Kilimanjaro: EX-Wife auza kiwanja cha mama mkwe baada ya aliyekuwa mumewe kushindwa kuhudumia Watoto

Kilimanjaro: EX-Wife auza kiwanja cha mama mkwe baada ya aliyekuwa mumewe kushindwa kuhudumia Watoto

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
Bibi mwenye umri wa miaka 66 anayefahamika kwa jina Julia Albin mkazi wa Tarafa ya Useri wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, amedai kuwa amejikuta katika hali ya sintofahamu baada ya eneo lake lenye makazi yakudumu kuuzwa kwa amri ya mahakama, kutokana na mwanae kushindwa kutoa matumizi kwa mtalaka wake ambaye amezaa naye watoto watatu.

Inaelezwa kuwa hatua hiyo imekuja baada kijana wa bibi huyo kutofanyia kazi amri mahakama, ambayo ilimtaka kila mwezi atoe shilingi elfu 90,000 za matumizi kwa mtalaka wake ambaye aliondoka na watoto watatu baada ya ndoa yao kuvunjika.

Aidha, Mwanaume anayedaiwa kushindwa kutoa fedha hizo kila mwezi aitwae Evarest Mrosso, amesema kuwa alishindwa kutii amri ya mahakama kutokana na hali ngumu aliyobakia nayo baada ya ndoa hiyo kuvunjika, na kisha mwanamke huyo kuondoka na mali zote pamoja na fedha za mauzo ya eneo walilokuwa wanaishi, ambazo zilidaiwa kuwa zinakwenda kutumika kuwatunzia watoto hao.

============================

Siku moja baada ya GADI TV kurusha habari inayomuhusu bibi mwenye umri wa miaka 66, aitwae Julia Albin ambaye ni mkazi wa Tarafa ya Useri wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, akidai kuwa amejikuta katika hali ya sintofahamu baada ya eneo lake lenye makazi yakudumu kuuzwa kwa amri ya mahakama, kutokana na mwanae kushindwa kutoa matumizi kwa mtalaka wake, hatimaye Uongozi wa juu wa wilaya hiyo umemfikia bibi huyo na kumpa msaada wa kisheria kutokana na madai yake.

Ikumbukwe inaelezwa kuwa, hatua hiyo ya uuzwaji wa eneo hilo ilikuja ikiwa ni baada kijana wa bibi huyo kutofanyia kazi amri mahakama, ambayo ilimtaka atoe shilingi elfu 90,000 kila mwezi za matumizi kwa mtalaka wake ambaye aliondoka na watoto wake watatu baada ya ndoa yao kuvunjika.

Aidha, Ikumbukwe pia mwanaume anayedaiwa kushindwa kutoa fedha hizo kila mwezi aitwae Evarest Mrosso, alisema kuwa alishindwa kutii amri ya mahakama kutokana na hali ngumu aliyobakia nayo baada ya ndoa hiyo kuvunjika, na kisha mwanamke huyo kuondoka na mali zote pamoja na fedha za mauzo ya eneo walilokuwa wanaishi, ambazo zilidaiwa kuwa zinakwenda kutumika kuwatunzia watoto hao.


CHANZO: GADI TV
 
Mama anaondoka na watoto wote watatu halafu anataka alipwe elfu 90000 kila mwezi, ni kama biashara fulani?
 
Baba pia anaweza kudai physically Custody 🤔
Cha kushangaza mama anaondoka na wotete wote halafu anadai matunzo au kama baba alikimbia familia na kuitelekeza. Hata mgao wa mali unapotoka unagawanywa sehemu taatu na baba anabaki naa mgao wake. Ukweli wanaujua wenyewe.
 
Cha kushangaza mama anaondoka na wotete wote halafu anadai matunzo au kama baba alikimbia familia na kuitelekeza. Hata mgao wa mali unapotoka unagawanywa sehemu taatu na baba anabaki naa mgao wake. Ukweli wanaujua wenyewe.
Tatizo kesi za hivi mpaka zifike mahakamani zinaanzia dawati la jinsia , huko kama hauna akili timamu ya kupangua hoja unakutana na wasimbe ,wanakubebesha zigo la mapupu , na nakala hizo zinatumika mahakamani pia🤔
 
Back
Top Bottom