Kilimo si kwa watu dhaifu

Watu wanasema kilimo kigumu yeah hakuna urahisi kwenye kutengeneza pesa

Iko hivi ukiamua kufanya kilimo ni kama biashara panda shuka hazikosekani

Kuna msimu mtu anaweza akawa ameanza kilimo akavuna akakuta bei sokoni ni nzuri. Kundi hili kwa mfano msimu ujao soko likiwa na bei ndogo ndio huwa wanajazana mitandaoni na kusema kilimo hakilipi hakieleweki. Kawaulize wafanyabishara kama muda wote wanapiga tu maokoto kuna wakati hali si hali.

Kundi hilo juu ni sawa na hili kundi la pili wale ambao wameanza kilimo hawajakutana na soko zuri huenda msimu mmoja au miwili kama walivyotarajia nao hulalamika kilimo hakina tija.

Ukitaka kuona kilimo kinalipa wewe lima tu usikate tamaa huenda wengine wasinielewe hapa namaanisha ukiwa unalima bila kuacha utaona jinsi kilimo kinalipa usiwe mtu wa kujaribu na kuacha.

Niwape mfano rahisi tu: Mwaka jana waliolima vitunguu watanielewa jinsi tumepiga maokoto, gunia 1 limefika hadi 400,000

Msimu wa mwaka juzi wengi hawakuingiza mtonyo kwenye vitunguu bei haikuwa nzuri na mvua ziliwakwamisha waliotegemea kilimo cha mvua hivyo msimu wa mwaka jana hawakulima vitunguu.

Sasa ona yale makundi 2 niliyotaja mwanzo watakavyoingia kwa pupa msimu ujao kwenye kulima vitunguu. Wakati wa kuvuna wakikuta bei iko chini kutoka mfano 400,000 kwa gunia mpaka 100,000 kwa sababu wengi wamelima vitunguu wataanza tena kulalamika

Ikiwa kilimo kipo hivyo suluhisho ni nini? Wewe cheza na kauli mbiu ile ile wewe lima tu

Kilimo is not for the weak hasa cha biashara lazima uweke mpunga wa kutosha, usimamizi, tegemea ups and downs

Hapa ume maliza kila kitu, hakika hakuna shortcut inahitaji ujiwekeze haswa. Nimefanya msimu huu kama pilot phase lakini nime jitosa haswa haswa nategemea mwakani nisahihishe makosa ya mwaka huu
 
Ukiondoa waalimu,
Hamna watu wanaishi kwa stress nchi hii Kama wakulima
utakua unazungumzia wakulima wa bustani za mchicha huko dar😂😂 hicho sio kilimo ni shughuli za mikono tu kuuchangamsha mwili na kukosa maeneo makubwa , vitendea kazi na mbegu bora zaidi
Kilimo ni moja kati ya kazi nzuri sana ila uwe na passion ! na usiende kulima kwa sababu umehadithiwa na kulimisha kwa simu !! hapo kilimo kitakua Forex ! Kuanguka na kusimama ni sehemu ya kila biashara na kazi
 
Umenena yaliyo kweli mkuu.
Niliwahi lima vitunguu pale Ruaha mbuyuni,nikaweka milion mbili na kitu ila baada ya kuvuna na kuuza nikapata kama laki nne hivi nikaapa sirudii tena na eneo liko tu nimewapa wanakijiji walime bure lisiwe pori.

Nina eneo liko mkuranga,mtoto wa aliyeniuzia akanishawishi sana tulime mahindi hadi nikakubali.Akasema tujaribu na heka chache kwanza.Akasema nipe 1 M nilime heka 4 tu kwanza then tukivuna najua utashawishika tulime hekari zote.Maelezo yake yalininogea,nikashawishika nikampa 1M akasepa.Mwisho wa siku sikupata hata hindi moja la kuchoma.

Nilichojifunza,kilimo kinataka uingie mwenyewe shambani mwanzo mwisho na mimi maisha ya kuishi shamban na manyoka siyawezi.
 
Nimejaribu kufanya kilimo cha mahindi msimu huu wa kilimo and let me tell you something maina, kilimo is not for the weak.

Hamna rangi sija acha ona lakini as they say maji ukisha ya vulia nguo sharti uyaoge so we move .
Nakubaliana nawe comradeee nimelima eka 6 za mpunga acha kabisaaa aiseeee
 
Hakuna kitu rahisi,labda kama unafanya ufugaji wa kienyeji wa Bora liende ila ufugaji wa kusaka pesa lazima uone maumivu.
Nimelima na nimefuga, kwaiyo kwangu mimi experience yangu niliyoipata ni bora kufuga kuliko kulima. Unaweza kuuza baaadhi ya mifugo mfano kwangu mimi ni nguruwe ukapata pesa ya kuwalisha wenzake wanaobakia lakini huwezi kukata shamba ukauza baadhi ya mazao ili upate pesa ya mbolea ununue kwa ajili ya yaliyobakia.
 
Ufugaji nao jau tu, unalala na vifaranga 2000 una amka viko 70
Dah kuku sijawahi jaribu baada ya kumuona sister broilers wake anabidi awauze siku ya 22 akaja jamaa akachagua wakubwa tupu akaacha wadogo wadogo sister akaanza kuwalisha tena hadi wapate nyama nyama, kuku labda nifuge wa kienyeji wa kula.
 
Umenena yaliyo kweli mkuu.
Niliwahi lima vitunguu pale Ruaha mbuyuni,nikaweka milion mbili na kitu ila baada ya kuvuna na kuuza nikapata kama laki nne hivi nikaapa sirudii tena na eneo liko tu nimewapa wanakijiji walime bure lisiwe pori.

Nina eneo liko mkuranga,mtoto wa aliyeniuzia akanishawishi sana tulime mahindi hadi nikakubali.Akasema tujaribu na heka chache kwanza.Akasema nipe 1 M nilime heka 4 tu kwanza then tukivuna najua utashawishika tulime hekari zote.Maelezo yake yalininogea,nikashawishika nikampa 1M akasepa.Mwisho wa siku sikupata hata hindi moja la kuchoma.

Nilichojifunza,kilimo kinataka uingie mwenyewe shambani mwanzo mwisho na mimi maisha ya kuishi shamban na manyoka siyawezi.
Wewe kosa lako ushalijua, ulikuwa unataka kulima kwa pdf
 
Peasants wanaumiza mgongo, ila farmers wanacheza na mashine tu, tatizo unatakiwa kuqa na mtaji.
Sasa bongo hii wangapi wanamudu mashine, graduates wanaambiwa wakajiajiri kwenye kilimo wanapewa mashine? Mimi ndio maana mambo ya kilomo nilishakataa...kama kulima nitakuwa namsaidia tu mzee tupate chakula ila kwamba niwe siriazi kabisa nitegemee kinitoe kwenye unaskini hapana siwezi kujidanganya, najua jeuri hiyo sina.
 
Back
Top Bottom