Kikwete unamuogopa Mwakyembe

Kikwete unamuogopa Mwakyembe

Jamani tusidanganyane sababu za uhamisho wa mwakyembe


Kilichofanyika (kumbadilishia portfolio) kimetafsiriwa na wengi kimakosa kwamba ametoswa wakati ukweli sio huo. Sanasana kilichotokea amehamishiwa kwenye wizara ambayo weledi wake, usomi wake na uzalendo wake utatumika kikamilifu na matunda makubwa zaidi kupatikana kwa nchi. Kwa maneno mengine kule aendako atamudu zaidi kulikohata kule atokako.


Na kweli kabisa tukitizama objectively, huku atokako Mhe Mwakyembe alipwaya. Tuache ushabiki- na kuwa move na television stunts za kufukuza wafanyakazi kwenye mikutano ya hadhara, kukamata wezi bandarini, kukamata wauza unga airport na kuchimba mikwara ya hapa na pale- kimsingi Mwakyembe hana accomplishment za msingi katika sekta ya uchukuzi nchini. Nitaelezea kwanini:


Sekta ya Anga
Mwakyembe ameingia madarakani, ATC ilikuwa na hali mbaya, leo anaondoka wizara ile ATC bado ikiwa taabani. Pamoja na jitihada za makampuni kadhaa ya nje kutaka kuingia Ubia na ATCL ikiwemo Turkish Airline, AVIC,Flydubai, Oman Air, Mwakyembe ameshindwa kuwezesha ubia mzuri kutokea ili Shirika hilo liondokane na laana ya kuwa shirika hoi na hatimaye lishindane na mashirika kama Fastjet, Rwandair, n.k- hapo Kenya Airways wala sina haja ya kujilinganisha nayo.


Sekta ya Bandari
kwenye sekta ya bandari Mwakyembe hakufanikiwa kuongeza ufanisi mkubwa uliotegemewa. Kikubwa alichoweza na hapo nampongeza ni kudhibiti wizi wa mizigo. Lakini mengine yote hakufankiwa. Toka aingia hadi anatoka idadi ya mizigo inayopitia bandari ya Dar es salaam ni ile ile container 400,000 kwa mwaka, wakati Bandari ya Mombasa katika kipindi hicho hicho imeongeza idadi maradufu. Kasi ya utoaji mizigo,urasimu na ukiritimba bandarini umeendelea kubaki vilevile,ndio kisa cha jirani zetu Rwanda na Uganda kuamua kuingia kwenye coalition of the willing ya Wakenya ili watumie bandari ya Mombasa. Ni ukiritimba huo umewafanya waone bora waunge mkono mradi wa reli ya kutoka mombasa hadi Nairobi kwa ajili ya kubeba mizigo yao, angali wakijua ni umbari mrefu, na gharama za usafiri zitakuwa kubwa kuliko route ya Dar es salaam......lakini wapi....wakaona bora ya lawama kuliko fedheha ya kutumia bandari ya Dar es saalam.


Wakati waziri Nundu anaondoka, ilikuwepo mipango kamambe ya kuboresha gati no 1-7 na kujenga gati mpya 13 na 14, lakini Mwakyembe toka aingie mipango hiyo imebakia kwenye makaratasi na ahadi hewa za maneno. Wawekezaji wengi wamejitokeza kutaka kufanya miradi hiyo kwa ubia na Serikali, mwakyembe ameshindwa kusimamia hilo litokee..... Ni katika kipindi hicho hicho, wakenya wamepata wabia wa kujenga gati mpya katika bandari ya mombasa- tena wabia hao walishaomba kuingia ubia Dar es aalaam wakapigwa chenga. Ni Mwakyembe huyo huyo, aliyeunda Bodi ya watu wenye weledi, kisha akawafukuza ndani ya miezi sita kwakuwa hawakukubaliana na mawazo ya Menejimenti ambayo Mwakyembe aliiamini na kuitegemea. Ni Mwakyembe huyo huyo ambaye toka ameingia hadi sasa, ameshindwa kusimamia mchakato wa kumpata Mtendaji Mkuu wa Shirika nyeti la Taifa, yaani Mamlaka ya Bandari Tanzania. Muda wote huo nafasi hiyo inakaimiwa (acting)........hakuweza kumconfirm anayekaimu, na kama alidhani hana uwezo anayekaimu, hajaweza kuteua anayefaa.


bandari ya Tanga na Mtwara zimeendelea kuwa bandari njiti zisizokua katika kipindi chote cha Mwakyembe. Bandari ya Bagamoyo imeendelea kuwa njozi ya kufikirika chini ya Uongozi wa Mwakyembe.


kwenye usafiri wa Maziwa, nako hakuna cha kuonyesha cha maana, sana sana kabla hajaondoka meli iliyokuwa inategemewa kwenye ziwa Victoria imesimamishwa (baada ya kuwa neglected miaka mingi kufanyiwa matengenezo, ikiwemo miaka aliyokaa Mwakyembe wizara ya uchukuzi). Kwenye ziwa Nyasa na Tanganyika habari ni ile ile, mile zilizopo zina hali isiyo ya kuridhisha....pengine Mwakyembe angetembelea kule pia, nazo angezifungia.


Reli
kwenye sekta ya reli habari ni ile ile....no progress, mere empty words. Ujenzi wa Reli katika viwango vya kimataifa umebakia kuwa njozi. Kushindwa kwa Mwakyembe kutekeleza mipango madhubuti aliyoiweka kufufua reli ile, kumepelekea Rwanda, Burundi na Uganda (wateja wakubwa wa bandari ya Dsm na reli ya Kati) waachane na Tanzania na kukimbilia mradi wa reli ya Kenya.




kwa analysis hii, ni sahihi kabisa kusema kwamba Mwakyembe, alipwaya kwenye wizara ya Uchukuzi, pamoja na makeke yake yote. Tatizo lake la msingi ni micro-management ya mashirika yaliyo chini yake....


Ninaamini kule alikopelekwa atakuwa na value zaidi....kwani kule anapokwenda anatakiwa mtu mwenye uwezo wa kujieleza, kujenga hoja, na umakini wa kuangalia maslahi ya nchi hayachezewi na nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Bahati nzuri Mwakyembe ameshawahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki.....anaifahamu vizuri process yote ya kule......atatumia weledi wake, ujuzi wake na uzalendo wake vizuri zaidi kule......


sidhani kama analysis yako iko sawa kwasababu inajulikana wazi kwamba taifa hili ni la limeshajifia
 
Jamani tusidanganyane sababu za uhamisho wa mwakyembe


Kilichofanyika (kumbadilishia portfolio) kimetafsiriwa na wengi kimakosa kwamba ametoswa wakati ukweli sio huo. Sanasana kilichotokea amehamishiwa kwenye wizara ambayo weledi wake, usomi wake na uzalendo wake utatumika kikamilifu na matunda makubwa zaidi kupatikana kwa nchi. Kwa maneno mengine kule aendako atamudu zaidi kulikohata kule atokako.


Na kweli kabisa tukitizama objectively, huku atokako Mhe Mwakyembe alipwaya. Tuache ushabiki- na kuwa move na television stunts za kufukuza wafanyakazi kwenye mikutano ya hadhara, kukamata wezi bandarini, kukamata wauza unga airport na kuchimba mikwara ya hapa na pale- kimsingi Mwakyembe hana accomplishment za msingi katika sekta ya uchukuzi nchini. Nitaelezea kwanini:


Sekta ya Anga
Mwakyembe ameingia madarakani, ATC ilikuwa na hali mbaya, leo anaondoka wizara ile ATC bado ikiwa taabani. Pamoja na jitihada za makampuni kadhaa ya nje kutaka kuingia Ubia na ATCL ikiwemo Turkish Airline, AVIC,Flydubai, Oman Air, Mwakyembe ameshindwa kuwezesha ubia mzuri kutokea ili Shirika hilo liondokane na laana ya kuwa shirika hoi na hatimaye lishindane na mashirika kama Fastjet, Rwandair, n.k- hapo Kenya Airways wala sina haja ya kujilinganisha nayo.


Sekta ya Bandari
kwenye sekta ya bandari Mwakyembe hakufanikiwa kuongeza ufanisi mkubwa uliotegemewa. Kikubwa alichoweza na hapo nampongeza ni kudhibiti wizi wa mizigo. Lakini mengine yote hakufankiwa. Toka aingia hadi anatoka idadi ya mizigo inayopitia bandari ya Dar es salaam ni ile ile container 400,000 kwa mwaka, wakati Bandari ya Mombasa katika kipindi hicho hicho imeongeza idadi maradufu. Kasi ya utoaji mizigo,urasimu na ukiritimba bandarini umeendelea kubaki vilevile,ndio kisa cha jirani zetu Rwanda na Uganda kuamua kuingia kwenye coalition of the willing ya Wakenya ili watumie bandari ya Mombasa. Ni ukiritimba huo umewafanya waone bora waunge mkono mradi wa reli ya kutoka mombasa hadi Nairobi kwa ajili ya kubeba mizigo yao, angali wakijua ni umbari mrefu, na gharama za usafiri zitakuwa kubwa kuliko route ya Dar es salaam......lakini wapi....wakaona bora ya lawama kuliko fedheha ya kutumia bandari ya Dar es saalam.


Wakati waziri Nundu anaondoka, ilikuwepo mipango kamambe ya kuboresha gati no 1-7 na kujenga gati mpya 13 na 14, lakini Mwakyembe toka aingie mipango hiyo imebakia kwenye makaratasi na ahadi hewa za maneno. Wawekezaji wengi wamejitokeza kutaka kufanya miradi hiyo kwa ubia na Serikali, mwakyembe ameshindwa kusimamia hilo litokee..... Ni katika kipindi hicho hicho, wakenya wamepata wabia wa kujenga gati mpya katika bandari ya mombasa- tena wabia hao walishaomba kuingia ubia Dar es aalaam wakapigwa chenga. Ni Mwakyembe huyo huyo, aliyeunda Bodi ya watu wenye weledi, kisha akawafukuza ndani ya miezi sita kwakuwa hawakukubaliana na mawazo ya Menejimenti ambayo Mwakyembe aliiamini na kuitegemea. Ni Mwakyembe huyo huyo ambaye toka ameingia hadi sasa, ameshindwa kusimamia mchakato wa kumpata Mtendaji Mkuu wa Shirika nyeti la Taifa, yaani Mamlaka ya Bandari Tanzania. Muda wote huo nafasi hiyo inakaimiwa (acting)........hakuweza kumconfirm anayekaimu, na kama alidhani hana uwezo anayekaimu, hajaweza kuteua anayefaa.


bandari ya Tanga na Mtwara zimeendelea kuwa bandari njiti zisizokua katika kipindi chote cha Mwakyembe. Bandari ya Bagamoyo imeendelea kuwa njozi ya kufikirika chini ya Uongozi wa Mwakyembe.


kwenye usafiri wa Maziwa, nako hakuna cha kuonyesha cha maana, sana sana kabla hajaondoka meli iliyokuwa inategemewa kwenye ziwa Victoria imesimamishwa (baada ya kuwa neglected miaka mingi kufanyiwa matengenezo, ikiwemo miaka aliyokaa Mwakyembe wizara ya uchukuzi). Kwenye ziwa Nyasa na Tanganyika habari ni ile ile, mile zilizopo zina hali isiyo ya kuridhisha....pengine Mwakyembe angetembelea kule pia, nazo angezifungia.


Reli
kwenye sekta ya reli habari ni ile ile....no progress, mere empty words. Ujenzi wa Reli katika viwango vya kimataifa umebakia kuwa njozi. Kushindwa kwa Mwakyembe kutekeleza mipango madhubuti aliyoiweka kufufua reli ile, kumepelekea Rwanda, Burundi na Uganda (wateja wakubwa wa bandari ya Dsm na reli ya Kati) waachane na Tanzania na kukimbilia mradi wa reli ya Kenya.




kwa analysis hii, ni sahihi kabisa kusema kwamba Mwakyembe, alipwaya kwenye wizara ya Uchukuzi, pamoja na makeke yake yote. Tatizo lake la msingi ni micro-management ya mashirika yaliyo chini yake....


Ninaamini kule alikopelekwa atakuwa na value zaidi....kwani kule anapokwenda anatakiwa mtu mwenye uwezo wa kujieleza, kujenga hoja, na umakini wa kuangalia maslahi ya nchi hayachezewi na nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Bahati nzuri Mwakyembe ameshawahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki.....anaifahamu vizuri process yote ya kule......atatumia weledi wake, ujuzi wake na uzalendo wake vizuri zaidi kule......


Pia yale mabehewa ya treni mapya ni mabovu....
 
Ali ahidi kuboresha TAZARA lakini mpaka anaondoka wafanyakazi wanadai mishahara ya miezi mitano na wizara inakwepa kuongea na wafanyakazi ...ngoja wamjaribu EAC
 
Jamani tusidanganyane sababu za uhamisho wa mwakyembe


Kilichofanyika (kumbadilishia portfolio) kimetafsiriwa na wengi kimakosa kwamba ametoswa wakati ukweli sio huo. Sanasana kilichotokea amehamishiwa kwenye wizara ambayo weledi wake, usomi wake na uzalendo wake utatumika kikamilifu na matunda makubwa zaidi kupatikana kwa nchi. Kwa maneno mengine kule aendako atamudu zaidi kulikohata kule atokako.

Bahati nzuri Mwakyembe ameshawahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki.....anaifahamu vizuri process yote ya kule......atatumia weledi wake, ujuzi wake na uzalendo wake vizuri zaidi kule......


MKUU!
Analysis yako ni ya nguvu na inaonyesha undani wa mambo ambayo kweli tunapaswa kuyazingatia katika hili.

Hata hivyo, yapo mengine pia ambayo ni vema tukayaweka hapa na kujadili "objectively" pia kama unavyosema. Na haya ni kama yafuatayo:
1. Suala la Uchukuzi na usafirshaji linagusa maslahi ya watu wenye nguvu kubwa sana ya kiuchumi. Ukiacha viwanda vinavyotengeneza vifaa vya kijeshi, yaani silaha nzito nzito, (hasa kwa nchi zilizoendelea) hakuna sekta yenye nguvu ya kiuchumi kwa nchi kama ya kwetu kama usafirshaji. Hata nchi iwe na rasilimali nyingine za nguvu kama madini nk, suala la uchukuzi na usafirishaji ni uti wa mgongo wa miundo mbinu yote mingine.

Mwakyembe ameingia wizara ile na kukutana na mambo mazito kwelikweli kama uvujaji mkubwa wa makusanyo au makusanyo hafifu kwa uzembe, pamoja na rushwa za aibu kama zile za kupitisha unga kwenye viwanja vya ndege.

Data za kuonyesha udhibiti wa mapato aliouanzisha katika entry points zipo na zinaonyesha mafanikio makubwa tu.

Willingness ya uongozi wa juu serikalini kukubali kutenga rasilimali za ziada ili kuinua sekta ya usafirishaji pia imekuwa questionable. Mwakyembe alishapeleka Action Plan yenye strategies za uhakika za kuinua sekta ya usafirishaji, lakini hadi sasa hakuna aliyeisemea kwa nguvu na kuonyesha commitment ya kutaka iwe na mafanikio zaidi yake mwenyewe! Kwa nini?

Bandari, Viwanja vya ndege, mashirika ya uchukuzi, vyote vinahitaji umakini na msukumo wa dhati wa uongozi uliopo, sio mtu mmoja lakini viongozi wa juu wa chama wanaishia kutuimbia tu "Ilani ya Chama Ilani ya Chama," huku hakuna hatua tunazoona za kumuunga mkono mwenzao.

Mimi sioni tatizo la Mwakyembe kutoa taarifa za uhalifu wa aibu kwenye vyombo vya habari. Manake tusipo fanya hivyo, ni wapi tunapojulishwa kwamba serikali imechukua hatua za kukabiliana na wavusha unga na wezi wengine? Yanabaki kuwa siri na ndio maana wakubwa ndio wanaonyooshewa vidole kuwa wao ndio Ma Drug Lords.

Ukweli utabaki kwamba Watanzania tumekuwa tukifaidika zaidi na uwepo wa Mwakyembe pale uchukuzi hata kama anao uwezo mzuri wa kusimamia mambo ya ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Na wengi tunashawishika kuamini kuwa kuondolewa kwake pale kuna msukumo wa kimaslahi ambao hauna heri kabisa kwa nchi hii. Tusaidiane kupambana nao kwa kushinikiza watu kama Harrison Mwakyembe hata kama sio yeye binafsi, WAWEPO KATIKA MAENEO KAMA LILE ALIPOKUWA!
 
Wauza sembe wameiweka siri kali mfukoni pale air port sasa wanapita bila hofu yeyote.

Usijidanganye Serikali haijalala kiasi hicho. Wenzio wamejaribu kusafirisha kupitia JNIA jana mchana. tena walikuwa wamemeza unga kilo moja moja waulize wapo wapi muda huu.
 
Wauza sembe wameiweka siri kali mfukoni pale air port sasa wanapita bila hofu yeyote.
2. Familia yake na biashara zao zimekuwa kwenye kashfa nzito nzito za kwa ukwepaji kodi

5ceda698ae8811e382ef125cd204e408_8.jpg



Chezee pesa wewe!
 
Dr Harison Mwakyembe alikuwa ni Waziri wa uchukuzi Wizara ambayo imekuwa na matatizo makubwa sana kiutendaji.

Kuanzia Dr Mwakiyembe alipokabidhiwa Wizara hiyo amefanya mambo makubwa sana kuhakikisha Sekta ya uchukuzi inafanya vizuri.

Moja ya mambo ambayo ameyashughulikia kwa nguvu zote ni usafirishaji kwa njia ya Reli ambayo ndio sababu kubwa ya yeye kuondolewa.

Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi ndio wenye Makampuni ya usafirishaji kwa njia ya Barabara na kitendo cha kufuafua usafiri wa Reli ni pigo kubwa kwa watu wenye malori.

Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi wanamiliki Malori mamia kwa mamia na wao ndio wenye tenda ya kubeba mizigo kutoka Viwandani kusambaza mikoani na nje ya Nchi.

Kwa mfano kipindi cha nyuma Cement kutoka Tanga kuja Arusha ilikuwa inasafirishwa kwa njia ya Reli kwa bei nafuu. Lakini sasa hivi ukienda Railway Station utaona Magari ndio yanayo shusha mizigo pale badala ya Train.

Sasa inamaanisha kuwa spidi ya Mwakyembe kufufua Reli ingekuwa ni pigo kwa wasafirishaji wa Malori kwani Train inasafirisha Mizigo kwa bei rahisi sana.

Kuchaguliwa kwa Samwel Sitta ni kuharibu System yote ambayo Dr aliweka kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakua.

Kama Sitta alivyoharibu Mchakato wa Katiba ndivyo atakavyo haribu Wizara ya Uchukuzi na Watanzania tusitegemee jipya ktk Wizara ya Uchukuzi.

Kuondolewa kwa Makyembe ni kwa faida ya Vigogo na Familia zao.

Dawa ya Mwakyembe sio kumtetea na kulalama kila kona! Kama yeye jasiri na mchapakazi anayekataa wezi na waovu, anajua majina yote ya vigogo anaosema wamemwondoa ili kufanikisha biashara zao kupitia 'kuliangamiza' shirika la reli (TRL), au kupitia njia haramu za usafirishaji kama magengo, na 'unga' aiport, na kupitisha nyara au bidhaa mipakani, kwa manufaa yao binafsi, AWATAJE MMOJA BAADA YA MWINGINE, aache woga! la sivyo kama anapiga porojo na woga, atakuwa anawahadaa watanzania, kuwadanganya na kuomba huruma 'ambayo hataipata kwa porojo' bali na kuwasema kiukweli-kweli! "Mwaga mboga nami nimwage ugali!" hatasahaulika akisema ukweli! Kama yeye mzalendo AWATAJE ili vyombo husika, PAC na taasisi nyingine zenye uzalendo zifuatilie na kuwawajibisha viongozi hao na familia zao!
 
Hebu mpigie simu mwakiembe tusikie yeye binafsi anasemaje?
Kupiga kazi vile (kwenye media) mpaka kuwaaminisha watanzania halafu mkuu anakuweka benchi mwaka wa uchaguzi aisee unaweza kuwa kichaa jamani!! Kumbe
Utabiri wa shehe Yahya junior kuwa kuna waziri wa jk atakuwa kichaa mwaka huu una weza kuwa kweli!! Mbona ngafu nkamugwangu!
 
Dawa ya Mwakyembe sio kumtetea na kulalama kila kona! Kama yeye jasiri na mchapakazi anayekataa wezi na waovu, anajua majina yote ya vigogo anaosema wamemwondoa ili kufanikisha biashara zao kupitia 'kuliangamiza' shirika la reli (TRL), au kupitia njia haramu za usafirishaji kama magengo, na 'unga' aiport, na kupitisha nyara au bidhaa mipakani, kwa manufaa yao binafsi, AWATAJE MMOJA BAADA YA MWINGINE, aache woga! la sivyo kama anapiga porojo na woga, atakuwa anawahadaa watanzania, kuwadanganya na kuomba huruma 'ambayo hataipata kwa porojo' bali na kuwasema kiukweli-kweli! "Mwaga mboga nami nimwage ugali!" hatasahaulika akisema ukweli! Kama yeye mzalendo AWATAJE ili vyombo husika, PAC na taasisi nyingine zenye uzalendo zifuatilie na kuwawajibisha viongozi hao na familia zao!

Subutu hajitaki? Nao wana yake kibao.
Cc lara
 
MKUU!
Analysis yako ni ya nguvu na inaonyesha undani wa mambo ambayo kweli tunapaswa kuyazingatia katika hili.

Hata hivyo, yapo mengine pia ambayo ni vema tukayaweka hapa na kujadili "objectively" pia kama unavyosema. Na haya ni kama yafuatayo:
1. Suala la Uchukuzi na usafirshaji linagusa maslahi ya watu wenye nguvu kubwa sana ya kiuchumi. Ukiacha viwanda vinavyotengeneza vifaa vya kijeshi, yaani silaha nzito nzito, (hasa kwa nchi zilizoendelea) hakuna sekta yenye nguvu ya kiuchumi kwa nchi kama ya kwetu kama usafirshaji. Hata nchi iwe na rasilimali nyingine za nguvu kama madini nk, suala la uchukuzi na usafirishaji ni uti wa mgongo wa miundo mbinu yote mingine.

Mwakyembe ameingia wizara ile na kukutana na mambo mazito kwelikweli kama uvujaji mkubwa wa makusanyo au makusanyo hafifu kwa uzembe, pamoja na rushwa za aibu kama zile za kupitisha unga kwenye viwanja vya ndege.

Data za kuonyesha udhibiti wa mapato aliouanzisha katika entry points zipo na zinaonyesha mafanikio makubwa tu.

Willingness ya uongozi wa juu serikalini kukubali kutenga rasilimali za ziada ili kuinua sekta ya usafirishaji pia imekuwa questionable. Mwakyembe alishapeleka Action Plan yenye strategies za uhakika za kuinua sekta ya usafirishaji, lakini hadi sasa hakuna aliyeisemea kwa nguvu na kuonyesha commitment ya kutaka iwe na mafanikio zaidi yake mwenyewe! Kwa nini?

Bandari, Viwanja vya ndege, mashirika ya uchukuzi, vyote vinahitaji umakini na msukumo wa dhati wa uongozi uliopo, sio mtu mmoja lakini viongozi wa juu wa chama wanaishia kutuimbia tu "Ilani ya Chama Ilani ya Chama," huku hakuna hatua tunazoona za kumuunga mkono mwenzao.

Mimi sioni tatizo la Mwakyembe kutoa taarifa za uhalifu wa aibu kwenye vyombo vya habari. Manake tusipo fanya hivyo, ni wapi tunapojulishwa kwamba serikali imechukua hatua za kukabiliana na wavusha unga na wezi wengine? Yanabaki kuwa siri na ndio maana wakubwa ndio wanaonyooshewa vidole kuwa wao ndio Ma Drug Lords.

Ukweli utabaki kwamba Watanzania tumekuwa tukifaidika zaidi na uwepo wa Mwakyembe pale uchukuzi hata kama anao uwezo mzuri wa kusimamia mambo ya ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Na wengi tunashawishika kuamini kuwa kuondolewa kwake pale kuna msukumo wa kimaslahi ambao hauna heri kabisa kwa nchi hii. Tusaidiane kupambana nao kwa kushinikiza watu kama Harrison Mwakyembe hata kama sio yeye binafsi, WAWEPO KATIKA MAENEO KAMA LILE ALIPOKUWA!

Mbatata nakubaliana na hoja yako ya sekta ya uchukuzi kuwa uti wa mgongo. Vile vile, nakubaliana nawe kwamba Mwakyembe alipoingia alikutana na mambo mazito na alifanya jitihada kubwa kuyashughulikia.....lakini tatizo ni kwamba alizama kushughulikia hayo akaacha kushughulikia mambo makubwa strategic katika sekta. Performance ya bandari inapimwa kwa ongezeko la idadi ya mizigo inayopitia hapo, idadi ya meli zinazotia nanga hapo...na sio idadi ya wezi ulioakamata....(sio kuseme kwamba kukamata wezi sio muhimu).

Hoja yako kuhusu action plan, aliipeleka wapi? Kwa nani? Yeye ndiye mwenye dhamana ya utekelezaji wa mikakati yoyte ya wizara, wala haihitaji kupitishwa popote. Ukiangalia mpango wa taifa wa maendeleo wa miaka mitano, ukiangalia BRN zoote zinatilia mkazo umuhimu wa kundeleza Central corridor kama priority-yaani reli ya Kati na bandari ya Dar es salaam......hivyo kilichobaki ni utekelezaj tu.

Kwa bahati nzuri ipo mifano ya mawaziri waliopata mafanikio ambao waliingia kwenye wizara zao wakiwa na mazingira kama ya Mwakyembe.......Prof muhongo ni mmmoja wao.....aliingia wizara ya nishati kukiwa na mchwa, wezi, wahujumu uchumi wa kila aina......lakini alichukua hatua ya kusafisha uozo na kujikita kwenye kufanya mambo makubwa strategic kama vile kuanzisha miradi mipya ya uzalishaji umeme Kinyerezi 3,4, Usambazaji wa umeme(transmission lines), usambazaji wa umeme vijijini, kupitisha sera na sheria zinazotaka uchimbaji wa madini ya vito nchini ufanywe na watanzania peke yake au wakiingia ubia lazima wawe majority shareholders, na processing ya vito ifanyikie nchini, sekta za gesi nayo inatake off. Je Muhongo aliungwa mkono na nani? Magufuli ambaye amejenga kilomita kibao za barabara kuunganisha nchi nzima anaungwa mkono na nani?


Kuhusu kutoa taarifa za uhalifu hakuna ubaya wowote....... sioni shida Mwakyembe kutangaza waalifu japo sina uhakika kama ilikuwa kwenye instrument (masharti ya kazi) ya waziri wa Uchukuzi...au majukumu ya wizara kwa ujumla


Ni kweli Watanzania tumekuwa tukifaidika na uwepo wa Mwakyembe pale uchukuzi, lakini tungefaidika zaidi maradufu kama angetekeleza majukumu makubwa zaidi (strategic).....miradi ya reli, bandari, ndege inge takeoff.....uti wa mgongo uliousema ungekuwa haswa umetimia....kwa sasa wacha tufaidike naye anapokwenda Afrika ya Mashariki.....kuna mambo muhmu na nyeti ya kusimamia kule kwa maslahi ya taifa,sina shaka kanisa na uwezo wake huko.
 
Issue sio kufurahishana...hiyo ni strategic move ya kuweka mtu dhaifu ili mafisadi waweze kupiga hela na kusaidia uchaguzi uende vizuri mwaka huu...bandarini kuna hela ya kutupa na mwakyembe alikuwa mwiba mkubwa..lazima atoke ili mambo yaende vizuri ....

Hivi mzee huyu anatumia kiungo gani kufikiria lakini...!!?? Jambo la maana analifanyia mzaha kweli..??? It is too much now..!!??
 
Kwani uchukuzi ni kwa ajili ya watu wa Kyela???? ubunge ndio unawahusu na vile mlimfanyia kwenye kampeni wakati EL alipojipenyeza kichini chini kumwangusha, ndoa kabisaaa, hana habari na nyie.

poleni lakini.

Swala la kuwaaid meli kyela ni utapeli wao ilikuwa ktk kutafuta kura ila ilikuwa ahadi walioitoa wao bila kushinikizwa na wana kyela hivyo a hadi ni deni lazima watimize na wasipo timiza lazima wapewe hukumu yao, wanakyela co lazima mwakyembe awe m bunge tuna wasomi wengi sana mwakyembe ni sehemu ndogo ya wasomi na wamiliki wa mali wa kyela asipo jirekebisha tutamuadhibu kyela co wavivu tambua hili uvivu kwetu tunatafsili kuwa ni dhambi, kama kijana wetu Harisoni jiangalie poti
 
Mwakyembe kapelekwa huko ili apate uzoefu wa mambo ya kimataifa,kumbukeni ndo mteuliwa wa uraisi kupitia ccm
 
Wewe uanashindwa kuona kwamba alihangaika sana na TAZARA sio ndio inakwenda huko kwenu? na Songwe airport havitoshi tu hivi?

Kaka ninakuambia hivi pr Mark Mwandosya ndie mwekuheshimika mkoa mzima wa mbeya,co mwakyembe .mwandosya jembe ww
 
Hayo mtajuana wenyewe watu wa ccm bhana , mmeshindwa miaka karibu 60 ndio mtaweza miezi 6 ? Hivi humu JF kuna mtu anaamini hawa magamba watafanya zaidi ya haya waliyofanya ?
 
Back
Top Bottom