Kilimo cha alizeti, utunzaji na soko

Kilimo cha alizeti, utunzaji na soko

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
1,132
Reaction score
2,681
Nimevutiwa sana na kilimo cha alizeti hasa ukizingatia mafuta yake ni miongoni mwa mafuta yanayopendwa na watumiaji wengi japokuwa yanauzwa bei ghali

Kwa msimu huu nimefanya majaribio ya kilimo hiki kama sehemu ya kupata uzoefu

Nimeweza kubaini yafuatayo na hapa nitafurahi kama wengine mtaweka uzoefu wenu ili tuendelee kujifunza zaidi;

1. Kilimo cha Alizeti ni rahisi sana kwani kina hitaji kuandaa shamba, kupanda, kupalilia na kuvuna tu

2. Ni kilimo kinachotumia pesa kuanzia stage ya mwanzo hadi unapopeleka kukamua mafuta mashineni

3. Kama kilivyo rahisi, pia ni rahisi kupoteza pesa nyingi sana na zisirudi kwasababu kila hatua inahitaji pesa

4. Soko lake ni zuri lakini bado bei ya mafuta haikidhi kumpa faida mkulima

Kwa mfano, walio wengi niliovuna nao tumepata wastani wa gunia 4 hadi 7 (za debe sita) kwa heka moja ambapo baada ya kukamua mafuta unapata wastani wa lita 16 hadi 20 kwa gunia moja

Kwa bei ya jumla lita 20 inauzwa Tsh.80,000/= hadi Tsh.85,000/=

Kwa mahesabu haya ni vigumu sana kutoboa japo wenye mashine wengi wanakupa option ya kukwepa gharama za ukamuaji kwa kuwaachia mashudu

Je, nyie wenzetu mnapataje faida kwenye kilimo cha Alizeti?

Karibuni mtupe uzoefu weni
 
Hongera Kwa mavuno mkuu
Nimejaribu kuangalia mapato kulingana na maelezo yako naona umepata Sana.

Mathalani, umevuna gunia 4 Kwa eka na kila gunia umepata Lita 20 ambazo umeuza Kwa bei ya 80.000. mapato yanaonekana kuwa ya kuridhisha
4*20*80000=6,400,000/=

Kwa ninavyofahamu gharama ya kuhudumia ekari moja haiwezi kuwa zaidi ya million moja, Kwa hiyo umefanikiwa Sana mkuu.
 
Back
Top Bottom