wamemnanga kule kwa mange mpaka nikajisikia vibaya
atafute pesa sasa atulie kashazalilishwa sana
ukitaka kumpata kirahisi mdada wa bongo we jifanye tu foreigner
hawa kinadada wanaojidai wako independent mara nyingi inawacost. Ukweli ni kwamba mwanamke anakuwa hatumiki kwenye mapenzi pale tu kunapokuwa na mapenzi ya kweli na ndoa takatifu. Hii mambo nyingine watu tunafanya mwanamke anatumika ila sasa kwa kuwa wanajifanya vichwa ngumu ngoja waendelee kuliwa.Haya mapenzi ya kumpa boifrendi hela huwa siyaelewagi mie
Basi wameamua hao wacameroon, me nlikutana na mmoja Bank..Wacha aning'ang'anie....na vile mtoto nlikuwa nimetupia ushungi akaja na gia kali sana ya ndoa...
Bahati nzuri sijawahi kuwaza kuolewa na foreigner even mmakonde mwenzangu wa Msumbiji....tutabanana huku huku uzaramoni....
Cha ajabu katika Chating nikamuuliza unaishi wapi? Mara anambie Kinondoni, mara Magomeni, mara Kariakoo...mwishowe akafunguka eti anataka aje aishi kwangu....Mwee hapo me mwenyewe nlikuwa naishi hostel...!
Nikaona hapa ni shida tu, nikampotezea...halafu mtongozo wenyewe ulikuwa kwa kizungu ndo kabisaa nikaona ananichosha kunihangaisha na dictionary...
Wadada tuwe makini sana, jamaa wameamua...!
Mi nilimpata mmoja baada ya kufahamiana siku 3 tu kasema he has been robbed hela ya pango! Hahaaa nilimpa pole nikamwambia kesho nitamsaidia ili asifukuzwe!
The next day nikampigia simu nampelekea hela ya pango! Baada ya 45 minutes nikampigia I have been robbed kwenye traffic lights! Guess what ahadi za kunioa zikayeyuka! Chattings zikaisha zote! Not a foreigner ni mbongo mwenzangu tu huyu! So wadada ukiona mwanaume matonya halafu anajifanya yupo serious anatangaza ndoa mchunguze!
Women decide with their hearts not their minds na ndio maana tunatakiwa kuwalinda ninyi sema ndio hivyo ubishi wenu tu.hapa wadada wengi tutajifanya ohh mie nisingeweza ujinga kama huo. i suggest to stop judging the lady,
lakini amini nawaambieni wadada wengi wakikolea katika mapenzi wako very weak and wanaweza kuamua mambo mengi ambayo baadae hujuta mtoa mapenzi akishapunguza mapenzi kwake.
huwa na hisia ya kwa vile ananipenda kwa dhati na kuniridhisha kwa nini nisimpe? na ndio hichi kwenye ndoa nyingi mama anaumia sana na majukumu ya nyumbani kwa uvumilivu haswa baba akishaonesha kumpetipeti japo kidogo halafu akaomba msaada kutoka kwa mama mamma hutoa masikini bila kinyongo.
tehe tehe tehe tehe watu wanapenda mteremko true luv imekuwa hadimu kama soda za alvaro
Usimpe hela kama ana shida sana akamuombe baba yake mzazi. Kwani wewe ndio umemleta mjini au bush kama bado mko huko?Hivi kuhonga maana yake ni nini? Nijuavyo mimi kuhonga ni pale unampa mtu pesa haina hata sababu.....unataka tu akupende. Lakini kuna wakati mtu anaweza kuwa na shida ya muhimu sana na hana hela kwa siku hiyo....utamuacha mtu wako aaidhirike simply bcoz hutaki 'kuhonga'?
Women decide with their hearts not their minds na ndio maana tunatakiwa kuwalinda ninyi sema ndio hivyo ubishi wenu tu.
hahahaha hii kali sanahahaha watakoma mwaka huu, pole yake kuna rafiki yangu Alipata mnaigeria yule kaka alijifanya ni mfanya biashara na akawa anatuletea vitenge kutoka kwako tukajua kweli, ila baadae mi nilimstukia kuna sehemu nilimfuma anaongea kiswahili kizuri sana wakati akiwa na rafiki yangu anajifanya kiswahili hakipandi, mambo yakaenda mpaka akazaliwa mtoto akapewa jina la kikwao, mwanamke alikuwa anaamini kama vile anavyowaona wanaigeria kwenye sinema zao akaona na yeye mambo yake yatakuwa safi, ikafikia wakati wa kujitambulisha mwanaume akadai ndugu zake hawawezi kuja watakuja kwenye ndoa, wakwe wakaweka ngumu ikabidi akawatoe huko walipo, kumbe yule bwana alizaliwa Naigeria tu, ila ni mtanzania kakulia huku kasoma huku na kwao ni sinza mapambano na hana kazi wala nini vitenge sijui alikuwa anaiba wapi. wasichana wanabidi wawe makini sana hali ya maisha imekuwa ngumu
Ila viashiria huwa vipo sema ndio hivyo hawa dada zetu ndivyo walivyo anyway. Wanaamua kwa mioyo sio akili.Omba Mungu yasikukute wewe hujakutana na hawa wacameroon nakwambia..
Anaanza kwa kukupa wewe wanajifanya high class kula hotel kubwa na watu wa international business.
Ata invest muda wake hata miezi mitatu siku atakuja anakwambia kuna container lake limekamatwa anahitaji milion 7 wewe hutahisi kweli na kwa jinsi ulivyoongopewa huwezi hisi kama ni mtu wa kukimbia na milion 7. Ukimpa ndo sahau
Ukitulia kwa Mungu huwezi kufika huku. Tatizo tunadhani kuwa tunayajua sana maisha kuliko huyo Mungu aliyeumba.Aisee Matola kuna kughafirika....af kuna mazingira akili haiwezi hata kusoma mchezo maana mwenyewe anakuwa kajiandaa haswaa. Tukitulia kwa Mungu tutapona tu
Zipo zipo za kutumia hapa na pale, za kununua gari na kiwanja ndo hamna tu.