Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,252
Kijana mmoja Anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35 aitwae Henry amejinyonga hadi kufa kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi. Tukio hilo limetokea leo mchana Katika Kijiji cha Narumu huko katika wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Sababu Za kijana huyo kujinyonga hadi kufa ni baada ya mke wake wa ndoa ajulikanae kwa jina la Zuhura Luteri kuondoka na kwenda kujihusisha Kimapenzi Na wanaume wengine na hivyo alifanya kila jitihada za kumrudisha lakini zilishindikana.
Polisi wamefika kuchukua mwili na kuondoka nao Kwa ajili ya Uchunguzi. Kijana huyo alikuwa akiishi na mama yake mzazi na ameacha watoto wawili mwenye umri wa miaka 7 na mwingine ana umri wa miaka 5.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Ismael Urassa amethibitisha kutokea Kwa tukio hilo.
Sababu Za kijana huyo kujinyonga hadi kufa ni baada ya mke wake wa ndoa ajulikanae kwa jina la Zuhura Luteri kuondoka na kwenda kujihusisha Kimapenzi Na wanaume wengine na hivyo alifanya kila jitihada za kumrudisha lakini zilishindikana.
Polisi wamefika kuchukua mwili na kuondoka nao Kwa ajili ya Uchunguzi. Kijana huyo alikuwa akiishi na mama yake mzazi na ameacha watoto wawili mwenye umri wa miaka 7 na mwingine ana umri wa miaka 5.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Ismael Urassa amethibitisha kutokea Kwa tukio hilo.