Kikwete: Nilikwishakabidhi orodha ya 'wauza unga'!

Kikwete: Nilikwishakabidhi orodha ya 'wauza unga'!

Na hili tayari lishafanywa suala la kisiasa...
 
Hakamatwi mtu hapa oooh no hakatwi mtu hapa
 
jk anajaribu kuficha udhaifu wake, kwani waliomkabidhi hiyo list yeye hawakumuona nzowa?? nzowa ni ofisa ktk taasisi ya kuzuia madawa ya kulevya unapomkabidhi jukumu la kupambana na mawaziri na wabunge wauza unga unamaanisha nini?? yaani wewe ndio bosi wao huchukui hatua ila unamkabidhi watu wenye limited power kufanya hivyo. This is called political scapegoating.

Tatizo la jk hataki kuonekana mbaya kwa watu anachofanya ni kusukumia wenzake tu
 
Raisi kikwete naye sasa alipokabidhi hayo majina kunakohusika si ilibidi afuatilie ili aon mwisho wake,mi navyojua mkuu wako akikupa kazi uifanye halafu hujaifanya ,si atauliza kuhusu hiyo kazi aliyokupa?haiwezekani raisi ashindwe kufuatilia jambo nyeti kama hilo,huo si umakini kwa kiongozi anayejua madhara ya madawa ya kulevya,raisi ana madaraka na vyombo vya dola vyote vipo chini yake kwanini anaota matende linapokuja swala nyeti kama hilo?
 
. 
Akizungumza na gazeti hili kupitia kwa Msemaji wake, Salvatory Rweyemamu, Rais Kikwete alisema orodha ambayo alisema anayo alikwishaikabidhi kwa vyombo husika kwa ajili ya hatua zaidi.

“Rais atembee nayo mfukoni ya nini?

KIKWETE.bmp



Chanzo.
MTANZANIA Jumapili

Nchi hii hatukosi kusikia maajabu. Rais anawaomba raia wake wampelekee orodha ya wauza madawa ya kulevya. Akipewa orodha yeye anaipeleka katika vyombo vinavyohusika. Kwanini kuna mzunguko wa aina hiyo? kwanini basi majina yasipelekwe moja kwa moja kwenye vyombo vinavyohusika? au kuna suala la mchujo unaofanywa na ofisi ya rais?
 
Tukubali kwamba ameshaikabidhi kwa watendaji wake...swali ameridhika na namna hiyo orodha ilivyoshughulikiwa??
Kwa maoni ya rais wetu hali ikojekwa sasa......sembe mtaani imepungua?? Kuna mrejesho wowote??
 
Huo ndio uhai wa chama tawala mnatarajia watajiangamiza wenyewe. Thubutu.
 
Tukubali kuwa hii game tumeshindwa,now tusubiri tu zawadi ya besti luza
 
Rais siyo polisi wala siyo mahakama ulitaka afanye nini au awaadhibu kwa sheria ipi tufikili kwanza.
 
Huo ndio uhai wa chama tawala mnatarajia watajiangamiza wenyewe. Thubutu.
 
Ukiona manyoya ya kuku ujue kaliwa huyo
 
Kama majina wanayo wayaweke hadharani ili watuhumiwa wajitetee kama si kweli hawahusiki. Mbona walala hoi wanatajwa nje nje.
Hata hivyo nahisi na wenyewe wamo kwenye hiyo list au waliomo ni wafanyabiashara wenzao hivyo nitaje nikutaje I mean jino kwa. jino
 
Nimechukia sana tena sana!amekabidhi orodha kwa maelekezo gani?wachunguzwe?wapotezewe?au tupigwe changa la macho?sipendi unafki mimi!
 
jk anajaribu kuficha udhaifu wake, kwani waliomkabidhi hiyo list yeye hawakumuona nzowa?? nzowa ni ofisa ktk taasisi ya kuzuia madawa ya kulevya unapomkabidhi jukumu la kupambana na mawaziri na wabunge wauza unga unamaanisha nini?? yaani wewe ndio bosi wao huchukui hatua ila unamkabidhi watu wenye limited power kufanya hivyo. This is called political scapegoating.
Asante mkuu nimejifunza "political scapegoating"
 
Back
Top Bottom