Mwanafunzi mtoro
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 223
- 797
Natanguliza salamu kwa unyenyekevu kabisa.
Juzi kati nilienda benki nje kwenye ATM kuuliza salio. Salio lilionesha laki kadhaa na elfu kumi. Sikutoa hata mia, nikajisemea moyoni hata kesho naweza kuzitoa kwanza zipo sehemu salama.
Siku iliyofuata nilienda tena ATM niliona bora nitoe pesa zote . Chakushangaza ikagoma nikaona acha niiache hiyo teni labda tozo inasababisha hata hiyo elfu kumi isitoke lakini napo hola.
Nikaona ngoja niulize salio, nilikuta elfu 10 na zaidi haipo. Nikatoa iliyopo na chenchi nilienda kutolea kwa wakala. Hapo imepungua kana elfu 13 hivi.
Basi nikapuuzia nikiamini labda ni mambo ya kitaalamu hayo haina haja kuwasumbua wataalamu. Niliamini huenda labda nilichukua bank statement ndio imekatwa sasa.
Sasa jana kuna mtu alitaka kunitumia vihela kidogo nifanye matumizi yangu ilikuwa kama laki kamili. Basi nikamweleza asiweke mpesa kutokana na mambo ya tozo. Basi nikampa acc. akaniwekea laki kamili.
Asubuhi nilipoamka nikasema sasa nikatoe. Ile kubofya laki ikagoma nkadhania kwakuwa pesa ilikuwa laki lazima igome. Nikatoa 90 huyo mbele.
Nikaenda hadi kwa wakala wa benk, nikamwambia naomba nitoe efu 7 ikawa hola. Jaribu elfu 6 hola jaribu elfu 5 hola jaribu elfu 4 hola alooooh. Kujaribu elfu 3 ikakubali.
Sasa swali nikajiuliza tangu lini gharama ya kutoa elfu 90 ikawa elfu 6, elfu 6 na miatano au 7 ??
Nikahisi benk wananizoea sasa ngoja niwafuate . Hapo ndio nilipewa maelezo nikachoka kabisa.
Hapo ndio niliona kumbe hawakuchukua benk yani niliambiwa sijui kuna money nini hiyo ya serikali walitangaza kumbe. Yaani nilikuta wamekata pesa hovyo hovyo timtim kama geto la chizi.
Dokezo 1
Kabla yangu juzi nilikuta dada flani nje ya benki analalamika elfu 25 hajui imekatwa ya nini. Nilihisi hayanihusu ni ishu binafsi kumbe ningezingatia maumivu yake huwenda ningeshtuka kupitisha pesa benki sio salama tena.
Dokezo 2
Wakati naeleweshwa kuhusu hayo makato mapya ghafla sura ya Ndugai ikanijia mbele yangu. Ndipo nilianza kuelewa kuwa kumbe aliposema kuna siku nchi itapigwa mnada hakumanisha kwamba raia tutafukuzwa bali tutaishi kwa mateso kama tupo nchi ya ugenini. Binafsi namuomba msamaha bwana ndugai . Hakika tulilewa mvinyo wa awamu mpya.
Twendelee
Sasa naanza kuhisi hata hizi post kodi kuna siku watu watakuja kusaga meno na kilio kikubwa . Lakini yote ya yote tumejifunza mara nyingi tumeona "Mungu huingilia kati popote kwenye malalamiko yaliyozidi". Anapolaumiwa kiongozi basi analaumiwa Mungu kwa kuwa wengi huamini uongozi hutoka kwa Mungu.
Juzi kati nilienda benki nje kwenye ATM kuuliza salio. Salio lilionesha laki kadhaa na elfu kumi. Sikutoa hata mia, nikajisemea moyoni hata kesho naweza kuzitoa kwanza zipo sehemu salama.
Siku iliyofuata nilienda tena ATM niliona bora nitoe pesa zote . Chakushangaza ikagoma nikaona acha niiache hiyo teni labda tozo inasababisha hata hiyo elfu kumi isitoke lakini napo hola.
Nikaona ngoja niulize salio, nilikuta elfu 10 na zaidi haipo. Nikatoa iliyopo na chenchi nilienda kutolea kwa wakala. Hapo imepungua kana elfu 13 hivi.
Basi nikapuuzia nikiamini labda ni mambo ya kitaalamu hayo haina haja kuwasumbua wataalamu. Niliamini huenda labda nilichukua bank statement ndio imekatwa sasa.
Sasa jana kuna mtu alitaka kunitumia vihela kidogo nifanye matumizi yangu ilikuwa kama laki kamili. Basi nikamweleza asiweke mpesa kutokana na mambo ya tozo. Basi nikampa acc. akaniwekea laki kamili.
Asubuhi nilipoamka nikasema sasa nikatoe. Ile kubofya laki ikagoma nkadhania kwakuwa pesa ilikuwa laki lazima igome. Nikatoa 90 huyo mbele.
Nikaenda hadi kwa wakala wa benk, nikamwambia naomba nitoe efu 7 ikawa hola. Jaribu elfu 6 hola jaribu elfu 5 hola jaribu elfu 4 hola alooooh. Kujaribu elfu 3 ikakubali.
Sasa swali nikajiuliza tangu lini gharama ya kutoa elfu 90 ikawa elfu 6, elfu 6 na miatano au 7 ??
Nikahisi benk wananizoea sasa ngoja niwafuate . Hapo ndio nilipewa maelezo nikachoka kabisa.
Hapo ndio niliona kumbe hawakuchukua benk yani niliambiwa sijui kuna money nini hiyo ya serikali walitangaza kumbe. Yaani nilikuta wamekata pesa hovyo hovyo timtim kama geto la chizi.
Dokezo 1
Kabla yangu juzi nilikuta dada flani nje ya benki analalamika elfu 25 hajui imekatwa ya nini. Nilihisi hayanihusu ni ishu binafsi kumbe ningezingatia maumivu yake huwenda ningeshtuka kupitisha pesa benki sio salama tena.
Dokezo 2
Wakati naeleweshwa kuhusu hayo makato mapya ghafla sura ya Ndugai ikanijia mbele yangu. Ndipo nilianza kuelewa kuwa kumbe aliposema kuna siku nchi itapigwa mnada hakumanisha kwamba raia tutafukuzwa bali tutaishi kwa mateso kama tupo nchi ya ugenini. Binafsi namuomba msamaha bwana ndugai . Hakika tulilewa mvinyo wa awamu mpya.
Twendelee
Sasa naanza kuhisi hata hizi post kodi kuna siku watu watakuja kusaga meno na kilio kikubwa . Lakini yote ya yote tumejifunza mara nyingi tumeona "Mungu huingilia kati popote kwenye malalamiko yaliyozidi". Anapolaumiwa kiongozi basi analaumiwa Mungu kwa kuwa wengi huamini uongozi hutoka kwa Mungu.