Kikwete: In Black And White

Kikwete: In Black And White

Mimi nimepata kumsikia mtu mzima na asie na hiyana anasema alikuwa na JK mlimani and he was one of the best students academical tangu siku ile namheshimu kwa mambo mawili moja elimu yake na ni rais wa nchi yangu. Ametumiaje elimu yake kwa Taifa labda ndio swali linaloniumiza kichwa... na JK yeye kama yeye sio mtekelezaji wa uchaguzi hapa naona matatizo yapo kwa wasaidizi wake na labda chama chake I am sorry kama nitakuwa nimetumia maneno yasiyofaa.

Kwa maswala yake binafsi kila mmoja wetu ana hulka yake. Hulka ni tabia isiyobadilishika kuna watu ukiwaona kama wanalia... hata awakiwa na furaha..kuna wengine kama wanacheka kumbe wanahuzuni. Kuna wengine wachamungu lakini wafiraji/wasagaji kuna wanaoonyesha wazi kuwa watu watotoz/wanaume kunawanaoficha kwa siri kubwa lakini mwisho wa siku ukichukua idadi ymathalani ya wanaojionyesha wameshatembea na totoz ngapi na wale wanaofanya siri unaweza kupata presha wa siri ikawa mara kumi ya wadhahiri.

Na ushauri mdogo tu msipende maneno ya kusikikia sikia mara nyingi hukuzwa kuliko yanavyotakiwa kuwa.

Mkuu, tupe maoni yako ya ziada katika hayo niliyobold ili tupate uelewa wa juu.
 
Mkuu asante sana. Wengi sasa umetufumbua macho.

Je, kuna chochote unachofahamu juu ya watoto wanaodaiwa JK alizaa na wanawake wengine kama baadhi ya post zinavyojieleza?

wale watoto wake walioko tabata je?mbona hamwasemi wako watatu.mama yao alikuwa anaishi karatu ambaye pia alimtelekeza kwa mda na mama yule alimfungulia kesi,ilibidi Mkwere amtunze mpaka alipo fariki mwaka Juzi mwishoni.

Not only that yule mwanamke mtoto wa mfalme anamtoto mdogo wa kikwete i think the kid is about 5 years now.
 
Jakaya_Kikwete_with_Obamas_cropped.jpg

Jakaya Mrisho Kikwete ni moja kati ya Watanzania wanaogombea kiti cha Urais wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM. Katika kipindi cha miaka 5 iliyopita yeye ndiyo amekuwa Rais wa JMT (Jamuhuri ya Muunganao wa Tanzania).

Lakini je, Kikwete ni nani hasa?

Historia na Uwezo wake ukoje?

Maisha yake yake yakoje?

Thread hii inakusudia kuweka kwa undani yote hayo yanayomhusu in Black and White ili wapiga kura wake waweze kumfahamu kwa undani mbali na propaganda za kisiasa. Na hii ni haki ya Mtanzania.

Kwa kuanzia ninaweka wasifu wake hapa:

Source: Gazeti la Uhuru

RAIS Jakaya Kikwete alizaliwa Oktoba 7, mwaka 1950 katika kijiji cha Msoga, wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani. Ni mtoto wa sita wa Mzee Khalfani Kikwete. Baada ya elimu ya msingi mwaka 1958-1961, Kikwete alijiunga na Shule ya Kati Lugoba mwaka 1962-1965.

Mwaka 1966-1969 alisoma katika Shule ya Sekondari ya Kibaha na mwaka 1971-1972, alisoma kidato cha tano na cha sita katika Shule ya Sekondari ya Tanga. Mwaka 1972-1975 alisoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuhitimu Shahada ya Kwanza ya Uchumi. Alijiunga katika mafunzo ya maofisa wa Jeshi katika Chuo cha Uongozi wa Jeshi Monduli, mwaka 1976-1977 na baadaye Mafunzo ya Makamanda wa Jeshi katika Chuo hicho, mwaka 1983-1984.

Kuanzia shule ya kati, sekondari hadi chuo kikuu alikuwa kiongozi wa wanafunzi. Alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanafunzi katika Shule ya Sekondari Kibaha na baadaye Naibu Kiongozi Mkuu wa Wanafunzi katika Shule ya Sekondari Tanga. Katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikuwa mwanaharakati wa siasa za wanafunzi na alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu hicho, mwaka 1973-1974.

Katika nafasi yake hiyo, alikuwa mstari wa mbele kuchochea vuguvugu la ukombozi kwa nchi za kusini mwa Afrika. Aliwawakilisha wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na vijana wa bara la Afrika katika mikutano ya kimataifa. Miongoni mwa mikutano hiyo ni ule wa International Youth Population Conference mwaka 1974, Bucharest, Romania. Jakaya Kikwete alipata mafunzo ya awali ya kijeshi kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa la Ruvu, na mafunzo ya uofisa wa kijeshi katika Chuo cha Uongozi wa Kijeshi, Monduli. Alifuzu na kuwa luteni 1976-1977.

Nchi ilipoingia katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Kikwete akiwa na cheo cha luteni Kanali, alistaafu jeshini, ili aendelee na siasa. Kikwete amekuwa katika utumishi wa Chama kwa miaka 35 na katika utumishi wa Serikali katika nafasi mbalimbali za Uwaziri kwa miaka 22. Akiwa na umri wa miaka 25, Kikwete alijiunga katika utumishi wa chama cha TANU, kilichoongoza mapambano ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Alianza utumishi akiwa Katibu Msaidizi wa TANU wa Mkoa, mwaka 1975-1977. Baadaye akawa Katibu Msaidizi wa CCM Ofisi Kuu Zanzibar, mwaka 1977-1980; Ofisa utumishi wa CCM Makao Makuu, mwaka 1980-1981; Katibu Mtendaji wa CCM Mkoa wa Tabora, mwaka 1981-1983; Kamisaa wa Siasa katika Chuo cha Uongozi wa Jeshi, Monduli, mwaka 1983-1986 na Katibu wa CCM Wilaya ya Nachingwea na baadaye Masasi mwaka 1986-1988.

Amekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM tangu mwaka 1982, na baadaye Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM hadi sasa. Katika utumishi wa Serikali, Rais Kikwete aliuanza kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Nishati, Madini na Maendeleo ya Maji, mwaka 1988-1990, Waziri wa Nishati, Madini na Maendeleo ya Maji mwaka 1990-1994, Waziri wa Fedha mwaka 1994-1995 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushjirikiano wa Kimataifa mwaka 1995-2005.

Kikwete amekuwa Mbunge wa kuteuliwa (1988-1990), Mbunge wa Bagamoyo (1990-1995) na Mbunge wa Chalinze (1995-2005). Ndani ya Chama, kipaji chake cha uongozi kilichoambatana na moyo wa kujitolea kilijidhihirisha mapema baada ya kumaliza masomo chuo kikuu alipoamua kujiunga na utumishi wa Chama, badala ya kukimbilia ajira serikali kulikokuwa na masilahi makubwa. Hutekeleza kazi kwa ufanisi na uadilifu. Kikwete ni mwanamichezo, mwenye haiba na mvuto na mwenye maono katika uongozi. Ana mke, Salma Rashid Kikwete, na ni baba wa watoto wanane; wanaume sita na wanawake wawili.

Je, ni hayo tu wananchi wanastahili kuyajua?

Kama yako mengine ni yapi?

Jakaya Mrisho Kikwete ni nani hasa in Black and White?

Post yako nimeisoma mpaka palipoandikwa:
Source: Gazeti la Uhuru

Huko kwingine sijasoma kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!
 
Faithful, umeiona post No. 88 ya Mlalahoi?
Nimeiona lakini sijaiona hy evidence inayosema anatembea na wanawake awape madaraka.kama wapo basi ni wachache sana hayo ya kusema ma dc wote na mabalozi wote wanawake wamempa nasema HAPANA na hao wanaume waliopewa madaraka halafu hawafanyi vizuri walitoa nini?acheni hizooo!
 
Nimeiona lakini sijaiona hy evidence inayosema anatembea na wanawake awape madaraka.kama wapo basi ni wachache sana hayo ya kusema ma dc wote na mabalozi wote wanawake wamempa nasema HAPANA na hao wanaume waliopewa madaraka halafu hawafanyi vizuri walitoa nini?acheni hizooo!

Muulize Kikwete aliyewaambia kuwa wakitaka kula lazima nao waliwe
 
wale watoto wake walioko tabata je?mbona hamwasemi wako watatu.mama yao alikuwa anaishi karatu ambaye pia alimtelekeza kwa mda na mama yule alimfungulia kesi,ilibidi Mkwere amtunze mpaka alipo fariki mwaka Juzi mwishoni.

Not only that yule mwanamke mtoto wa mfalme anamtoto mdogo wa kikwete i think the kid is about 5 years now.

Kagemro; hizi facts ni nzito sana . . .

Unaweza kutoa data za hao wa tabata na ni kipindi gani walizaliwa na wana umri gani?

Any details kuhusu mama yao alikuwa anafanya kazi gani enzi za uhai wake na alikufa kwa nini?

Kesi aliyomfungulia kuna details zozote?

Hii ya Mtoto wa mfalme: Please tunaomba details zaidi. Ni yupi, mfalme wa wapi? walikutana wapi na anaishi wapi nk.
 
Post yako nimeisoma mpaka palipoandikwa:
Source: Gazeti la Uhuru

Huko kwingine sijasoma kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!

Mkuu, unakosa mambo . . .

Pitia post zote. Kuna mazuri na mabaya.
 
Nimeiona lakini sijaiona hy evidence inayosema anatembea na wanawake awape madaraka.kama wapo basi ni wachache sana hayo ya kusema ma dc wote na mabalozi wote wanawake wamempa nasema HAPANA na hao wanaume waliopewa madaraka halafu hawafanyi vizuri walitoa nini? acheni hizooo!

Mkuu ninakubaliana na hoja yako kwamba siyo rahisi kwamba wanawake wote aliowateuwa amewapitia. Hii ni ngumu kuweza kuithibitisha, ingawa wapo ambao wamepitiwa na inajulikana wala sio siri.

Wanaume ambao amewateuwa siyo kwamba kuna kitu walimpa, bali walimsaidia katika kufanikisha azima yake ya kuwa Rais [huko ndiko unakoanzia mtandao - kumbuka jinsi wana mtandao walivyosambaratika wengine wakawa mtandao maslahi na wengine mtandao matumaini]. Kwa hiyo hizo appointments za wanawake/wanaume wengi wao wameshiriki kumsaidia kuingia madarakani. Ndiyo maana kila siku analia kwamba watendaji ni wabovu na huku akishindwa kuwawajibisha kwa kuwa hana ubavu wa kuwashughulikia maana wanaweza kumlipua ama kufichua uchafu waliofanya.

Je, wewe ulimfahamu Tom Mwang'onda kabla hajateuliwa na JK kuwa mbunge wa kuteuliwa? Uliwahi kusikia akishiriki siasa mahali popote? Ni kwanini alimteua? Je, alikuwa na sifa za kuteuliwa au ilikuwa ni kumpa ulaji ama kulipa fadhila za yaliyofanywa wakati wa kumuandaa JK kuingia madarakani?

Hakuna appointment ya JK inafanyika hivi hivi, ukichunguza behind the scene kuna key players ambao wanapeleka majina au wanapendekeza nani ateuliwe, na wengine ni wa kwake yeye mwenyewe JK. Upupu wa Salva uko hapa, ukiwa kama ushahidi wa watu waliofanya madudu na wakasahaulika kupewa ulaji na wakaanza kulialia kwamba wamesahauliwa.
 
Mimi nimepata kumsikia mtu mzima na asie na hiyana anasema alikuwa na JK mlimani and he was one of the best students academical tangu siku ile namheshimu kwa mambo mawili moja elimu yake na ni rais wa nchi yangu. Ametumiaje elimu yake kwa Taifa labda ndio swali linaloniumiza kichwa... na JK yeye kama yeye sio mtekelezaji wa uchaguzi hapa naona matatizo yapo kwa wasaidizi wake na labda chama chake I am sorry kama nitakuwa nimetumia maneno yasiyofaa.

Mkuu Sokomoko,

Mimi hapa ndipo ninapochoka kabisa, JK akipita huko kwenye kampeni anasema chama chake na serikali yake wamefanya hiki na kile. Lakini kukitokea mapungufu mnasema ni matatizo ya wasaidizi. Je, nani anateua hao wasaidizi? Mara ngapi baadhi ya wanachama wa CCM wamelalamika kwamba Makamba ameshindwa na kumuomba JK amtoe? Je, JK alisikia hicho kilio cha hao wanachama? Nani wa kulaumiwa hapo?

JK ni Rais ndio anateua mawaziri, wakuu wa mikoa, wilaya na vigogo wengine wa idara za serikali, kwanini hao watendaji wakishindwa kutekeleza majukumu yao anashindwa kuwawajibisha? Kwanini kama anaona wana kasoro au wameshindwa kutekeleza ipasavyo majukumu yao bado anaendelea kuwabeba, ina maana hakuna wengine wenye uwezo wa kufanya hizo kazi?

Kweli mwenye tatizo ni JK mwenyewe na sioni sababu ya kulaumu chama chake wala watendaji wa serikali, maana yeye ndio anawateua. Mfano kwenye Chama, yeye ndio anapendekeza nani awe Katibu Mkuu pamoja na makatibu wa Idara nyingine zote. Sasa kama Katibu amepwaya kwanini asimbadilishe?
 
Rev. Nchi fulani "Muhimu" ni UK na US tu? Mtafute Mlalahoi aje aweke mambo sawa.

Nimenong'onezwa ni Bal Majaar chakula ya Kiwete na mumewe mzee Sharif anajua hilo ndo maana naye alijirusha na yule mbunge wa Singinda! hizi habari hazina uhakika
 
Nimenong'onezwa ni Bal Majaar chakula ya Kiwete na mumewe mzee Sharif anajua hilo ndo maana naye alijirusha na yule mbunge wa Singinda! hizi habari hazina uhakika

kikwete+london+2.jpg



Masanilo, Wabunge wa Kanda ya kati Singida ni Dewji, Msindai, Nyarandu na Missanga. Kuna wa kike? Diana Chilolo ni wa Viti Maalumu na hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha alisoma UK. Kanda ya kati ni ipi? Au Dodoma?
 
Masanilo, Wabunge wa Kanda ya kati Singida ni Dewji, Msindai, Nyarandu na Missanga. Kuna wa kike? Diana Chilolo ni wa Viti Maalumu na hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha alisoma UK. Kanda ya kati ni ipi? Au Dodoma?

lol .... Martha Mlata kasoma UK juzi juzi na alikuwa kwenye blogs kibao kila kukicha akifungua matawi ya CCM huko UK akishirikiana na aliyekuwa Balozi wa hapo aliyetajwa na Mchungaji Masanilo. Kwa hiyo kama Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Singida aliyesoma UK, basi jibu ni hilo mkuu wangu.
 
lol .... Anna Mlata kasoma UK juzi juzi na alikuwa kwenye blogs kibao kila kukicha akifungua matawi ya CCM huko UK akishirikiana na aliyekuwa Balozi wa hapo aliyetajwa na Mchungaji Masanilo. Kwa hiyo kama Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Singida aliyesoma UK, basi jibu ni hilo mkuu wangu.
=======

Na huyu Mama Mlatta alikuwa anaolewa Karagwe-Kagera kwa Prof Runyoro wa UDSM. Aliachwa akawa anafagia kanisa pale Azania Front na baadaye kuimba kwaya. Alitoa CD moja ndiyo ikamweka chati, Mkwere akamuona. Akavutwa sketi mpaka viti maalum. Hivi sasa anakula kuku kwa mrija. Mmewe waq zamani alirudi kumktaka warudiane akarusha, na yeye akagoma kutoma makaratasi ya talaka, kwa hiyo Mkwere anakula lakini hana ruhusa ya kumiliki asiye kufunguliwa mashtaka. Amekaa sana London mwaka jana akisoma kwa sababu elimu ya awali sidhani kama ilikuwa zaidi ya shule ya msingi. Ila na miguu ya kunywea bia ndo maana mkwere aligwaya. Salma hampendi huyo si haba.
 
JK and CCM have managed to steer this country towards peace, harmony and prosperity. Vote CCM, Vote JK!
The opposition folks in this country are full of tribalism, xenophobia, jealousy and racism. When foreigners in this country become successful after years of hardwork and perseverance, majority of you keep on blaming them for bribing the corrupt incumbent politicians, which is absolutely not true! Remember it takes two to tango! In addition, this is a democratic country and therefore you can throw out the party in power through the ballot box. CCM has proved time and time again to be the choice of the majority Tanzanians since independence. Stop whining and being lazy. Work hard and avoid Xenophobia.
Vote CCM, Vote JK:A S 100:
 
Wow!! Even Raj Jr. is in the house. Welcome aboard man. Whatever became of Raj Patel Sr.?
 
Wow!! Even Raj Jr. is in the house. Welcome aboard man. Whatever became of Raj Patel Sr.?

Duhh nilifikiri hujamuona........maana nilikuwa nakuletea hii quote hapa chini
Vote CCM, the choice of the majority of Tanzanians. We have several CCM branches and Reps all over India, UK, US, Canada and all over the world. What's the big deal? If the opposition political parties can not afford to open or establish the party branches or offices, then they need to stop whining. This is a democratic country, and time and time again since independence, Tanzanians have made their choice in Nyerere, Mwinyi, Mkapa and now JK. If you do not like CCM then you can voice your concern in the ballot on election day. If your politician lose the election then you need to take a deep breath, accept the election results and move on. Stop xenophobia. Vote CCM. Vote JK

.....hapa inabidi aje na Mkuu Njabu ndio timu itatimia................
 
Nakupata mkuu. Inawezekana kuna tatizo la kuelewa au sijaeleza kwa undani, au sifahamu ukweli. Ninachofahamu ni kuwa architects wa mpango wote wa kujenga chuo Dodoma ni awamu ya tatu, si awamu ya nne. Awamu ya nne walitekeleza tu yaliyopangwa na awamu ya tatu.

Kuna baadhi ya wenzetu wanaona kufunguliwa chuo na awamu ya nne maana yake wao ndio wamejenga chuo. Kama lilikuwa ni wazo la JK hakuna ubaya nadhani kwa hilo anastahili sifa, lakini hayo mengine hamna kitu.

Mkuu Bongolander, kudanganya ni dhambi, na sidhani kama unataka dhambi hizo tu kwa kutaka kuonyesha uongo. Haiwezekani wazo la kuanzisha Chuo cha Dodoma alitoe Kikwete, halafu useme kuwa kila kitu kilipangwa awamu ya tatu. Inaanza mipango ndio kije chuo, na kama ilianza mipango, ningesema ni Mkapa. Kwa nini kama kafanya Mkapa nikatae, sihitaji dhambi ya uogo, kama kujidanganya nafsi yangu kwa kitu kilicho wazi. Kikwete alilitangaza hili katika kampeni, na haikuwa katika ilani ya CCM. Akasema akiwa Rais atajenga Chuo Dodoma, na kwa kuanzia atatumia majengo ya Chimwaga.

Nitazungumzia uwanja wa Taifa, huu ulianza awamu ya tatu, na ukaisha wakati wa Kikwete ni Rais, huwezi sema kuwa wazo la uwanja wa Taifa lilitoka kwa Kikwete. Pia daraja la Mkapa kama unalijua, wazo halikuanza awamu ya nne, bali awamu zilizopita. Hivyo kwenye ukweli tuwe wakweli, na katika uongo tujitenge nao.
 
Mkuu asante sana. Wengi sasa umetufumbua macho.

Je, kuna chochote unachofahamu juu ya watoto wanaodaiwa JK alizaa na wanawake wengine kama baadhi ya post zinavyojieleza?

Kwa watoto wengine kwelisijui, lakini wanaosema kuna watoto wangetaja majina ya hao watoto na Mama zao. Kwa nini wanaficha, hapa tuwe wawazi na wakweli. Kama unajua mtoto wa JK yuko Magomeni, unamficha wa nini, kumficha ni ufisadi wa nafsi, na kusema yuko wakati hayuko ni uongo wa kifisadi.
 
Back
Top Bottom