Basi wameamua hao wacameroon, me nlikutana na mmoja Bank..Wacha aning'ang'anie....na vile mtoto nlikuwa nimetupia ushungi akaja na gia kali sana ya ndoa...
Bahati nzuri sijawahi kuwaza kuolewa na foreigner even mmakonde mwenzangu wa Msumbiji....tutabanana huku huku uzaramoni....
Cha ajabu katika Chating nikamuuliza unaishi wapi? Mara anambie Kinondoni, mara Magomeni, mara Kariakoo...mwishowe akafunguka eti anataka aje aishi kwangu....Mwee hapo me mwenyewe nlikuwa naishi hostel...!
Nikaona hapa ni shida tu, nikampotezea...halafu mtongozo wenyewe ulikuwa kwa kizungu ndo kabisaa nikaona ananichosha kunihangaisha na dictionary...
Wadada tuwe makini sana, jamaa wameamua...!
hahahahaha inaitwa nipe nikupe
Matapeli ni weng tu wabongo na wagen
Ivi inakuweje tugegedane afu hela zangu tna nikakope nikupe
Hii akili ya huyu Dada nadhan ndo mapenz nivuruge kumbe anajivuruga mwenyewe
hahaha watakoma mwaka huu, pole yake kuna rafiki yangu Alipata mnaigeria yule kaka alijifanya ni mfanya biashara na akawa anatuletea vitenge kutoka kwako tukajua kweli, ila baadae mi nilimstukia kuna sehemu nilimfuma anaongea kiswahili kizuri sana wakati akiwa na rafiki yangu anajifanya kiswahili hakipandi, mambo yakaenda mpaka akazaliwa mtoto akapewa jina la kikwao, mwanamke alikuwa anaamini kama vile anavyowaona wanaigeria kwenye sinema zao akaona na yeye mambo yake yatakuwa safi, ikafikia wakati wa kujitambulisha mwanaume akadai ndugu zake hawawezi kuja watakuja kwenye ndoa, wakwe wakaweka ngumu ikabidi akawatoe huko walipo, kumbe yule bwana alizaliwa Naigeria tu, ila ni mtanzania kakulia huku kasoma huku na kwao ni sinza mapambano na hana kazi wala nini vitenge sijui alikuwa anaiba wapi. wasichana wanabidi wawe makini sana hali ya maisha imekuwa ngumu
Whether umekopa benki,umechukua uliyohongwa na mwenzie,umechota akiba yako....suala si linabaki palepale UMEMPA?
Mungu hausiki na ujinga wa binadamu, amekupa vyote akili na ufahamu ukishindwa kuvitumia ni juu yako mwenyewe.
Kabisa yan hata mi waga nashindwa kuwaelewa wanawake wenzangu cjui huaga tunawaza nn
Kuna dada tuko naye ofisini, sasa huku na huku akapata mchumba kutoka West Africa, huyu mchumba anadai amesoma Russia na sijui alikuwa anafanya kazi gani hapa Bongo, maana hata dada mwenyewe ukimuuliza haelewi elewi. Harafu jamaa alikuwa fasta kujitambulisha mpaka kwa bi mkubwa, akaonyesha ana nia ya kweli kabisa ya kuoa, akawa anaenda naye kwenye harusi za hapa ofisini na za kwa marafiki zao wengine.
Basi mapenzi yameendelea, jamaa akawa ndo anaendesha gari la yule dada, anampeleka ofisini na kumfata jioni. Jamaa taratibu akaanza kutumia hela ya yule dada huku akidai kuna mafao yake atalipwa soon so watakuwa poa kifedha.
Dada wa watu akachukua mkopo kama Mil 9 kwa ajili ya kuanza ujenzi lakini kumbe zikaingia kwenye mkumbo wa kuliwa. Ikafikia wakakubaliana eti jamaa aende Marekani, akifika kule akishaandaa mazingira atamchukua dada yetu wa kazini akaishi naye huko mambelez. Hela ya mkopo ikaisha, akakopa kwa washkaji hapa hela nyingine kama Mil 2 ya kuongezea ili kufanikisha safari.
Jamaa sasa ni muda kama wa miezi miwili toka aende USA na hajawahi hata kutoa contacts zake kwa dada yetu, huku jamaa wanamsakama kwa madeni yao (hasa hasa ile mil 2 ya nyongeza). Facebook jamaa hayuko active tena, inshort kapotea mazima. Dada wa watu saa hizi ni full stress, mshahara unakatwa hela ambayo hakuitumia, madeni yanamwandama, mpenzi kamkatia mawasiliano.
Kwa hiyo dada zetu mfanye uchunguzi wa kina kabla ya kugawa mioyo na mali wa wageni, wengine wamekuja kuchuma vilivyo vyetu kwa njia yoyote ile.
Ha ha akili tumepewa tunapenda kupokea kutoa hatutaki loo
Na kama alimpa hakuna haja ya kudai...ukimpa mtu kitu hutegemei kulipwa
Kama alimkopea ndo imekula kwake
Tujifunze jamani kuwa na misimamo na value zetu
Na hii ndo inawaponza weng wasichana
Mtu anahonga akitaraj ndo mshikaji atampenda na kumuoa kumbe zile hela na gar ndo anatanulia na wengine
Chezea mapenz
Angewekeza kwenye biashara Leo angefaidi
Huu upuuzi wa kuhongana,kujenga pamoja,kwangu not applicable kwa maisha ya boy/ gal friend
At end lazima mmoja ataumia tu.moyo wa mtu fumbo
Mkuu sio Mimi # ichana# I swear never labda unigonge sindano ya usingiz achukue kwenye pochi au niwe unsound mind
Na akili timamu hii hupati mkuu
You have not fall in love with handsome
Ulivyosema alitoka russia nimemhisi mmoja wao alitoka russia akapita hapa kwa lengo la kwenda U.K lakini alishindwa hiyo ilikuwa mwaka jana kama mwezi wa tatu.
Hivyo aliikaa hapa tz almost mwaka mzima...
Hii imenikumbusha kisa cha mdada mmoja (rip)
Alihonga pesa yake karibia yote ya mirathi
Mwanaume akafungua biashara na kuoa mwanamke mwingine
Very sad....
we acha tuu, tena wasichana wanapenda sana wanaigeria wanawaza ile mipesa wanayoiona kwenye sinema ikichezewa chezewa
Hongera kwa hili kula maisha
Na tusitoe mianyaa ya kupokea pokea vyao..
Ukimkopea mpenz utakosa Uhuru wa kumdai bhana hat stareh ya kugegedana itapungua kisa hajakulipa hela
Mpenz wang wakwanza nakumbuka aliniazima buku 2 alikua kazn alsahau hela nyumban kwa madai yake...ebana ee nlivompa iyo buku 2 akazan msamaha wa rais umpepita kumbe mie nakumbuka vizur ck nakuja mdai acha ue ugomvi....aliirudisha buku2 yangu na tukaacha mpaka leo...