Kikwete ni mhehe wa Iringa?

Whaaaaat????Bigirita;2761484]Mbona nazi zipo tanga, mtwara, newala, moshi...hata kigoma zipo.
Sasa nazi ni mwenyeji wa mkoa gani?[/QUOTE]
 
Wakazi wa asili kabisa wa Bagamoyo ni kina nani?. Wengi wa hao waliopo ni masalia ya watumwa wenye afya duni walio chukukuliwa bara na kutelekezwa hapo sokoni Bwagamoyo hivyo kuloweya hapo.
Tena wengine walitokea Kongo, Malawi na Zambia
 
Kikwete%288%29.jpg


DSCF9890.JPG


Bw.Titus Mussa Kikwete (kulia) akiwa na mdogo wake hawa ni wakazi wa mkoa wa Iringa na wanadai kuwa na mahusiano ya kifamilia na Rais Dkt Jakaya Kikwete na kuwa chimbuko la akina Kikwete ni mkoa wa Iringa,je wewe wajua chimbuko la familia ya Rais Kikwete ni wapi ?

Usikose uhondo huu tembelea JE WAJUA KAMA UKOO WA AKINA KIKWETE CHIMBUKO NI MKOA WA IRINGA? mzee wa matukio daima
haitusaidii ki2, but mkuu wa kaya ni mzee wa chalinze, hao hawana jipya
 
Kihistoria siku za ukoloni mkoa wa Iringa ulikuwa moja ya source ya manamba kwenye kanda zinazozalisha zao la Mkonge ambao kwa kwakati huo Tanganyika ilikuwa jabali namba one duniani kwa uzalishaji wa mkonge. Na wengine walivuka bahari hadi Unguja kulikostawishwa zao la karafuu na kuwa supplier number one duniani.

Kwa vyo vyote uzi wa koo nyingi za mwambao kuunganika na za ukanda wa nyanda za juu na sehemu nyingine nchini si za kusadikika tu, bali ni source za uhakika. Majina kama Kombo utakuta wengi tu huko Iringa nk. Hakuna sababu ya kushangaa au kupinga wakati tunajua karne iliyopita na kurudi nyuma jamii hazikuwa za kusetirika, uhamaji ilikuwa jambo la kawaida kama tufanyavyo siku hizi kwa sababu mbalimbali ikiwemo uchumi, uhasama, vita, na mengineyo.

Yusuf Makamba kuna walioniambia kuna ukoo wake huko Ludewa tarafa za Mlangali na Mawengi ambako ziko koo za akina makamba, ni warefu na weupe kadiri ya mmoja mtafiri alivyonipa data, ila si vizuri kuziweka taswiras hapa kwa vile zinagusa privacy ya watu.

Kipindi cha awamu ya kwanza, kuna baadhi ya jamii zilituhumiana kuhusu baadhi yao kuwa ni wachawi wanaowadhuru. Utawala wa Nyerere uliamua kuwanusuru watu hao kutouawa, na hivyo kuwahamishia sehemu nyingine na kuwa kijiji chao peke yao wanaotuhumiwa kwa uchawi, maana wakikaa wachawi peke yao vigumu kuchawiana. Kuna kijiji fulani moja wapo mkoani Dodoma walikohamishiwa, ila sipendi kukiandika hapa maana baadhi ya waheshimiwa serikalini wanatokana na jamii hizo nisije mwagiwa tindikali.

Tuendelee kujadili.
 
Inawezekana, koo nyingi sana zinaexist in more than one region. Kwani hata ukiangalia maana ya neno kikwete lina maudhui ya kihehe ikimaanisha kimepita. Lakini swala la akina Mgaya wakina mgaya asili yao ni iringa walienda Tanga kipindi cha manamba na wakazaliana huko. Ila kwa swala la Jk kuwa ni wa Iringa sina uhakika sana naamini wataalam wa history watatwambia.

Pale Bagamoyo kulikuwa na soko kubwa la watumwa. Wamisionari walifanya kila wanachoweza kupunguza idadi ya watumwa waliokuwa wanavushwa kwenda Zanzibar kwa safari ya kwenda kuwatumikia mabwana wa ulaya na kwingineko. Walichofanya ni kuwanunua na kisha kuwaficha ndani ya ngome yao ili wasishikwe tena. Ngome ya wamisionari hiyo wananchi waliita Kizuiani kwa vile walizuiwa kutoka kwa usalama wao. Hii ndio maana pale Bagamoyo mission kwenye majengo mengi makuu ya kihistoria ambayo mababu zetu waliishi pale kizuiani walisaidia kujenga panaitwa BAGAMOYO KIZUIANI." Si ajabu mababu wa Kikwete walichukuliwa utumwani toka Iringa na kisha kuokolewa na wamisionari pale Bagamoyo na kuishi kizuiani hadi hali ilipokuwa shwari kuachwa huru. Historia ya nchi hii inatufunza na kuibua mengi yasio kifani.
 
kikwete hata kwenye historia yake yeye mwenyewe alishawahi kueleza kuwa babu yake alihamia bagamoyo akitokea iringa. kwa hao kina mgaya kuwa wanatoka tanga, hao ni wabena, wengi tu na wakiwa kule tanga hawajiiti wasambaa au nini, bado wanajirecognise kama wabena wa njombe iringa...mgaya wote ni wabena wa iringa. wale wa tanga walichukuliwa kama manamba kipindi cha ukoloni kwenda kufanya kazi kwenye mikonge...na hata wakiwa kule tanga wanajitambulisha kama wabena.
 
kikwete hata kwenye historia yake yeye mwenyewe alishawahi kueleza kuwa babu yake alihamia bagamoyo akitokea iringa. kwa hao kina mgaya kuwa wanatoka tanga, hao ni wabena, wengi tu na wakiwa kule tanga hawajiiti wasambaa au nini, bado wanajirecognise kama wabena wa njombe iringa...mgaya wote ni wabena wa iringa. wale wa tanga walichukuliwa kama manamba kipindi cha ukoloni kwenda kufanya kazi kwenye mikonge...na hata wakiwa kule tanga wanajitambulisha kama wabena.
 
haitusaidii ki2, but mkuu wa kaya ni mzee wa chalinze, hao hawana jipya

Haya tunayodharau ndiyo hazina ilipo ambapo tunaweza kujifunza na kujua mengi. vinginevyo tusingekuwa tunajifunza mashuleni somo la historia kwa mtazamo wako kwamba halitusaidii.

Ukitaka kujua ulipo tazama ulikotoka
 
Back
Top Bottom