Kimbembe cha VAT: Wawekezaji wanaondoka!!

Kimbembe cha VAT: Wawekezaji wanaondoka!!

Watanzania tunaweza kuwekeza tukaiendeleza nchi yetu badala ya kukaa daily tunawatolea macho wakuja, waacheni waondoke kama hawataki kulipa VAT la sivyo tuwatumbue fasta
 
Acha waende kuliko kufaidi bure!! Imetosha kuwa shamba la bibi!!
 
Kweli. Mfano mwingine mzuri zaidi ni wa Venezuela - nchi tajiri yenye visima vingi vya mafuta mafuta. Kiongozi wao (Maduro) ana tabia hizi hizi tunazozishuhudia ... ukurupukaji, ubabe dhidi ya wapinzani wake, ukanda, uvunjaji wa katiba, u-Mungu mtu, kulaumu wawekezaji & kuwaita wanyonyaji, etc. Matokeo yake wawekezaji wameondoka na mitaji yao, hakuna ajira, hakuna mzunguko wa fedha, serikali haina hela ya mishahara na katoa decree wafanyakazi wa serikali waende kazini siku 2 tu kwa wiki, biashara zimesimama na hamna bidhaa madukani - badala yake akiamka vizuri anaamua mipaka ya nchi ifunguliwe ili watu wakafanye shipping Colombia. Na sisi inaonekana tunaelekea huko huko
Ma nationalists daima upingwa vikali na makuhadi wa unyonyaji
 
Nchi zilizoendelea, kwa kodi heri hata kwetu hapa.
Mkuu,
Nchi zilizoendelea hazina kodi nyingi kwa makampuni. Zina kodi kwa mtu mmoja mmoja.

Kampuni ukililipisha kodi kubwa, linahamia nchi nyingine.
 
Wadau, habari za majukumu! Baada serikali mpya kuingia waliingiza VAT kila sehemu hata kwa waliosamehewa kodi hiyo, nasemea upande wa watengenezaji chakula cha kuku! Kampuni ya thailand CPF wanafunga operation na kuondoka mwisho wa mwezi huu!! Nawasilisha
Mwaumbie huyo mwekezaji awasiliane nami tufunge mkataba wa "LEVERAGE BUY OUT"
 
Katika nchi yote yote kodi ni lazima. Na ukwepaji kodi upo nchi zote na adhabu kali huwaandama wakwepaji. Ni tz pekee wakwepa kodi wakubwa wanapewa mkono na kukaribishwa chai na wakubwa, na vidagaa kuadhibiwa.
 
Wadau, habari za majukumu! Baada serikali mpya kuingia waliingiza VAT kila sehemu hata kwa waliosamehewa kodi hiyo, nasemea upande wa watengenezaji chakula cha kuku! Kampuni ya thailand CPF wanafunga operation na kuondoka mwisho wa mwezi huu!! Nawasilisha
Chakula cha kuku?
Wewe inakuingia akilini kwamba nchi hii tunahitaji muwekezaji wa msosi wa kokolikoo?
 
Wadau, habari za majukumu! Baada serikali mpya kuingia waliingiza VAT kila sehemu hata kwa waliosamehewa kodi hiyo, nasemea upande wa watengenezaji chakula cha kuku! Kampuni ya thailand CPF wanafunga operation na kuondoka mwisho wa mwezi huu!! Nawasilisha
Waambie wakawasalimie kwao.........
 
mi kuna kitu humu naomba mnisaidie wajuzi wa mambo, hivi ni kwamba wawekezaji walikuwa hawalipi kodi ama walikuwa wanalipa ila haifiki kwa mamlaka husika?
 
Mi
Halafu biashara yenyewe kuuza chakula cha king...what a joke[emoji12] [emoji12] [emoji12]

Midagaa imejaa sokoni kuku watakufa? Cha maana alichonachi itakuwa mashine ya kusaga na kuchanganya, kiwanda chenyewe utakuta chaaribu mazingira, mimaji inchirizika, wafanya kazi hawalipwi kwa wakati na wananyanyasika, waende? Hakuna shamba la Bibi tena hapa. Wawekezaji waoneni hivi hivi, hakuna lolote
 
Tang kipindi cha Raisi mstaafu JK misamaha yote ilikuwa kwenye import duty and other charges lakini kwenye issue ya VAT no exemption wawekezaji wote sio hao wa chakula cha kuku tu.
 
Hata Sisi Watanzania Tunafahamu Vizuri Tu Kutengeneza Vyakula Vya Mifugo Aina Zote Mimi Binafsi Naona Kama Wamechelewa Waondoke Hata Leo Tu
 
Back
Top Bottom