hasi Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, ndugu Kinana. Hakuna mfanyakazi yeyote wa ndani ama mlinzi ambae ametuhumiwa kuiba si tu kwa Kinana lakini hata sehemu nyingine yeyote. Pia hakuna mtuhumiwa yeyote aliyefikishwa katika kituo cha polisi cha mabatini kwa kuhusishwa na wizi wa pesa kiasi hicho kutoka sehemu yeyote na pia hakuna kesi yeyote ambayo imefunguliwa kwa yeyote kuhusiana na shitaka la namna hiyo.

Huu ni uzushi na unapigiwa chapuo na kuchangiwa na watu wenye nia mbaya na wenye mkakati wa kumshambulia katibu mkuu kwa malengo yao binafsi hasa malengo hayo yakihusiana na dhamana ya cheo alichonacho ndugu Kinana yaani Ukatibu Mkuu wa Cham Cha Mapinduzi, hivyo uzushi na uwongo huu una mlengwa wa kisiasa. Ni aibu kubwa kwa mwanasiasa ama chama cha siasa kutumia uzushi, uzandiki na fitina kama silaha yao na mbinu ya kujijengea umaarufu na kujitangaza kwa wananchi.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
 
basi mwenye thread atoe upuuzi wake....amlete yuleeeeeeeeeeee 'msomari'
 
ndio maana shilingi yetu inashuka thamani kila siku,viongozi wa ccm wanathamini dola kuliko shilingi hata adam malima sii aliibiwa dola 4000 na changu morogoro!dola 60,000 nyumbani za nini kama sio za kulipia ma deal ya chap chap?mwaka 1983 dola 1 ilikuwa sawa na shilingi 12.leo ni shilingi 1625

Sasa ndugu yangu soko kubwa la pembe za ndovu ni Vietnam na Hong Kong unategemea huko watalipana kwa pesa zetu za madafu hizi? Lamawa nyingine mnazompa mzee wetu mnamuonea jamani.
 
kwanza hicho kituo cha mabatini sina uhakika ni kipi. maana hapa songea tuna kituo cha polisi cha mabatini. sijui ndo hicho? hiyo namba ya simu mbona hujaiweka ili tuwapigie tupate ufafanuzi wa hilo?
Mkuu unatumia masburi kufikiri? kama unajua kuandika iweje usijue kusoma. nimesema mabatini kijitonyama, au songea napo kuna kijitonyama?
 
...........kijana huyo mwenye asili ya mkoa wa iringa.......:coffee:
 
Afadhali!! Huo 'mzigo' umepona. Angalau hao wanyama wana hata wiki mbili za kuendelea kuishi.
 
KWA MARA NYINGINE TENA, UZUSHI UNAPOGEUZWA ZANA YA KUPAMBANA KISIASA.

Muda mchache uliopita kumekuwepo na taarifa za kutungwa na uzushi ambao umeanzia hapa JF na kuzungushwa katika mitandao mingine ya kijamii k.v facebook na twitter ambazo zinadai Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahaman Kinana amepatwa na mkasa wa kuibiwa kiasi cha dola za kimarekani elfu sitini na mfanyakazi wake wa ndani.

Taarifa hiyo aina ukweli hata chembe, ni uzushi ambao unalenga katika kumchafua na kumjengea tafsir hasi Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, ndugu Kinana. Hakuna mfanyakazi yeyote wa ndani ama mlinzi ambae ametuhumiwa kuiba si tu kwa Kinana lakini hata sehemu nyingine yeyote. Pia hakuna mtuhumiwa yeyote aliyefikishwa katika kituo cha polisi cha mabatini kwa kuhusishwa na wizi wa pesa kiasi hicho kutoka sehemu yeyote na pia hakuna kesi yeyote ambayo imefunguliwa kwa yeyote kuhusiana na shitaka la namna hiyo.

Huu ni uzushi na unapigiwa chapuo na kuchangiwa na watu wenye nia mbaya na wenye mkakati wa kumshambulia katibu mkuu kwa malengo yao binafsi hasa malengo hayo yakihusiana na dhamana ya cheo alichonacho ndugu Kinana yaani Ukatibu Mkuu wa Cham Cha Mapinduzi, hivyo uzushi na uwongo huu una mlengwa wa kisiasa. Ni aibu kubwa kwa mwanasiasa ama chama cha siasa kutumia uzushi, uzandiki na fitina kama silaha yao na mbinu ya kujijengea umaarufu na kujitangaza kwa wananchi.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

tutajuaje kama wewe sio Muongo na uko unajaribu kumtetea mzee wa tembo ili wananchi tusihoji midola yote hiyo ilikuwa inafanya nini ndani ya nyumba yake... ???
 
Tembo bi wetu na pesa ni yetu.. Hakuna kesi hapo
 
Habari za uhakika zilizonifikia ni kwamba, Kinana amepata balaa kubwa baada ya mfanyakazi wake wa ndani kumuibia kiasi cha dola elfu 60, taarifa zinasema kuwa kijana huyo mwenye asili ya mkoa wa iringa yuko sasa hivi ktk kituo cha polisi mabatini, na tayari alikuwa ameshanunua gari moja ain ya vitz na pikipiki 3 na nyumba maeneo ya mbagala, gari na pikipiki bado zinashikiliwa na polisi na nyumba bado muuzaji anatafutwa ili arudishe pesa.

Muuzaji wa nyumba ni kijana wa kichaga na ameapa hawezi kurudisha pesa. Kwanini mtu msomi kama yule aweke kiasi kikubwa cha pesa nyumbani kwake?

Kwa uhakika zaidi juu ya suala hili ampigie mkuu wa kituo cha Mabatini hapo Kijitonyama

Jamani hili ni changa la Macho.......! jamaa anatuchezea mchezo wa kitoto, ili muachane na hoja ya MENO YA TEMBO, mhamie kwenye hii issue ambayo haina kichwa wala miguuu.......
Turudi kwenye hoja ya "TEMBO WETU WANAKWISHA...."
 
tuna haki ya kujua maana huu ni upotoshaji mkubwa. kama wewe ndo mleta uzi basi tufafanulie zaidi maana kuna mwingine anasema kuwa aliyeibiwa ni mkazi wa tegeta kwa ndevu
Kijana aliyeuza nyumba anaitwa SHIRIMA. Endeleeni kutoa tu mapovu, maana kila la ukwali mnapinga. kama una simu piga kituoni kwa sababu kijana hajapata dhamana leo ni siku ya 6
 
thread za uzushi na uwongo uliokithiri wenye kulenga kumchafua mtu na kuishusha hadhi yake zinaihribia JF na kuonekana na moja miongoni mwa medias zinazotumiwa kimkakati katika kuchafua viongozi wa Chama na serikali. Jambo hili ni baya na linaloleta tafsir mbaya mbele ya jamii, ni vibaya mno media kutumika kwa maslahi ya mtu au kikundi. Mods thread hizi za namna hii kwanini zipewe nafasi hapa JF..?

Kama umeshajiridhisha pasi na saka kuwa JF ni jukwaa la uzushi na uongo kwa nini mnazidi kulundikana humu si muwaache wazushi na uzushi wao nanyi muanzishe LumumbaForum ambayo itakuwa inadili na habari za ukweli na uhakika tu au hakuna wataalamu wa IT pale ofisi ndogo ya chama? Nenda kasimamie kombe lako uliloanzisha lisije kupoteza umaarufu ukaukosa tena udiwani kwa sababu ya kutokwa povu Jf.
 
Mkuu unatumia masburi kufikiri? kama unajua kuandika iweje usijue kusoma. nimesema mabatini kijitonyama, au songea napo kuna kijitonyama?

hiyo kijitonyama ndo unaitaja sasa baada ya kushikwa pabaya. by the way sina haja ya kujibishana na mtu ambaye uwezo wake wa kufikiri ni finyu na hafifu
 
thread za uzushi na uwongo uliokithiri wenye kulenga kumchafua mtu na kuishusha hadhi yake zinaihribia JF na kuonekana na moja miongoni mwa medias zinazotumiwa kimkakati katika kuchafua viongozi wa Chama na serikali. Jambo hili ni baya na linaloleta tafsir mbaya mbele ya jamii, ni vibaya mno media kutumika kwa maslahi ya mtu au kikundi. Mods thread hizi za namna hii kwanini zipewe nafasi hapa JF..?
Umempigia mkuu wa kituo Mabatini akakuambia ni uongo? Mbona mnamtetea sana Kinana kwa kila kinachosemwa dhidi yake bila hata kuchunguza? Kuwa na fedha sio jambo baya,ila kuweka fedha nyingi nyumbani badala ya Bank ndio shangao. Viongozi haohao ndio wanahimiza watu waweke fedha bank kisha wao wana weka nyingi nyumbani kwa nini? Ana biashara gani ya kuhitaji cash yote hiyo kukaa nyumbani?
Hili linaleta mashaka kuwa huwa anazo biashara zisizo halali.
 
tuna haki ya kujua maana huu ni upotoshaji mkubwa. kama wewe ndo mleta uzi basi tufafanulie zaidi maana kuna mwingine anasema kuwa aliyeibiwa ni mkazi wa tegeta kwa ndevu

Kinana wa Tembo haishi Tegeta kwa Ndevu
 
..... na nyumba bado muuzaji anatafutwa ili arudishe pesa.

Kijana aliyeuza nyumba anaitwa SHIRIMA. Endeleeni kutoa tu mapovu, maana kila la ukwali mnapinga. kama una simu piga kituoni kwa sababu kijana hajapata dhamana leo ni siku ya 6

Sasa kwa nini wanataka huyo Shirima arudishe pesa?

Kwani alishirikiana na huyo mtuhumiwa kuiba hizo pesa?
 
Kijana aliyeuza nyumba anaitwa SHIRIMA. Endeleeni kutoa tu mapovu, maana kila la ukwali mnapinga. kama una simu piga kituoni kwa sababu kijana hajapata dhamana leo ni siku ya 6

huyo shirima anakaa wapi na tutajie namba ya hiyo nyumba aliyouza. halafu tutajie na jina la mnunuzi kama wewe wasema kweli. otherwise jiandae kukatwa midomo na vidole siku ya hukumu kwa mikasi ya moto kwa kusema na kuandika uongo
 
Back
Top Bottom