Sishangai kusikia ahadi zikiongezwa, 2015 si mbali. Sijui mgombea Rais ajaye kutoka CCM ataahidi nini tena. Tuliahidiwa kuishi kama peponi Maisha Bora kwa kila Mtz. 2005 sukari ilikuwa kilo shs 400 leo 2500 nyama kilo 800 leo 6000. Kweli haya ni maisha bora. 2010 tukaambiwa tutatoka Dar mpaka Tabora masaa 2 mpaka 3 kwa treni ya reli ya kati. Leo tunakaa siku 3 njiani tena kwa mbinde watu wamejazana kama magunia ya makopa. Anaendelea kuahidi meli mbili ziwa Victoria, Mheshimiwa Rais wangu. Si ulete moja tu kwanza hiyo ya pili hata ikichelewa tuonyeshe huo mfano?
Mbona nakujua wewe ni mswahili safi tu. Kwenu huwa mnasemaga; "Ada ya mja, kunena tu, muungwana kutenda." Nakuomba tu mtukufu Rais, ngonjera punguza tu baba, tenda zaidi.
CCM tutaikumbuka sana baada ya 2015, kwa;
Kuwatetea mafisadi, Kutetea Wauza sembe ng'ambo baada ya soko la hapa kujaa
Kufukua madini yetu yoote kama kwamba yalikuwa yanalipuka huko ardhini mkaogopa yataua watu wetu.
Kuwaomba Makaburu warudi kwa kasi kuja kugandamiza mazawa yasiyo na uwezo, mpaka waziri anasema uwezo wa mzawa ni kukoroga juice tena inywewe na watu wa kijijini kwani juice zilisoko super markiti ni za South tu.
CCM tutaikumbuka, kwa kuuza nyumba zote za serikali na za viongozi kama kwamba hakuna tena kiongozi ajaye. Ni Ikulu tu imebaki na hata hiyo tuna wasiwasi kuwa huenda tukaambiwa ibaki kama makumbusho ya kitaifa kumbe ishauzwa.
Kweli CCM tutaikumbuka kwa mengi waliyo fanya. Hakuna ambaye hakuyaona.
KIDUMU CHAMA! Sema; KIDUMU. Kwa heri
Mbona nakujua wewe ni mswahili safi tu. Kwenu huwa mnasemaga; "Ada ya mja, kunena tu, muungwana kutenda." Nakuomba tu mtukufu Rais, ngonjera punguza tu baba, tenda zaidi.
CCM tutaikumbuka sana baada ya 2015, kwa;
Kuwatetea mafisadi, Kutetea Wauza sembe ng'ambo baada ya soko la hapa kujaa
Kufukua madini yetu yoote kama kwamba yalikuwa yanalipuka huko ardhini mkaogopa yataua watu wetu.
Kuwaomba Makaburu warudi kwa kasi kuja kugandamiza mazawa yasiyo na uwezo, mpaka waziri anasema uwezo wa mzawa ni kukoroga juice tena inywewe na watu wa kijijini kwani juice zilisoko super markiti ni za South tu.
CCM tutaikumbuka, kwa kuuza nyumba zote za serikali na za viongozi kama kwamba hakuna tena kiongozi ajaye. Ni Ikulu tu imebaki na hata hiyo tuna wasiwasi kuwa huenda tukaambiwa ibaki kama makumbusho ya kitaifa kumbe ishauzwa.
Kweli CCM tutaikumbuka kwa mengi waliyo fanya. Hakuna ambaye hakuyaona.
KIDUMU CHAMA! Sema; KIDUMU. Kwa heri