Kilimo cha Parachichi - Fahamu Aina, Namna ya Kulima na Masoko

Mkuu kama unataka kulima parachichi nenda MBEYA au NJOMBE, wanalima sana hiyo aina HASS,tena zipo aina tofauti tofauti kama vile GWEN HASS, CALFONIA HASS na LAMB HASS ila kwa sabab unataka kwa ajili ya export nakushauri ulime lamb hass mana ni kubwa halaf lina peke dogooo, pia kuna zile mbegu za burundi kama penkerton na chorquatte zote zina stawi tu. Hata hivyo kama hautapenda ku-export waweza kuwauzia wawekezaji (1kg 2500/3000 pia inalipa sana), wanapatikana hukohuko MBEYA na sasa wako mbioni kufungua plantation zingine NJOMBE.

Na kama unataka kufanya biashara ya kupeleka dar/dom, usiende MOSHI kama mdau flani hapo juu alivyosema nenda RUNGWE ndiko kwenye uhakika wa parachichi iliyobora na yenye faida kutokana na maoni ya walaji,hasa parachi ya x-ikul.ambayo ni kubwa na ina ngozi ngumu, inapatikana kwa wingi sana maeneo hayo na ai haribiki haraka.lakini pia waweza kwenda hata moshi kuangalia aina za kule ili kujiridhisha. Mimi niliyagundua haya yote mana nilikuwa kwenye industry kwa muda wa kama 5yrs hivi.
 
Asante kwa mchanganuo mzuri, nadhani Rungwe na hizo sehemu utofauti wa hali ya hewa na mahitaji haujapishana almost the same, issue ni kwamba hass type huku Moshi hazilimwi lakini ni kifanya majaribio maana nina eneo kubwa tu lazima zitagrow kama kawaida.
 
Kama kuna mtu anategemea kupanda parachichi mwaka huu Wilaya ya Kilolo, basi tuwasiliane, tutakuletea seedlings mpaka shambani kwako, price yetu ni 2500/- kwa mchi,
Ni-PM

Nyie ndo nmebandika tangazo njia panda ya kwenda lulanzi.
 
Hizi ndio seedlings za hass species nzuri sana ila zinakubali vizuri Njombe na Mbeya

IMG-20181218-WA0003.jpeg
IMG_20190101_131022.jpeg
IMG_20181218_112458.jpeg
 
Hivi ikikubali Mbeya na Arusha milimani si itakubali?
Hili zao sijalielewa kimsingi Njombe halikutakiwa kustawi ila maajabu ndio sehemu inazalisha kwa ubora mkubwa, fanya research kwa huko Arusha seedlings Nairobi zinapatikana.
 
Hivi ikikubali Mbeya na Arusha milimani si itakubali?
Yanakubali te
Hili zao sijalielewa kimsingi Njombe halikutakiwa kustawi ila maajabu ndio sehemu inazalisha kwa ubora mkubwa, fanya research kwa huko Arusha seedlings Nairobi zinapatikana

Sent using Jamii Forums mobile app
Yanakubali vizuri tu, kuna mashamba makubwa ukitokea arusha kuelekea Moshi maeneo ya USA River, ukipita stand ya USA River utakuta mashamba ya kahawa kwa barabarani kwa ndani ndio kuna ya maparachichi, kuhusu soko TAHA watakuunganisha na wanunuzi kama wanavyofanya kwenye mazao mengine ya horticulture kama maua (roses).
 
Asante kwa mchanganuo mzuri, nadhani rungwe na hizo sehemu utofauti wa hali ya hewa na mahitaji haujapishana almost the same, issue ni kwamba hass type huku Moshi hazilimwi lakini ni kifanya majaribio maana nina eneo kubwa tu lazima zitagrow kama kawaida.
Kwa Moshi unaweza kwenda Sanya Juu, Kifufu Estate kuna mwekezaji yuko pale analima na ana-export, kipindi cha nyuma alikuwa anawagawia wenyeji walioko karibu kwa sharti ya kumuuzia yeye, kipindi cha mavuno.
 
Swali la kujiuliza hizi parachichi wanazo vuna leo walipanda lini ? Au n za kisasa
 
Kilimo cha maparachichi ni moja ya miradi bora wilaya ya Rungwe na sehemu zingine, wadau naomba kujua umbali unaofaa kati ya mche na mche.
 
unapanda aina gani? Kila parachichi linatofautiana ukuaji, mengine yanakua kuelekea juu, mengine yanatanua pembeni Kama Hass.
Shamba lako lina ukubwa gani? Kama una ardhi kubwa 10*10m ni nzuri sana, 7*7 ni sawa kama una ardhi ndogo ila baada ya miaka 5+ miti itaoverlap na avocado haitaki shades so utarudi hapa kulia "kwanini sipati mavuno mengi"
 
Kila eneo la ekari moja it is Ideal kuvuna matunda ya parachichi yenye thamani ya milioni mbili. Kwa ekari hamsini inamaana unakuwa unavuna matunda ya thamani ya milioni mia. yaani hapo unaajiri na kuajiri wafanya kazi kadhaa kwa ajili ya shamba tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom