MZIMU
JF-Expert Member
- Apr 29, 2011
- 4,058
- 1,377
Mheshimiwa Kessy atoa taswira halisi ya Muungano. Wazinzibari hawachangii chochote bara. Vipi kuwe na wabunge wao zaidi 86 wanaogharamiwa na bara wao na wake zao.
Vile vile amehoji vipi Raisi wa Zanzibar awe makamu wa Raisi kwani huku amechaguliwa na nani.
Hali imekua tete ni ngumi mkononi. Mheshimiwa mmoja kutoka zanzibar alikua anatoka nje huku akimwiita Mheshimiwa kessy wakazichape kavu kavu.
Mheshimiwa kessy aliongeza chumvi kwenye kidonda kwa kusema, hata bunge hili maalum la katiba Wazanzibari hawakuchangia.
Jamani hizo ndio hekaya za Muungano wetu wa Ajabu kama alivyo sema Raisi wa Kenya Uhuru Kenyata.
Vile vile amehoji vipi Raisi wa Zanzibar awe makamu wa Raisi kwani huku amechaguliwa na nani.
Hali imekua tete ni ngumi mkononi. Mheshimiwa mmoja kutoka zanzibar alikua anatoka nje huku akimwiita Mheshimiwa kessy wakazichape kavu kavu.
Mheshimiwa kessy aliongeza chumvi kwenye kidonda kwa kusema, hata bunge hili maalum la katiba Wazanzibari hawakuchangia.
Jamani hizo ndio hekaya za Muungano wetu wa Ajabu kama alivyo sema Raisi wa Kenya Uhuru Kenyata.