Kila nchi Duniani inapigana na Changamoto zake

Kila nchi Duniani inapigana na Changamoto zake

mcTobby

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2018
Posts
6,631
Reaction score
18,676
Ni ukweli usiopingika, Kila nchi kwa sasa inapigana na shida na Changamoto zake kuanzia za kisiasa na zile za kijamii.

Kwa mfano , sasahivi kuanzia Mexico hadi kule Nepal au Indonesia Changamoto za kisiasa na za kijamii viongozi wanahaha kuzikabili.

Mbaya zaidi kinachonyima Watawala na viongozi Duniani, ni Hii Wave ya Gen Z kama Changamoto ya Kisiasa.

Mexico hadi Morocco ni mwendo wa maandamano. Watu wamechoka. Ni juzi tu hapo kwenye visiwa vya Malagasy Rais aliamua kuikimbia Nchi kutokana na Maandamano.

Huko Nepal ndio usiseme. Haya yote yanatokana na Nini? Jibu ni moja tu. Watawala wameshindwa kuyafikia matarajio na mahitaji ya raia wao.

Mwisho wa siku watu wanaamua kuingia Barabarani. Hapo ndipo nchi inapoamua kujipigania yenyewe pasipo msaada wa kimataifa.

Vita ya hapo Sudani tu AU wameamua kuwa watazamaji pasipo kuingilia au kuchukua Hatua stahiki.

Hata kwa upande wetu kama TZA, tuna matatizo yetu. Kuanzia ya kisiasa na kijamii. Lolote Likitokea tutabaki Sisi kama Sisi kusuluhisha.

Hakuna tena ule ujinga wa nchi nyingine kubeba misalaba isiyowahusu.
 
AU na UN ni syndiates za utapeli mnoo.

Unafiki na uoneaji.

Sasa naelewa kwanini trump anaipiga kila siku UN kwa maneno.

Jiulizs kwanini UN wamekatalia Gaza pekee?
 
AU na UN ni syndiates za utapeli mnoo.

Unafiki na uoneaji.

Sasa naelewa kwanini trump anaipiga kila siku UN kwa maneno.

Jiulizs kwanini UN wamekatalia Gaza pekee?
Kabisa.. kila Nikiona hizi taasis za kimataifa zinavyo operate naona nchi kama nchi za hii dunia Zinahitaji kukabiliana na Changamoto zake yenyewe pasipo kutegemea hawa wanafiki. Congo, Sudan zote wameshindwa kutoa Technical au moral support wameziacha zijifie zenyewe. Halafu wamekomalia Middle East. Hii ni impunity of the highest order
 
Back
Top Bottom