Kuna hadithi flani inazungumzia maisha ya mzee mbabe na mchawi katika kijiji flani......
"Mzee huyo alikuwa ni mbabe na mpenda sifa na alijiita MTUKUFU jambo ambalo ni kufuru kwa imani ya watu wa kijiji hicho, kwani watu hao waliamini kuwa jina MTUKUFU ni maalumu kwa Mungu wao tu.
Basi wale wanakijiji waliamua kumuomba Mungu wao ashushe adhabu kwa huyu anayemdhihaki.
Siku moja mvua kubwa na radi ya kutisha ilishuka kwenye kijiji hicho. Mvua na radi ile ilikuwa na madhara makubwa kwenye maisha na mali za wanakijiji hao.
Cha kushangaza ni miezi kadha na kadha kupitia bila yule Mzee mbabe na mchawi kuonekana wala sauti yake kusikika.
Siku moja ikaja bainika kuwa mzee huyo mbabe alikuwa amepatwa na Ugonjwa usiofahamika uliomfanya alale tu, kwani viuongo vyote vya mwili vilisimama kufanya kazi.
Kumbe ile mvua na radi zile ilikuwa ni adhabu iliyoshushwa na Mungu wa wale wanakijiji dhidi ya yule mzee mbabe na mchawi."
Mtanisamehe GT wote, kwa kuwapotezea muda kuisoma hadithi hii isiyohusiana na chochote kwenye mada hii.