FYATU
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 5,392
- 4,468
Naungana kabisa na wale wote wanaoona kuwa JIDE amekosea, kwa ukubwa wa jina lako na clouds ambao amewahi kushirikiana nao kabla, Ulipaswa kuweka hasira kando na kufikiria vya kotosha kile unachofanya. Ungeweza kuandika kwa busara kubwa na kuonyesha yale yote ambayo unadhani Clouds wanakosea bila kutengeneza mazingira ambayo kwa mtazamo wangu ni kama unajidhalilisha.....Pia ungeweza kutumia watu wakubwa kufikisha malalmiko yako kwa clouds.Ulichofanya ni sawa na mwanandoa anayeanza kuropoka kasoro za mwenzake pale inapotokea tu wameachana. Kwa sababu mwisho wa siku si kwamba nawe ni msafi sana. Kwa kuwa wewe si malaika basi una kasoro zinazokwaza wengine na ungependa uliyemkosea aje akwambie face to face bila kusambaza nje.
Kosa lingine kubwa ulilofanya ni kuapiza mambo yanayohusiana na kifo , Kwa mtu mwenye ufahamu wa wastani huwa hakuna maana yoyote ya kufanya hivi kwa sababu hakuna anayejua siku ya kufa au kwa kifupi hatujui siri iliyojificha kwenye kifo. Marehemu hata siku moja hausiki na kinachoendelea mara tu anapokata roho, Kwa kuwa hujui kwa nini wewe unabaki mwngine anatangulia au vise versa ni vema kuepuka viapo tusivyovielewa. Kama ni mtu mwenye imani fulani ni bora ufute hii kauli.
Kosa lingine kubwa ulilofanya ni kuapiza mambo yanayohusiana na kifo , Kwa mtu mwenye ufahamu wa wastani huwa hakuna maana yoyote ya kufanya hivi kwa sababu hakuna anayejua siku ya kufa au kwa kifupi hatujui siri iliyojificha kwenye kifo. Marehemu hata siku moja hausiki na kinachoendelea mara tu anapokata roho, Kwa kuwa hujui kwa nini wewe unabaki mwngine anatangulia au vise versa ni vema kuepuka viapo tusivyovielewa. Kama ni mtu mwenye imani fulani ni bora ufute hii kauli.