Kilimanjaro yamsusia Kikwete ama?

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,226
79,517
Hivi jamani hebu tuongee ukweli yaani kutangazwa kote kule harambee ya kuchangia CCM Kilimanjaro kumepatikana millioni 200 tu? Hivi kunani huko Kilimanjaro? au ndo mwendo wa kususa maana najua hizo hela ni ndogo sana kwa jinsi watu wa huko walivyo na moyo wa kujitolea na mwamko wa kupata uongozi bora! Hii inamaanisha nini? CCM haikubaliki ama? Yangu mie macho kuna individuals wamenunua choppers tayari kwa kikishindo kikuu! au hawataki kufuata upepo au kuwa mbayuwayu au kufanywa mbuzi wa kafara! Kwanini mchango usianzie Mwanza? au Mbeya? kuna umuhimu gani mchango uanzie Kilimanjaro? Na Makamba alikuwa wapi? CCM haina Katibu Mkuu siku hizi?
 
Hivi jamani hebu tuongee ukweli yaani kutangazwa kote kule harambee ya kuchangia CCM Kilimanjaro kumepatikana millioni 200 tu? Hivi kunani huko Kilimanjaro? au ndo mwendo wa kususa maana najua hizo hela ni ndogo sana kwa jinsi watu wa huko walivyo na moyo wa kujitolea na mwamko wa kupata uongozi bora! Hii inamaanisha nini? CCM haikubaliki ama? Yangu mie macho kuna individuals wamenunua choppers tayari kwa kikishindo kikuu! au hawataki kufuata upepo au kuwa mbayuwayu au kufanywa mbuzi wa kafara! Kwanini mchango usianzie Mwanza? au Mbeya? kuna umuhimu gani mchango uanzie Kilimanjaro? Na Makamba alikuwa wapi? CCM haina Katibu Mkuu siku hizi?

Mzee
kwa nisivyowapenda naona kama hizo pia ni nyingi sana, niliposoma title nilitegemea wawe wamepata mchango fulani mdogo sana wa kuboa.
 
Wewe chache hizo? hpo unatakiwa usikitike kabisa wamepata nyingi mnoo ukata huu wote wa Tanzania bado unawachangisha watu uwapigie kampeni hao hao si ujinga huu? Watanzania bana wanaiga wakina Obama wale ni tofauti aisee
 
Hao wanafiki wanaojiona Kilimanjaro ni yao wakina mama Nsilo Swai mama mtu mzima, wakina Innocent Macha na Mareale wao kwanza waende kumfukuza mwizi wao wa kiwanja cha Uhuru Park. CCM wezi wakubwa walishalamba hapo eti wanadai mwekezaji apewe hati akakopee? hivi wanaleta laana za wapi? walishaona mchaga anatoa ardhi kwa mgeni tena kwa kiburi eti akakopee kama si madiwani wa Chadema leo hii sio tukingekua hakieleweki kama ilivyo hivi sana bali kungeshawekwa uzio maskini ardhi yetu. Cha kushangaza ukisoma hiyo list ya CCM wakina kinabo sijui wakurugenzi sijui mwanasheria crap wa kuiba wa wilaya ni wachaga, tena wameacha mila wanaleta upumbavu wao kwenye ardhi ya wananchi. Tatu uliona wapi harambee ya moshi ifanyike dar si matusi hayo? hao ni washikaji wake kikwete wana mtandao tunawajua sasa hizo 200m kwani agrey na inno walishindwa kuzichanga mpaka waweke harambee? Pili labda wangeiita harambee ya wachaga kama ni kilimanjaro inamakabila mengi wako wapi wakina cleopa Msuya, wakina Kisumo pamoja na siku hizi kuwa tarumbeta la mafisadi baada ya kupewa ulaji vodacom, wakina Senkoro, wavungu vaathu vosa ava tuvamanje vaho hiyo? hatujamuona Jumanne Maghembe kachanga ngapi? wakina Mramba, Augustino Lyatonga Mrema mchovu angetoa katika zile milioni alizosema anazo benki kuendelea kununua ubunge. This was a scam, poleni wanafiki na zaidi pole huyo kikwete yaani ni kweli hizo hela achana na makamba hata hao wanafiki wake Macha na Agrey wangeweza kuchangisha harambee hiyo, utadhani harambee ya kanisani? KIKWETE fanya kazi za taifa acha hicho cheap pay backs za marafiki wajinga ubora ungekua unamarafiki wenye akili, sasa ona makamba anakwenda igunga kufanya nini? inamaana CCM bila Rostam Aziz haiwezekani? mbona mnatukana hata wakunga walioatangulia kabla yenu? kumbuka kabla ya CCM kulikua na TANU na wazazi wetu walihenyeka ndio mkapata CCM, msitutie vidole machoni kudai hiki ni chenu na sisi tukidai chetu kutokana na jasho la wazazi wetu mtapata pakusimamia?
 
Kuna mtu hapo juu kasema kweli. Yaani kampeni mnaenda kupiga kwa wananchi halafu mnawachangisha wananchi hao hao. Tena kwa bugudha. Mimi nimepata ujumbe mfupi kama mara 2 wa kuchangia CCM. Ujinga mtupu.

Halafu, kama kweli ni kwa ajili ya kampeni, basi hamna haja ya kuchanga, ni kuhamasisha tu hao wananchi ambao wangechanga kuwa kila mtu afanye kajikampeni kake, ujumbe utafika!!

Yaani CCM imenifikia hapa!!
 
Katika hizo 200mil, kama 10mil zimechangiwa na familia ya Kikwete. Hivyo unaweza ukakuta 50mil imetoka kwa viongozi wakuu wa CCM wa Taifa na Mkoa. Hiyo itamaanisha kwa wananchi wamepata 150mil tu. Hiki ni kiwango cha kumfanya JK afikirie mara 2. Katika enzi zao kiwango kama hicho kilikuwa kinatolewa na fisadi mmoja tu.
 
Kilimanjaro hakuna wahindi?

wadosi mbona wa kumwaga tu!
Ila si wanasema hiyo harambee imefanyika Dar?hapo hatuwezi kusema ni "wakaazi" wa Kilimanjaro,wangesema wachagga wakaazi wa Dar,ambao labda nao ni mafisadi tu!Kwa upande wa wahindi wao ni ccm damu.
 
Kilimanjaro hakuna wahindi?

Mkuuu....jibu ni ndio. Hakuna wahindi. Waliopo wamefulia mbaya. Wanauza mablanket ya katani....kwisha lazi yao. Knjaro hufanyi biashara lama sio mchaga au Mpare. Amebaki panjuani tu. Anauza a few electronics!
 
Naomba kuuliza swali la kijinga. Hivi CCM wanataka kushinda majimbo yote Tanzania by hooks and crooks?
Jimbo la moshi mjini wamelifuatilia kwa nguvu zote, watu wamejenga nyumba, kununua mashamba na kuanzisha biashara kwa pesa ya CCM.
Napenda sana jinsi timu ya kampeni ya Ndesa inavyodeal na watu wa CCM. Wanasema kabisa kuwa watu wote wanaoshabikia CCM ni kwa vile wanataka hela na ni haki yao wazipate maana ni pesa zao za kodi. Kwa hiyo wapiga kampeni wa Mama minde wakati huo wanachukuliwa kama wapiga kura wa Ndesa maana siku ya mwisho ni wewe mwenyewe utakuwa kwe kibanda cha kupigia.
Kwa kutohangaika kushindana shilingi kwa shilingi na CCM na kuhakikisha kuwa ujumbe wa kula pesa ila kura mpe Ndessa CCM wamekuwa kila baada ya uchaguzi wanaanza kutafutana mchawi...
Mama Minde aka shemeji ya Mkapa aligawa pesa mpaka basi, Ben hakuisha kumuuza lakini mwisho wa siku wanajua yaliyowafika. Hii inatokana na watu kuwa na uelewa na kuhoji kwa nini wanataka hili jimbo hivi? Hatuwapi. Kama wanataka kuleta maendeleo wanasema Mkapa si akaendeleze kwao Mtwara kuna mapori kibao na watu wanatembea uchi si awasaidie Wamachinga wenzake. Kilimanjaro wanaamini kuwa maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe na sio CCM hii ni moto ambayo watu wa mikoa mingine wanatakiwa wayajue.
Yangu ndo hayo...
 
Back
Top Bottom