mwagito25
JF-Expert Member
- Aug 11, 2013
- 633
- 350
Habarini wana jamvi, ninapenda kuwashirikisha jambo ambalo nililiona huko mkoani Iringa, wilaya ya Mufindi.
Mwezi march mwaka huu 2021, nilienda kijijini kwetu huko mufindi, nikabahatika kumtembelea ndugu mmoja shambani kwake.
Shamba lake la parachichi lenye ukubwa wa ekari 15, lakin sehemu ambayo tayari kaanza kuvuna ni ekari tano.
Jambo la kuvutia kuliko yote ni kwamba kwa sasa soko bado lipo imara saana endapo umepanda mbegu inayofaa kuuza nje ya nchi. Mbegu hii ina maganda imara na inachelewa kuharibika.
Lakini pia kilichonishangaza ni kwamba matunda ameanza kuvuna baada ya muda wa miaka miwili na nusu tangu alipopandikiza miche.
Nilipoona hayo ilibidi niendelee kuhoji kuhusu maeneo ambayo matunda hayo hustawi, na jibu lilikuwa ni kaskazini mwa nchi na nyanda za juu kusini ingawaje kwa kaskini kikwazo ni bei ya ardhi kwa kuwa hupaswi kukodi kwani ni zao la kudumu.
Lakini pamoja na mazuri hakusita kunijuza changamoto za kilimo hiki ambazo ni kama ifuatavyo:-
Kwa wapenzi wa kilimo endeleeni kufuatilia kwa undani kama utavutiwa na maelezo hayo.
NB: Fuatilia kwa umakini kwa faida yako, usikatishwe tamaa wala usivutiwe tu bila kujiridhisha na uhalisia.
Asanteni
Mwezi march mwaka huu 2021, nilienda kijijini kwetu huko mufindi, nikabahatika kumtembelea ndugu mmoja shambani kwake.
Shamba lake la parachichi lenye ukubwa wa ekari 15, lakin sehemu ambayo tayari kaanza kuvuna ni ekari tano.
Jambo la kuvutia kuliko yote ni kwamba kwa sasa soko bado lipo imara saana endapo umepanda mbegu inayofaa kuuza nje ya nchi. Mbegu hii ina maganda imara na inachelewa kuharibika.
Lakini pia kilichonishangaza ni kwamba matunda ameanza kuvuna baada ya muda wa miaka miwili na nusu tangu alipopandikiza miche.
Nilipoona hayo ilibidi niendelee kuhoji kuhusu maeneo ambayo matunda hayo hustawi, na jibu lilikuwa ni kaskazini mwa nchi na nyanda za juu kusini ingawaje kwa kaskini kikwazo ni bei ya ardhi kwa kuwa hupaswi kukodi kwani ni zao la kudumu.
Lakini pamoja na mazuri hakusita kunijuza changamoto za kilimo hiki ambazo ni kama ifuatavyo:-
- Upatikanaji wa mbolea ya samadi.
- Kumwagilia miche wakati wa kupandikiza kwani hupaswi kuipanda msimu wa mvua, hivo kama shamba halipo karibu na mto utapaswa kuwa na vifaa vya kuhifadhia maji ili uweze kumwagilia miche hadi mvua itapokuja.
- Kuweka fenzi ya wire ili kuilinda miche ya mifugo kama mbuzi nk.
Kwa wapenzi wa kilimo endeleeni kufuatilia kwa undani kama utavutiwa na maelezo hayo.
NB: Fuatilia kwa umakini kwa faida yako, usikatishwe tamaa wala usivutiwe tu bila kujiridhisha na uhalisia.
Asanteni