6 Pack
JF-Expert Member
- Apr 17, 2022
- 1,826
- 4,074
Niaje waungwana?
Wazungu baada ya kuona wamefanikiwa kutawala sehemu kubwa ya dunia haswa haswa katika bara zima la Afrika, wakaona kuwa hata uongo wao pia watakaoleta kwa watawaliwa utaweza kuishi milele, bila kujua kwamba zama zinabadilika na akili za watawaliwa nazo pia zinabadilika.
1. Kwanza wazungu walitudanganya kuwa wanakuja kutukomboa kiuchumi na kiroho, kumbe nyuma ya pazia lengo lilikuwa ni kututawala, kumiliki ardhi yetu na kila kilichopo katika nchi zetu.
2. Pili walitudanganya kuwa binadamu wa kwanza au wa kale walikuwa ni manyani, lakini hapo hapo kupitia vitabu vitakatifu vya dini wakatuambia kuwa binadamu wa kwanza alikuwa ni binadam wa kawaida ambae jina lake ni Adam.
cha kushangaza katika vitabu vinavyoonesha kuwa binadamu wa kwanza walikuwa nyani, utakuta waliochorwa ni watu weusi, na vile vinavyoonesha kuwa binadam wa kwanza alikuwa Adam utakuta amechorwa mzungu, hivyo ni wazi kuwa binadam wote tulikuwa ni binadam wa kawaida kutoka kwa baba yetu Adam, hao nyani tulioambiwa ilikuwa ni uongo mahususi uliotengenezwa kwa malengo yao watawala (wazungu)
3. Tatu wanadanganya kuwa pale Mashariki ya kati nchi yenye nguvu zaidi za kijeshi ni Israel, lakini wengi tumeshuhudia kwamba Israel haina tofauti na Ukraine, kwamba kila inapotaka kupigana na adui yake, au hata kikundi cha vijana wasiozidi hata 20,000 kama vile Hamas lazima waombe msaada wa silaha kutoka Marekani, huku UK na EU nao wakiipa kwa njia ya kimya kimya ili kupambana na kakundi hako.
Bora hata Ukraine inapambana na taifa ambali ni la kwanza kwa ukubwa duniani, taifa ambalo Ukraine inaingia zaidi ya mara 10, lakini pia ni la pili kwa nguvu za kijeshi duniani, hivyo kutokana na udogo wake na pia utoauti wa nguvu za kijeshi, ina haki ya kuomba msaada kutoka katika nchi nyingine. Lakini Israel inaomba msaada wa kifedha na silaha hata pale inapopambana na kikundi cha watu wachache wasiofika hata elfu 50 ambacho sio nchi, sasa inawezaje kuwa taifa lenye nguvu kuliko nchi zote za eneo hilo?
Mbona tukifuata uhalisia wa kweli bila kutanguliza mihemko ya kipropaganda za magharibi ni kama vile Israel haiwezi kufua dafu hata mbele ya mziki wa Iran kijeshi, japo nchi hiyo ina vikwazo lukuki vilivyodumu kwa zaidi ya miaka 70. Kama vikundi vidogo vidogo vinavyodhaminiwa na Iran iliyowekewa vikwazo kwa takribani miaka 70 Hezbollah, Hamas na vinaitoa kamasi Israel inayodhaminiwa kijeshi na kifedha na Marekani kwa zaidi ya miaka 80 tena bila kikwazo hata kimoja, je hiyo ndio ya kuuita yenye nguvu hapo Mashariki ya kati zaidi ya nchi zingine? Kuna kikundi kidogo tu cha vijana kadhaa kilichopewa silaha mbili tatu na Iran hapo Yemen, kimesababisha nchi kubwa duniani zaidi ya 10 kuingia baharini kwenda kupambana nacho. Hivyo kudai kuwa Israeli ni taifa lenye nguvu kwa sasa, kwakweli ni uongo wa dhahiri ambao kwa dunia ya leo watu wanaanza kuushtukia kutokana na kile kinachoendelea katika eneo hilo.
Fikiria hiyo miaka zaidi ya 70 ambayo muisrael anapewa misaada ya kijeshi na kifedha na Marekani pamoja na vibaraka wa magharibi, kama pia ingetumika kutoiwekea vikwazo Iran hali ingekuaje, bado wangeendelea kudanganya hivi hivi au wangeongea ukweli kwa sababu ingekuwa ngumu kuuficha ukweli huo?
4. Walidanganya kuwa Russia ni nchi hatari kwa usalama na amani ya dunia, japo Russia ni wazungu wenzao, lakini ukweli ni kwamba wazungu wa nchi za West ndio wanaoongoza kwa kuhatarisha usalama na amani katika nchi za wenzao. Wengi tuliona jinsi wafaransa walivyopachika wavaa kobaz huko Mali, Niger, na kwengineko ili aweze kutumia mwanya huo kuiba rasilimali za nchi hizo kupitia maeneo yale ambayo serikali haiwezi kuyadhibiti tena. Hata miaka kadhaa iliyopita Msumbiji iligundua kuwa katika eneo la kusini mwa nchi yake kuna utajiri mkubwa wa gesi, hivyo waliingia mkataba na kampuni fulan ya kifaransa kwa lengo la kuja kuchimba gesi hiyo kwa makubaliano maalum, bila kujua kwamba nchi hiyo ya kusini mwa Afrika inakaribisha nyoka katika ardhi yake.
Miezi michache tu baada ya wafaransa kuingia eneo la kazi na kuisoma vizuri ramani, wakaunda kikundi cha wavaa kobaz kama ilivyozoea kufanya katika nchi Mali, Niger, Gabon nk. Lengo la kuunda kikundi kile ni kutaka lile eneo lisitawalike na kampuni yao ijifanye inakimbia kutokana na sababu za kiusalama, kumbe nyuma ya pazia wawe bado wapo wanachota gesi hiyo watakavyo huku wakiwapa silaha na hela ya kula viongozi wa wavaa kobazi ambao wanajua kile kinachoendelea katika eneo hilo. Hivyo kusema kuwa Russia ni nchi hatari kwa usalama na amani ya dunia ni uongo mtupu wanaojaribu kutudanganya sisi watawaliwa ambao wanahisi hatuwezi kujua lolote.
Uongo wao ni mwingi, siwezi kuuorodhesha wote, ila wajue kwamba watawaliwa tumeshaamka, sio kila tango pori watakaloturushia sisi tutalimeza bila kulimung'unya ili kujiridhisha kuwa ni lenyewe kweli au tango la miba.
Wazungu baada ya kuona wamefanikiwa kutawala sehemu kubwa ya dunia haswa haswa katika bara zima la Afrika, wakaona kuwa hata uongo wao pia watakaoleta kwa watawaliwa utaweza kuishi milele, bila kujua kwamba zama zinabadilika na akili za watawaliwa nazo pia zinabadilika.
1. Kwanza wazungu walitudanganya kuwa wanakuja kutukomboa kiuchumi na kiroho, kumbe nyuma ya pazia lengo lilikuwa ni kututawala, kumiliki ardhi yetu na kila kilichopo katika nchi zetu.
2. Pili walitudanganya kuwa binadamu wa kwanza au wa kale walikuwa ni manyani, lakini hapo hapo kupitia vitabu vitakatifu vya dini wakatuambia kuwa binadamu wa kwanza alikuwa ni binadam wa kawaida ambae jina lake ni Adam.
cha kushangaza katika vitabu vinavyoonesha kuwa binadamu wa kwanza walikuwa nyani, utakuta waliochorwa ni watu weusi, na vile vinavyoonesha kuwa binadam wa kwanza alikuwa Adam utakuta amechorwa mzungu, hivyo ni wazi kuwa binadam wote tulikuwa ni binadam wa kawaida kutoka kwa baba yetu Adam, hao nyani tulioambiwa ilikuwa ni uongo mahususi uliotengenezwa kwa malengo yao watawala (wazungu)
3. Tatu wanadanganya kuwa pale Mashariki ya kati nchi yenye nguvu zaidi za kijeshi ni Israel, lakini wengi tumeshuhudia kwamba Israel haina tofauti na Ukraine, kwamba kila inapotaka kupigana na adui yake, au hata kikundi cha vijana wasiozidi hata 20,000 kama vile Hamas lazima waombe msaada wa silaha kutoka Marekani, huku UK na EU nao wakiipa kwa njia ya kimya kimya ili kupambana na kakundi hako.
Bora hata Ukraine inapambana na taifa ambali ni la kwanza kwa ukubwa duniani, taifa ambalo Ukraine inaingia zaidi ya mara 10, lakini pia ni la pili kwa nguvu za kijeshi duniani, hivyo kutokana na udogo wake na pia utoauti wa nguvu za kijeshi, ina haki ya kuomba msaada kutoka katika nchi nyingine. Lakini Israel inaomba msaada wa kifedha na silaha hata pale inapopambana na kikundi cha watu wachache wasiofika hata elfu 50 ambacho sio nchi, sasa inawezaje kuwa taifa lenye nguvu kuliko nchi zote za eneo hilo?
Mbona tukifuata uhalisia wa kweli bila kutanguliza mihemko ya kipropaganda za magharibi ni kama vile Israel haiwezi kufua dafu hata mbele ya mziki wa Iran kijeshi, japo nchi hiyo ina vikwazo lukuki vilivyodumu kwa zaidi ya miaka 70. Kama vikundi vidogo vidogo vinavyodhaminiwa na Iran iliyowekewa vikwazo kwa takribani miaka 70 Hezbollah, Hamas na vinaitoa kamasi Israel inayodhaminiwa kijeshi na kifedha na Marekani kwa zaidi ya miaka 80 tena bila kikwazo hata kimoja, je hiyo ndio ya kuuita yenye nguvu hapo Mashariki ya kati zaidi ya nchi zingine? Kuna kikundi kidogo tu cha vijana kadhaa kilichopewa silaha mbili tatu na Iran hapo Yemen, kimesababisha nchi kubwa duniani zaidi ya 10 kuingia baharini kwenda kupambana nacho. Hivyo kudai kuwa Israeli ni taifa lenye nguvu kwa sasa, kwakweli ni uongo wa dhahiri ambao kwa dunia ya leo watu wanaanza kuushtukia kutokana na kile kinachoendelea katika eneo hilo.
Fikiria hiyo miaka zaidi ya 70 ambayo muisrael anapewa misaada ya kijeshi na kifedha na Marekani pamoja na vibaraka wa magharibi, kama pia ingetumika kutoiwekea vikwazo Iran hali ingekuaje, bado wangeendelea kudanganya hivi hivi au wangeongea ukweli kwa sababu ingekuwa ngumu kuuficha ukweli huo?
4. Walidanganya kuwa Russia ni nchi hatari kwa usalama na amani ya dunia, japo Russia ni wazungu wenzao, lakini ukweli ni kwamba wazungu wa nchi za West ndio wanaoongoza kwa kuhatarisha usalama na amani katika nchi za wenzao. Wengi tuliona jinsi wafaransa walivyopachika wavaa kobaz huko Mali, Niger, na kwengineko ili aweze kutumia mwanya huo kuiba rasilimali za nchi hizo kupitia maeneo yale ambayo serikali haiwezi kuyadhibiti tena. Hata miaka kadhaa iliyopita Msumbiji iligundua kuwa katika eneo la kusini mwa nchi yake kuna utajiri mkubwa wa gesi, hivyo waliingia mkataba na kampuni fulan ya kifaransa kwa lengo la kuja kuchimba gesi hiyo kwa makubaliano maalum, bila kujua kwamba nchi hiyo ya kusini mwa Afrika inakaribisha nyoka katika ardhi yake.
Miezi michache tu baada ya wafaransa kuingia eneo la kazi na kuisoma vizuri ramani, wakaunda kikundi cha wavaa kobaz kama ilivyozoea kufanya katika nchi Mali, Niger, Gabon nk. Lengo la kuunda kikundi kile ni kutaka lile eneo lisitawalike na kampuni yao ijifanye inakimbia kutokana na sababu za kiusalama, kumbe nyuma ya pazia wawe bado wapo wanachota gesi hiyo watakavyo huku wakiwapa silaha na hela ya kula viongozi wa wavaa kobazi ambao wanajua kile kinachoendelea katika eneo hilo. Hivyo kusema kuwa Russia ni nchi hatari kwa usalama na amani ya dunia ni uongo mtupu wanaojaribu kutudanganya sisi watawaliwa ambao wanahisi hatuwezi kujua lolote.
Uongo wao ni mwingi, siwezi kuuorodhesha wote, ila wajue kwamba watawaliwa tumeshaamka, sio kila tango pori watakaloturushia sisi tutalimeza bila kulimung'unya ili kujiridhisha kuwa ni lenyewe kweli au tango la miba.