mzee wa liver
JF-Expert Member
- Dec 14, 2014
- 81,403
- 423,245
Kaka yangu,
Dotto Bulendu.
2015 Vyombo vya Habari hususani TV viliweka utaratibu mzuri wa namna ya kuandika na kutangaza Habari za Kisiasa hususani uchaguzi mkuu kuanzia hatua ya mchakato ndani ya vyama mpaka Siku ya kutangazwa Kwa mshindi.
TV zilivipa vyama vyote hadhi Na haki Sawa ,ilikuwa ukifungua taarifa ya Habari ya TV,Kama leo stori ya kwanza ni CCM itakayofuata itakuwa ya Chama shindani,na kesho stori ya kwanza itakuwa ya kwanza ya Chama shindani inayofuatia CCM.
Mfano Mmoja wapo walikuwa ITV, walipeleka waandishi upande wa UKAWA Na Upande wa CCM,Na kama leo Kwenye taarifa ya Habari CCM wakitengeneza Habari kuu,basi kesho itakuwa zamu ya Kambi ya vyama shindani.
Mwaka huu imekuwa tofauti kidogo,Jana nilitazama Kwa wakati mmoja taarifa za Habari za TBC,Azam(UTV),Star TV,na ITV ambapo hiyo jana vyama viwili vya upinzani vilikuwa vimeanza Vikao vyao vya juu vya kupitisha majina ya wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na upande wa Zanzibar.
Nilichoshuhudia kilikuwa tofauti kabisa Na zile Siku ambazo CCM ilikuwa inapitisha majina ya wagombea Uraisi,CCM Kwa Siku zote ilitawala maudhui ya Vyombo vya Habari ,Karibu Taarifa ya Habari zote ,stori ya kwanza ilihusu mchakato ndani ya CCM.
Ila kwa Jana, ni Azam (UTV) pekee Kwenye taarifa ya Habari ndiyo waliotoa uzito Kwenye matukio ya Vikao vya vyama vya Chadema Na ACT,Azam waliipa kipaumbele stori ya Chadema Kwa kuifanya Kuwa stori namba Moja Na waliipa Karibu dakika 6,ikafuatiwa na ile ya ACT,Stori ya Chadema Na ACT ilikwenda karibu dakika 12 Kwa uzito ule ule ambao waliupata CCM.
ITV Kwenye taarifa yao ya Habari ya saa mbili stori Hii haikuwa Habari kuu,iliruka baada ya dakika 20,Yaani saa mbili Na dakika 20,Na ilirushwa Kwa mfumo wa kifurushi ambacho hakikuzidi dakika 2 Na sekunde 45 ,Kwenye Uandishi Habari kuwekwa hapo maan yake haina uzito.
Star TV wao waliirusha baada ya dakika 18,Yaani saa mbili Na dakika 18,Na stori hiyo haikuwa Na sauti za wagombea wala taarifa za matokeo ya Kura za wawania ridhaa ndani ya Chama,stori hakikuzidi dakika Tatu Na ilikuwa ni kirufurushi.
Je, leo Chadema Na ACT wataweza kupenya Na kutengeneza Habari kuu Kwenye taarifa za Habari za saa mbili Usiku Na saa Moja Usiku Kwenye TV za Tanzania?ama watawekwa Kwenye kundi la Habari za kawaida?
Dotto Bulendu.
2015 Vyombo vya Habari hususani TV viliweka utaratibu mzuri wa namna ya kuandika na kutangaza Habari za Kisiasa hususani uchaguzi mkuu kuanzia hatua ya mchakato ndani ya vyama mpaka Siku ya kutangazwa Kwa mshindi.
TV zilivipa vyama vyote hadhi Na haki Sawa ,ilikuwa ukifungua taarifa ya Habari ya TV,Kama leo stori ya kwanza ni CCM itakayofuata itakuwa ya Chama shindani,na kesho stori ya kwanza itakuwa ya kwanza ya Chama shindani inayofuatia CCM.
Mfano Mmoja wapo walikuwa ITV, walipeleka waandishi upande wa UKAWA Na Upande wa CCM,Na kama leo Kwenye taarifa ya Habari CCM wakitengeneza Habari kuu,basi kesho itakuwa zamu ya Kambi ya vyama shindani.
Mwaka huu imekuwa tofauti kidogo,Jana nilitazama Kwa wakati mmoja taarifa za Habari za TBC,Azam(UTV),Star TV,na ITV ambapo hiyo jana vyama viwili vya upinzani vilikuwa vimeanza Vikao vyao vya juu vya kupitisha majina ya wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na upande wa Zanzibar.
Nilichoshuhudia kilikuwa tofauti kabisa Na zile Siku ambazo CCM ilikuwa inapitisha majina ya wagombea Uraisi,CCM Kwa Siku zote ilitawala maudhui ya Vyombo vya Habari ,Karibu Taarifa ya Habari zote ,stori ya kwanza ilihusu mchakato ndani ya CCM.
Ila kwa Jana, ni Azam (UTV) pekee Kwenye taarifa ya Habari ndiyo waliotoa uzito Kwenye matukio ya Vikao vya vyama vya Chadema Na ACT,Azam waliipa kipaumbele stori ya Chadema Kwa kuifanya Kuwa stori namba Moja Na waliipa Karibu dakika 6,ikafuatiwa na ile ya ACT,Stori ya Chadema Na ACT ilikwenda karibu dakika 12 Kwa uzito ule ule ambao waliupata CCM.
ITV Kwenye taarifa yao ya Habari ya saa mbili stori Hii haikuwa Habari kuu,iliruka baada ya dakika 20,Yaani saa mbili Na dakika 20,Na ilirushwa Kwa mfumo wa kifurushi ambacho hakikuzidi dakika 2 Na sekunde 45 ,Kwenye Uandishi Habari kuwekwa hapo maan yake haina uzito.
Star TV wao waliirusha baada ya dakika 18,Yaani saa mbili Na dakika 18,Na stori hiyo haikuwa Na sauti za wagombea wala taarifa za matokeo ya Kura za wawania ridhaa ndani ya Chama,stori hakikuzidi dakika Tatu Na ilikuwa ni kirufurushi.
Je, leo Chadema Na ACT wataweza kupenya Na kutengeneza Habari kuu Kwenye taarifa za Habari za saa mbili Usiku Na saa Moja Usiku Kwenye TV za Tanzania?ama watawekwa Kwenye kundi la Habari za kawaida?