Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
KwioKwa Mpira ule mkubwa wanaoucheza AS Vita Club ambao hata Waarabu wenyewe na Mabingwa Afrika Al Ahly wamekiri kupata nao Taabu nimeamini kuwa nje ya Kucheza Mpira mwingi lakini hata Bahati nayo ina nafasi Kubwa mno katika Mafanikio (Ushindi) wa Mchezo wa Soka (Kabumbu) duniani.
Hofu yangu Kubwa tu ni kwamba kwa sasa Watanzania bado tupo katika Kipindi cha Maombolezo (Majonzi) ya Kufiwa na Hayati Mpendwa Rais wetu Dkt. Magufuli hivyo huenda Wapenzi wa Soka Tanzania na hasa wa Klabu ya Simba tusipojiandaa Kikamilifu kuwakabili AS Vita Club basi baada ya tarehe 3 April, 2021 tukawa na 'Double Majonzi' ya Kufiwa na Kiongozi na pia Kutotinga Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika.
Naiamini Klabu yangu ya Simba SC tena kwa 100% Ila kwa Mpira mwingi walionao AS Vita Club tukiwafunga au hata tu kutoka nao Sare ya Suluhu (bila bila) au Pacha (ya Magoli) hatimaye tukafuzu rasmi Robo Fainali Klabu Bingwa Afrika nitaomba Serikali ya Tanzania itoe Tamko la kuwa na Public Holiday nchini.
Moyo wangu una Wasiwasi mwingi sana.