Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,226
- 79,517
Hivi jamani hebu tuongee ukweli yaani kutangazwa kote kule harambee ya kuchangia CCM Kilimanjaro kumepatikana millioni 200 tu? Hivi kunani huko Kilimanjaro? au ndo mwendo wa kususa maana najua hizo hela ni ndogo sana kwa jinsi watu wa huko walivyo na moyo wa kujitolea na mwamko wa kupata uongozi bora! Hii inamaanisha nini? CCM haikubaliki ama? Yangu mie macho kuna individuals wamenunua choppers tayari kwa kikishindo kikuu! au hawataki kufuata upepo au kuwa mbayuwayu au kufanywa mbuzi wa kafara! Kwanini mchango usianzie Mwanza? au Mbeya? kuna umuhimu gani mchango uanzie Kilimanjaro? Na Makamba alikuwa wapi? CCM haina Katibu Mkuu siku hizi?