Wajemeni,
Tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi bukoba Tanzania, kuna sauti fulani ilipaswa kusikika, lakini hadi leo hii ni siku ya 7 sauti hiyo bado haijasikika kusema lolote au kuonekana popote kuhusiana na tukio hili!.
Hali hii sii ya kawaida na kimya hiki sii cha kawaida ambako pia kutokuonekana popote eneo la tukio au kutokulizungumzia lolote akiwa popote sii kawaida! . Jee kuna nini au nini kimemsibu? !.
Kwa maoni yangu, lilipotokea tuu, mimi miongoni mwa tuliotaraji kusikia neno moja tuu kutoka kwake, na roho zetu zingeponywa, ila mpaka leo ni kimya kabisa!. Nadhani kimya hiki sii bure, hivyo kunauwezekano huu ukimya lazima kuna jambo!, tena sii dogo ni kubwa ila labda hatuambiwi! .
Swali la msingi ni jee tuna haki kuhoji kulikoni?!, au kuuliza atafanya nini?!. Mbona hajaongea au hata kuonekana tuu bila hata kuongea? !.
Kimya hiki, is not right!, could there be something wrong somewhere somehow?!. Jee hii ni kawaida?!, au mimi ndio niko wrong kuulizia jambo ambalo there is nothing wrong?!.
Japo statement ilitolewa, statement ni statement na kauli ni kauli, zingekuwa statement tuu zinatosha, kusingekuwa na sababu watu kuhudhuria misiba, tungekuwa tunatuma tuu salamu za pole na zikatosha!.
Watu tunashauku ya kusikia sauti, tunataka kusikia kauli kwa masikio yetu na kuona kwa macho yetu na sio kutolewa tuu kauli ya maandishi ya salamu za rambi rambi, au pole za maandishi pekee!. Pole ya sauti huku mtu akionekana inafaraja zaidi kuliko salamu za rambi rambi ya maandishi pekee!.
Jee wale wenzangu na mimi mmenielewa?, au mmetosheka?, mmeridhika na kimya hiki? , and is it right?!.
NB.
Uzi huu is meant kwa ma GT tuu wa humu jf. Wewe kama sio GT, nakuomba tafadhali sana usichangie chochote uzi huu kwa sababu is not ment for you!.
Great mind discuss ideas, ordinary minds discuss events na simple mind discuss people! .
Hili sio bandiko la kudiscuss people bali ideas kuwa ukimya huu is it normal? , is right? or could there be something wrong somewhere?!.
Kipimo cha kwanza cha wewe kujipima if you are GT or not ni iwapo utajiuliza kimya cha nini na kimya cha nani kuhusu tetemeko la ardhi lilotokea Bukoba.
Ukijiuliza tuu maswali hayo, jihesabu you are not, hivyo please just jisomee tuu bandiko hili na ujipitie zako bila kuchangia chochote!.
Ma GT, wa humu jf, wanajua ni nani bila hata kuuliza na subject matter ya bandiko hili sio people, sio event bali ideas kuhusu conduct kuhusiana na tukio lenyewe! .
Hivyo nashauri, hata ilitokea wewe kuwa you are not a GT, I beg you, please jifanye kama you are a GT kwa kutotaja jina lolote la mtu yoyote humu wala sio kuzungumzia event ya mafuriko, bali kwa kuzungumzia the idea ya huu ukimya, if kimya hiki ni right, why is it right?, lakini kama kimya hiki is not right, why is it not right?!.
Nawatakia Furahi Dei Njema.
Pasco
Note 1.
Pasco wa JF sio GT, na ndio maana hatathubutu kuchangia lolote katika uzi huu bali mwisho wa uwezo wake ni kupandisha tuu bandiko hili kwa ajili ya ma GT wetu humu jf! .
2.Sababu za kuomba tusitaje taje majina ni kufuatia kufunguliwa kwa kesi nyingi kuhusiana na freedom of expression katika mitandao ya kijamii. Tumeshuhudia mtu ana ji express feelings zake kuhusu mtu fulani anafunguliwa mashitaka ya kumdhalilisha mtu! .
Mfano inawezekana kabisa jamaa akawa yuko very wrong, ukisema fulani is wrong unaweza kushangaa kesho unaambiwa ulimtukana fulani etc. etc., hivyo kwenye discussion za great minds hakuna haja ya kutaja taja majina! .
Pasco