Mkuu kama watanzania tungekuwa ni watu wenye kufatilia mambo tungejua ni kwanini angalau barabara zinajengwa? Hivi nchi masikini kama Tanzania inaweza kuiacha reli ife halafu ielekeze nguvu zake kwenye kujenga barabara kweli! Hakuna nchi yenye viongozi sahihi inaweza kununua huu ujinga ni Tanzania tu hili linaweza kutokea!
Hebu tujiulize kwanini barabara lakini siyo reli? Mwakyembe amepiga tambo weeee lakini mkulu hakuna hata siku moja ameonyesha kumuunga mkono! Kuna agenda gani kwanini reli haitakiwi kufufuka? Ni kweli barabara ni rahisi kusafirishia makontena toka dar mpka mwanza,kigari, burundi, kongo nk? Ni kweli tunahitaji barabara kwa ajili ya kuwafikia wakulima kwa urahisi lakini je tunaweza kujenga uchumi mkubwa kwa kusafirisha mizigo kwa barabara kweli?
Magufuli amekuwa akilialia kuhusu magari makubwa kuharibu barabara lakini hata siku moja hadhubutu kusema hilo mbele ya raisi ni kwanini? Anaogopa nini? Kuna masilahi gani kwenye barabara? Barabara zenyewe za mkopo na zimeishi sana ni miaka 2-3 baada ya hapo ni vumbi kama kawaida!
Kwa nini tusiwe na reli imara kwanza ambayo itahakikisha mizigo yote mizito haitatumia barabara na hivyo barabara zitakazojengwa zitadumu kuliko hivi sasa tunajenga barabara za mkopo halafu ndani ya miaka 2 zimechoka na mkopo bado haujalipwa! Nani atakuja kulipa haya madeni ambayo hata investiment zake hazitakuwepo wakati wa kudaiwa?
Kwa maoni yangu raisi anafanya tu ilimradi yeye anatimiza ahadi zake bila kujali hasara na mzigo atakaotuwachia! Kama anataka akumbukwe kweli basi ajenge kwanza reli ili barabara zitakazo jengwa zidumu na mikopo ile ijekulipika bila maswali maana investiment zake zitakuwa bado zinaonekana na kila mtu!