Kwanza Kikwete muondoe, kwa sababu yeye ameisha maliza muda wake.
Shein na Magufuli wasipokuwa makini issue gani itawatafuna?!. Zanzibar hakuna issue yoyote! . Hakuna ukiukwaji wowote wa haki za msingi za binaadamu!.
Uchaguzi ulipofutwa kihuni na kiubatili na Jecha, hakuna mtu yoyote aliyeupinga rasmi uhuni na ubatili huo!. Ubatili usipopingwa rasmi, hugeuka ni halali!.
Uchaguzi wa marudio ulipoitishwa tena, hakuna yeyote aliyepinga rasmi!. Japo ule ulikuwa ni ubakwaji wa demokrasia, lakini mtu akibakwa na kutulia tuu kumuacha mbakaji amfanye anavyotaka, na baada ya kubakwa ukatulia tuli!, utahesabika uliridhia ubakaji ule!.
Uchaguzi wa marudio umefuata kanuni zote za uchaguzi huru na wa haki, hivyo Shein ni rais halali wa Zanzibar hadi mwaka 2020 na hakuna yoyote wa kufanya lolote na rais Magufuli hapaswi kufanya jambo lolote, kwa sababu uchaguzi ni mambo ya ndani na Zanzibar ina autonomy yake!.
Lakini kwenye tuhuma za ukiukwaji wa haki za binaadamu kimataifa, hakuna kitu kinachoitwa Zanzibar kinachotambulika kimataifa, kinachotambulika kimataifa ni Tanzania!. Maalim Seif akizidisha choko choko za kutaka kuchafua recodi ya Tanzania katika haki za binaadamu kimataifa, anakuwa ni anamchokoa Magufuli! . Kuna msemo maarufu kule Zanzibar kuhusu choko choko, wanasema "choko choko mchokoe pweza binadamu hutamuweza!", hivyo ndivyo ilivyo kwa Magufuli, Seif hatamuweza!. Hizo kelele za Maalim Seif zinaweza kutafsiriwa kuwa ni fyokofyoko hivyo sana atakachoambulia Maalim Seif ni Magufuli anaweza kumhifadhi katika mahala salama!, kule wanaita pahala salama!
Au Magufuli akijiridhisha hizo kelele za Maalim Seif hazina athari zozote kiusalama, anaweza kumpuuzia tuu ila kwanza atamtafuta na kumpa mkono aone Maalim Seif atafanya nini, baada ya hapo mtashuhudia heshima na adabu! .
Pasco