Jayfour_King
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 1,135
- 128
Kwenye mambo ya msingi ni lazima tuwe pamoja kama wananchi, hizi siasa za upambe ndizo zinatufanya nchi yetu tajiri kuendelea kuwa masikini kwa sababu ya upeo mdogo wa siasa za nchi na ukosefu wa elimu ya uraia kwa wananchi walio wengi. Hii inachukuliwa kama ndio mtaji wa watu wenye nia mbaya kwa nchi yetu na kuendelea kuwahadaa wananchi kwamba wao ndio viongozi watakao wafikisha kwenye nchi ya ahadi wakati ki ukweli wanajua kwamba wanadanganya kwa makusudi na lililo kubwa kwao ni kutafuta mtaji binafsi wao na familia zao na sio nia njema wanayoitangaza kwenye majukwaa ya siasa.
Umefika wakati sasa tuone haja ya kuwa na mgombea binafsi hata ikitokea kwamba hatokuwa na wabunge wa kutosha lakini itasaidia kutoa somo kwenye demokrasia yetu iliyo lala usingizi wa pono. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeanza na maendeleo yatakuwa yanaanza kuchukua uelekeo. Imefikia wakati mtu hakubaliki hata kwenye chama chake mwenyewe lakini kwa kutumia pesa na wapambe hata akiwachosha watu eti tunalazimika mpaka amalize dakika 90 zake, katika nchi zenye uongozi makini huu ni utani na haupaswi kuendelezwa.
Umefika wakati sasa tuone haja ya kuwa na mgombea binafsi hata ikitokea kwamba hatokuwa na wabunge wa kutosha lakini itasaidia kutoa somo kwenye demokrasia yetu iliyo lala usingizi wa pono. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeanza na maendeleo yatakuwa yanaanza kuchukua uelekeo. Imefikia wakati mtu hakubaliki hata kwenye chama chake mwenyewe lakini kwa kutumia pesa na wapambe hata akiwachosha watu eti tunalazimika mpaka amalize dakika 90 zake, katika nchi zenye uongozi makini huu ni utani na haupaswi kuendelezwa.