Huo ukubwa wa eneo letu ndio unaofanya ionekane tunamtandao mkubwa wa barabara, ukifanya proper scalling tunatoka hata nje ya normal distribution curve.Rais , Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema wale wote wanaombeza kuhusu utendaji kazi wake wataona aibu atakapomaliza muhula wake 2015.
Rais ameyasema hayo wakati akizindua mradi wa kusambaza umeme katika mikoa ya Mwanza na Geita unaofadhiliwa na mfuko wa Changamoto wa Milenia(MCC).
Rais amesema Serikali yake itavunja recodi ya kusambaza umeme katika vijiji vingi nchini.
Jk amesema Tanzania inaongoza kwa mtandao wa barabara ambao ni bora afrika mashariki huku akiwahakikishia wakazi wa Kagera kuwa meli mbili alizowaahidi wakati wa kampeni ziko njiani zinakuja.
Rais alikuwa akishangiliwa na wananchi wakati wote wa hotuba yake.
Alisema Tanzania ni nchi kubwa kuliko nchi nyinine za Afrika Mashariki ,lakini ina mtandao mkubwa wa barabara kuliko nchi kama Kenya , lakini akawalaumu watu wanaoisifia nchi hiyo jirani na kubeza mafanikio ya serikali yake.
Aidha, Rais Kikwete amewashangaa baadhi ya viongozi wa CCM pamoja na wananchama kushindwa kuzungumzia mafanikio yaliyofikiwa na serikali ya CCM na badala yake wamekuwa hodari wa kujadili wanapobezwa na wapinzani"
Source: Mwananchi
ndio nitaumbuka sana kama ahadi ya reli ya kati itakuwa imetekelezeka hadi iyo 2015.
Kikwete amejitahidi wala sio unafiki ila ambacho mimi sikifurahii ni kutokudhiti mfumuko wa bei za vyakula maana wananchi wengi hasa wa vijijini wanaumia sana na bei za vitu kama mchele, sukari, maharage nk.
Mkapa aliweza kudhibiti mfumuko wa bei sana, ila wajipange tu vizuri.
Mzee wa porojo, mimi hata huwa sipotezi muda wangu kumsikiliza huyo dhaifu wenu.
Ahadi ni nyingi kuliko uwezo kwani hata iweje hawezi kuzitimiza kwa muda uliobaki!
Chadema wanafanya siasa tu ila wanajua kuwa hakuna raisi bora katika historia ya nchi yetu ya tanzania km jk.
Lazima akumbukwe Jakaya ni Rais gani msikivu kama Jakaya tutampata sie Wanyonge wa Taifa hili? Watoto wa wanyonge waliopata shahada chini ya Mpendwa Jakaya ni wengi kuliko waliopata shahada kuanzia kuumbwa kwa dunia mpaka 2005 kabla hajaingia, Hata Slaa analijua hili, barabara, umeme,maji,demokrasia, uwazi yanazidi awamu zote hata kama utajumlisha. Kwa ufupi Jakaya Success > (Nyerere + Mkapa+Mwinyi) Success.
Kama JK ndy rais bora katika historia ya TZ mpaka sasa, basi hii nchi haijawahi kupata rais.
siku CCM itaacha kuwatetea mafisadi ndio siku hiyo hata mafanikio yake yataonekana ambapo siku hiyo haitafika!
jk amefanya mengi ya maana ila yanachafuliwa na sifa mbaya ya chama chake
Rais Kikwete, atakumbukwa kwa kusaidi watoto wa masikini kusoma elimu ya juu, kuanzia sekondari mpaka vyuo vikuu.
Ahadi ni nyingi kuliko uwezo kwani hata iweje hawezi kuzitimiza kwa muda uliobaki!