KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Looo! mkuu, inanilazimu nikubaliane na unayoandika hapa, maana naona umenichanganya au umejichanganya mwenyewe kiasi cha kutotambua ni kipi hasa unachong'ang'ania katika mada hii!Katiba na sheria vinasemaje kuhusu uhuru wa vyombo vya habari?, Katiba inasemae kuhusu mikutano ya vyama vingine vya siasa kufanya mikutano? Katiba na sheria ndiyo njia, sasa kama havifuatwi ndiyo yale unayoona kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kuibuka kwa watu wasiojulikana, n.k. Mtu anaomba aruhusiwe ampige risasi Tundu Lissu. Sheria inasemaje kuhusu kumuua mwenzako? Leo Zitto watu wanajadili wamemfanyie kitu mbaya zaidi ya Tundu Lissu. Je, katiba na sheria vinasemaje?
Unajua kama kumtishia mwenzako kumtoa uhai, ni kosa la kisheria?
Unaona yote haya ni kutofuatwa Katiba na sheria za nchi.