Kilichomponza Tido Mhando ni uzalendo wake

Kilichomponza Tido Mhando ni uzalendo wake

Akiwa BBC Nairobi miaka hiyo aliingia matatizoni na serikali ya Rais Moi kwa kufichua mauaji ya Robarth Auko. Wakenya wengi na serikali walikuwa wakidhani Tido ni Mkenya lkn kumbe alikuwa ni Mtanzania.

Alikuwa akiwindwa sana na kwa sababu hizo BBC ikamuondoa Kenya na kumpeleka London. Akiwa London alifanya kazi ya utangazaji kwa mafanikio makubwa sana na inaelezwa historia yake haijavunjwa na mtangazaji yeyote kwa kuwahoji viongozi wengi hususan marais tena kwa ujasiri mkubwa. Ikumbukwe aliwahi kumhoji Marehemu Laurent Kabila juu ya uongozi wake usalama wake na usalama wa nchi kwa ujumla na baada ya mahojiano yale haikupita wiki kabila akauwawa.

Kwa wakati huo miaka takriban 50 ya BBC haijawahi kuongozwa na mtu mweusi katika nafasi ya ukurugenzi.

Lkn Tido mhando alifanikiwa kuwa mkurugenzi wa BBC wa kwanza mweusi tena tena mtanzania baada ya yule mama wa kizungu aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo kuhamishwa kwenda kuwa mkurugenzi wa BBC katika bara Asia.

Nikutokana na uchapakazi wake uliomletea sifa na heshima dunia nzima katika fani ya utangazaji ndipo Rais kikwete alipomuomba arudi Tanzania kuja kuboresha kama siyo kukifufua chombo cha habari cha Taifa.

Wakati huo kulikuwa na Radio Tanzania na television ya Taifa TVT zilizounda kitu kilichoitwa taasisi ya utangazaji Tanzania TUT. Ilikuwa ni vigumu sana kumshawishi Tido akubali kazi yake aliyokuwa akilipwa ma pound ya Uingereza lkn hatimae kwa uzalendo wake alikubali kuacha kazi yake na kuja Tanzania.

Alipofika kitu cha kwanza aliomba apewe mamlaka kamili ya kukisuka upya chombo cha Taifa huku akifafanua kwamba ni aibu kwa nchi kama Tanzania kutokuwa na shirika la utangazaji akitolea mfano kama BBC, KBC, UBC, CNN nk.

Ndipo alipopewa mamlaka ya kuisuka na ndio akaanzisha shirika la utangazaji la Taifa TBC. Akafanikiwa kulifanya kuwa shirika pendwa na lenye wapenzi wengi kuliko chombo chochote Tanzania.

Kilichokuja kumponza ni kipindi cha uchaguzi kilipofika alipoanzisha kipindi cha mchakato majimboni.

Kipindi kilikuwa kikiongozwa na yeye mwenyewe na alikuwa akikutanisha wagombea wa CCM na wa upinzani kujinadi pamoja na kuelezea sera zao. Na kisha kuruhusu maswali kwa watazamaji.

Ngoma ilielekea kuwa ngumu sana kwa CCM kutokana na kushambuliwa kila kona na wananchi kwenye maswali ndipo CCM walipogoma kuendelea na kipindi cha mchakato majimboni na wakamwambia Tido akiondoe kipindi kisiendelee.

Tido alikataa akasema ameshasaini mkataba na hakielimu kama wadhamini wakuu wa kipindi hivyo kuuvunja mkataba ni gharama akashauri kama CCM wameamua kujitoa basi yeye ataendelea na ambao wako tayari

Kweli kipindi kiliendelea na kilisaidia wapinzani kupata wabunge wengi na kushuhudia anguko la wabunge wengi maarufu wa CCM kwenye uchaguzi ule. Hivyo kitendo kile hakikuwafurahisha mabwana wakubwa wakamuondoa Tido TBC

Walipomuondoa alichukuliwa na Mwananchi Comunication kama mkurugenzi mkuu ambapo pia alifanya kwa mafanikio makubwa kabla ya kumaliza mkataba wake na kuchukuliwa na Azam Tv. Ambapo kama kawaida yake amefanikiwa kukufanya king'amuzi cha Azam kuwa kinga'amuzi kinachoongoza kwa mauzo mengi kuliko king'amuzi chochote Tanzania.

Sasa pichani hapo chini ni Tido Mhando akiwa amefikishwa mahakamani kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi akiwa TBC. Binafsi nimeumia roho sana maana nimjuavyo Tido ni jembe na CV zake zinamruhusu Kufanya kazi kwenye chombo chochote cha habari duniani kwa nafasi ya ukurugenzi.

Ila kwakuwa mahakama ni chombo cha haki ngoja tuiachie itende haki ila kwakweli inasikitisha sana. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Tido aliondolewa TBC au alimaliza Mkataba wake? Tafadhali fafanua.
 
Masahihisho kidogo

Mh rais kikwete wakati huo hakutengua uteuzi wa bwana tido muhando bali muda wa mkataba wake ulikwisha na aliulizwa na katibu mkuu wa wizara ya habari wakati huo seth kamuhanda kama yeye (tido) anataka kuendelea na mkataba mpya na tido akakubali,japo baadae serikali ikasema tena haioni haja ya kumpa mkataba mpya.

Japo kulikuwa na figisu figisu na msukumo mkubwa wa chama kwa jk kumuondoa tido lakini kuweka rekodi sawa ni "kuwa hakutengua uteuzi wake bali alimnyima mkataba mpya"
 
Kinyongo cha CCM dhidi ya Tido ni pale aliporusha midahalo ya wagombea ubunge majimboni la ajabu CCM waligoma kushiriki wakidai siyo sera yao kuwajuza wananchi juu ya wasifu na malengo ya kugombea ya wateule wao.

Baada ya hapo, JK kwa ghadhabu kubwa alitengua uteuzi wa mwathirika huyu wa umangimeza wa CCM!

Leo azushiwa jinai za manunuzi huku haohao leo wananunua from single source mifano mfukoni lakini.

Hata kandarasi kubwa kubwa waheshimiwa hawa hudai..."waachiwe wao" kwani mkandarasi tayari wanaye mfukoni.

Sijui wako juu ya sheria au kuna nini hapo.

Sheria ya manunuzi inaruhusu single sourcing sasa uhujumu uchumi unachipukia wapi?

Viwanda vya kusulubiana kwa sababu za chuki na vinyongo vya kisiasa ni tishio kwa usalama wa taifa!

Acheni uhasama tujenge nchi, pliiiiiiiiiiz

SAHIHISHO CHA KICHWA CHA HABARI

Siyo uwaziri bali uwazi
Kwani Tido ni Mwanasiasa anayegombea cheo chochote?
 
Visasi havitailetea nchi yetu maendeleo,waliolitia taifa hasara ya mabilioni wanapewa vyeo na kulindwa,huyu Tiddo makubwa aliyolifanyia taifa anadhalilishwa,hata km kulikuwa na mapungufu ya kiutendaji hiyo ni kawaida kazini lakini hakuwa na lengo baya kiasi hicho,milioni 800/?Mungu tusaidie nchi yetu ivuke kipindi hiki cha mpito
 
TVT enzi hizo inawashwa saa sita mchana na kuzimwa saa nne usiku, uku ITV, EATV, DTV zikiwa hewan full time. Dah jamaa kaitoa mbali iyo tv
 
Naona sasa DPP hana kazi za kufanya wanatakumfunga kila mtu. Tido amefanya kazi kubwa na yenye mafanikio katika media.
 
Mkuu unamung'unya maneno ya nini? Nani alishiriki tenda ya Bombadier? Nani alishiriki kwenye tenda ya ujenzi wa uwanja wa ndege Chattle? Je, wao hawatumii madaraka vibaya?
 
Wiki kadhaa nyuma niliiona Azam TV taarifa ya Tundu Lissu akihojiwa na Tido, yalikuwa ni mahojiano marefu sana na ya uwazi.

Nilijua tu siku za Azam TV au Tido zinahesabika.
 
Acha, acha tu! Ulimwengu ndio ulivyo. Tenda mema nenda zako usingoje shukrani.
Hizi nchi za kiswahili ni za kuja kuzikwa tu ukishafika level za kimataifa utaharibu tu CV yako kinachoangaliwa ni siasa binafsi, ufanye watakayo hawa wakoloni weusi, ukisema usimamie kati utaalamu wako haufiki mbali utaharibu tu CV yako.Km yalomkuta mhongo msomi mzuri anaheshimika nje ya nchi,hizi nchi za kiafrica ukiwa mtaalamu na mahiri huwezi fika mbali vikwazo nyingi siasa imewekwa mbele kuliko utaalamu.
 
Bavicha bana eti Tido kaleta uwazi,hapo hapo wanasahau wamejiapiza kutoangalia Tbc yenye huo uwazi
Nadhani ni muda mzuri kujielekeza kwenye kampeni kesho lowassa anazindua mwenyewe,mbeleko ya kijana wake mwalimu
 
Tido anasimama mbali na wanafiki wote

Pasca mayala
Maud kitenge
Tido mhando

Tundu lisu
 
Akiwa BBC Nairobi miaka hiyo aliingia matatizoni na serikali ya Rais Moi kwa kufichua mauaji ya Robarth Auko. Wakenya wengi na serikali walikuwa wakidhani Tido ni Mkenya lkn kumbe alikuwa ni Mtanzania.

Alikuwa akiwindwa sana na kwa sababu hizo BBC ikamuondoa Kenya na kumpeleka London. Akiwa London alifanya kazi ya utangazaji kwa mafanikio makubwa sana na inaelezwa historia yake haijavunjwa na mtangazaji yeyote kwa kuwahoji viongozi wengi hususan marais tena kwa ujasiri mkubwa. Ikumbukwe aliwahi kumhoji Marehemu Laurent Kabila juu ya uongozi wake usalama wake na usalama wa nchi kwa ujumla na baada ya mahojiano yale haikupita wiki kabila akauwawa.

Kwa wakati huo miaka takriban 50 ya BBC haijawahi kuongozwa na mtu mweusi katika nafasi ya ukurugenzi.

Lkn Tido mhando alifanikiwa kuwa mkurugenzi wa BBC wa kwanza mweusi tena tena mtanzania baada ya yule mama wa kizungu aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo kuhamishwa kwenda kuwa mkurugenzi wa BBC katika bara Asia.

Nikutokana na uchapakazi wake uliomletea sifa na heshima dunia nzima katika fani ya utangazaji ndipo Rais kikwete alipomuomba arudi Tanzania kuja kuboresha kama siyo kukifufua chombo cha habari cha Taifa.

Wakati huo kulikuwa na Radio Tanzania na television ya Taifa TVT zilizounda kitu kilichoitwa taasisi ya utangazaji Tanzania TUT. Ilikuwa ni vigumu sana kumshawishi Tido akubali kazi yake aliyokuwa akilipwa ma pound ya Uingereza lkn hatimae kwa uzalendo wake alikubali kuacha kazi yake na kuja Tanzania.

Alipofika kitu cha kwanza aliomba apewe mamlaka kamili ya kukisuka upya chombo cha Taifa huku akifafanua kwamba ni aibu kwa nchi kama Tanzania kutokuwa na shirika la utangazaji akitolea mfano kama BBC, KBC, UBC, CNN nk.

Ndipo alipopewa mamlaka ya kuisuka na ndio akaanzisha shirika la utangazaji la Taifa TBC. Akafanikiwa kulifanya kuwa shirika pendwa na lenye wapenzi wengi kuliko chombo chochote Tanzania.

Kilichokuja kumponza ni kipindi cha uchaguzi kilipofika alipoanzisha kipindi cha mchakato majimboni.

Kipindi kilikuwa kikiongozwa na yeye mwenyewe na alikuwa akikutanisha wagombea wa CCM na wa upinzani kujinadi pamoja na kuelezea sera zao. Na kisha kuruhusu maswali kwa watazamaji.

Ngoma ilielekea kuwa ngumu sana kwa CCM kutokana na kushambuliwa kila kona na wananchi kwenye maswali ndipo CCM walipogoma kuendelea na kipindi cha mchakato majimboni na wakamwambia Tido akiondoe kipindi kisiendelee.

Tido alikataa akasema ameshasaini mkataba na hakielimu kama wadhamini wakuu wa kipindi hivyo kuuvunja mkataba ni gharama akashauri kama CCM wameamua kujitoa basi yeye ataendelea na ambao wako tayari

Kweli kipindi kiliendelea na kilisaidia wapinzani kupata wabunge wengi na kushuhudia anguko la wabunge wengi maarufu wa CCM kwenye uchaguzi ule. Hivyo kitendo kile hakikuwafurahisha mabwana wakubwa wakamuondoa Tido TBC

Walipomuondoa alichukuliwa na Mwananchi Comunication kama mkurugenzi mkuu ambapo pia alifanya kwa mafanikio makubwa kabla ya kumaliza mkataba wake na kuchukuliwa na Azam Tv. Ambapo kama kawaida yake amefanikiwa kukufanya king'amuzi cha Azam kuwa kinga'amuzi kinachoongoza kwa mauzo mengi kuliko king'amuzi chochote Tanzania.

Sasa pichani hapo chini ni Tido Mhando akiwa amefikishwa mahakamani kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi akiwa TBC. Binafsi nimeumia roho sana maana nimjuavyo Tido ni jembe na CV zake zinamruhusu Kufanya kazi kwenye chombo chochote cha habari duniani kwa nafasi ya ukurugenzi.

Ila kwakuwa mahakama ni chombo cha haki ngoja tuiachie itende haki ila kwakweli inasikitisha sana. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Yan kinachomwuma Magufuli na CCM ni kwa sababu Azam hawajaacha kutujuza maendeleo ya Afya ya Tundu Lissu, hakuna sababu nyingine!
 
Back
Top Bottom