Kikwete Hana Mchezo!

Uswe

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,204
626
Nimeona kwa kifupi, TBC walikuwa wanaonesha kwa ufupi ziara ya JK kwa wizara mbalimbali, aisee huyu Mr angekuwa mkali namna hii siku zote nchi yetu ingekua mbali, waziri wa uchukuzi alikua anampiga longo longo za kitoto jamaa akamkatisha katikati ya speech halafu akatema madini ya kutosha, yaani hadi ananifanya nijiulize mara mbili mbili hivi anafanyaga makusudi tu kuwabeba watu wasio na tija au?

Kitu gani kimemsukuma sasa amewawakia, yaani sijui kama hili baraza litamaliza 5 yrs
 
sijawahi ona msanii ambaye hana mchezo

Kwani kaanza leo kuwakia watu kwenye TiiVii?? Aliwawakia akina Mramba na EPA halafu akaenda kumnadi rombo :ballchain:
 
uvccm maslahi @ work. watu wamebanwa na ukali wa maisha wewe unatuambia habari ya mtu anaefanya kazi za Hollywood kuuza sura kila siku kwenye runinga! hayo maigizo ni fani za akina Van Damme.
 
Hana lolote huyu...si ndio zake hizo??asijetake kuwatuliza watu......
 
Umesahau usaniiwa kuyu Kikwete? Hukumbuki 2005 aliingia na mkwara wa kwenda Manzese badae yaliishia wapi?
 
sijui ngoja niendelee kumcheck hizi siku mbili tatu, blv me jamaa alikua hackeck na mtu, kawaka sana, waziri wa nishati alikua anatetemeka tu, ile haikuwa sanaa jamaa alim-mind sana yule waziri, dizaini alitaka kumchakachua halafu Kikwete akashtukia issue dah ilikua mara ya mwisho nimemuona Kikwete kachukia vile ni ile siku ya mgaya wa walimu
 
Nimeona kwa kifupi, TBC walikuwa wanaonesha kwa ufupi ziara ya JK kwa wizara mbalimbali, aisee huyu Mr angekuwa mkali namna hii siku zote nchi yetu ingekua mbali, waziri wa uchukuzi alikua anampiga longo longo za kitoto jamaa akamkatisha katikati ya speech halafu akatema madini ya kutosha, yaani hadi ananifanya nijiulize mara mbili mbili hivi anafanyaga makusudi tu kuwabeba watu wasio na tija au?

Kitu gani kimemsukuma sasa amewawakia, yaani sijui kama hili baraza litamaliza 5 yrs

Hana lolote huyo amepata kikombe kutoka kwa babu sasa amepona. Kama ni kweli angeanza na RA, EL, Mkapa, Chenge et al.
 
Pia waziri wa utumishi wa umma kaonja joto ya jiwe. Na Mkulo kapewa maelekezo kuona namna ya kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma kupunguza makali ya maisha. Ama kweli nguvu ya umma imemwamsha usingizini na sasa anaanza kutekeleza madai ya CDM. Hongera CDM jitihada zinaonyesha dalili ya kuzaa matunda.

Kaza buti mpaka kieleweke na wale wanaobeza chama chetu na wasema sasa la sivyo wanyamaze milele!!!
 
sijawahi ona msanii ambaye hana mchezo

Kwani kaanza leo kuwakia watu kwenye TiiVii?? Aliwawakia akina Mramba na EPA halafu akaenda kumnadi rombo :ballchain:

Wajua JK anapaswa kuitambua kitu kinachoitwa alama za nyakati, Me huwa na mfuatilia sana huyu Rais wetu na huwa anajikanganya sana kwenye hotuba zake ukizikusanya zote utakuta anajipinga hili anakubali lile ambalo alisha lipinga zamani

Kwanini nasema hivyo Tuje tu kwenye wizara ya Miundombinu. JK amekuwa kwenye serikali ya Tanzania kwa muda gani kwanza tujiulize? kwa upeo wake Nchi inaweza endeshwa bila Future strategic plan kweli ? hii inawaingia wananchi akilini kweli Hivi hizi Halimashauli za miji wakati wakifanya mipangomiji hakuna ramini zilizo chorwa na kuonyesha hiki na kile katika maeneo yake?? Wataka kuniambia lini barabara zilifanyiwa upimaji na kuachwa maeneo ya wazi kwa ajili ya kujenga barabara kubwa siku za usoni? na hawa rai wanao gawiwa viwanja vya kujenga kwenye maeneo ya barabara na kukubali kujenga walilijua hilo au watendaji wa JK wasio kuwa na utashi wa kujua kazi zao ni zipi huko halmashauri?

Sasa simwelewi JK anatetea nini au ndiyeye aliyesema tupige kazi tuachana na siasa sasa yeye anatufundisha nini hapo kwa kumwambia magufuli ati waangalie kwa utu khaaa wakati unaplan miji hukujua kuwa sheria ikifika mahali lazima ichukue mkondo wake? sasa unapo fika Rais wa nchi unajisahau kufanya kazi wakati sheria uliiweka ya nini sasa kumbe uzembe wa kuwajibika unaanzia kwako na unawatetea watendaji wako wa halmashauri huko mikoani???

Rais na watendaji wake wanawakanganya wanchi kabisa Katiba ya nchi na sheria zake hazifuatwi JK anajiosha ili akitoka madarakani wasimwone mbaya hataki kabisa aonekane mbaya huku yeye ndie aliwalipa fadhira na sasa ndio hiyo inamkumba na serikali yake kuyumba kabisa na CCM kuwa katika hali mbaya zaidi

 
Nimeona kwa kifupi, TBC walikuwa wanaonesha kwa ufupi ziara ya JK kwa wizara mbalimbali, aisee huyu Mr angekuwa mkali namna hii siku zote nchi yetu ingekua mbali, waziri wa uchukuzi alikua anampiga longo longo za kitoto jamaa akamkatisha katikati ya speech halafu akatema madini ya kutosha, yaani hadi ananifanya nijiulize mara mbili mbili hivi anafanyaga makusudi tu kuwabeba watu wasio na tija au?

Kitu gani kimemsukuma sasa amewawakia, yaani sijui kama hili baraza litamaliza 5 yrs

USANIII TU. Walipanga tangu mwanzo, nitapita mawizarani kwenu, nitawekemea ili nionekane mkali. Ziara zikimaliza tuendelee na kamchezo ketu kalekale "Chukua Chako Mapema
 
Huyu changa la macho tu, Hana lolote. anatafuta mbuzi mwingine wa kafara ili aonekane msafi. kama alivyofanya kwa Dani yona na Mramba! ila mi namuona ni kama mtu anayenuka jasho afu anajipulizia pafyum, wakati dawa yake ni kuoga tu!!
 
Simjui mmiliki wa dowans, sijui kwa nini tanzania ni maskini. By jakaya kikwete.
uvccm maslahi @ work. Watu wamebanwa na ukali wa maisha wewe unatuambia habari ya mtu anaefanya kazi za hollywood kuuza sura kila siku kwenye runinga! Hayo maigizo ni fani za akina van damme.
 
Ukiendelea kuishi kwa usanii, basi jua hata jamii nayo itakuwa hivyo hivyo kabla hawajageuka na kugundua kwamba wanaliwa! A man should look for what is, and not for what he thinks should be.
 
Anajifanya mkali kwenye vitu vidogo vidogo mbona vikubwa anachekelea tu?

Mkuu ndio hapo sasa nashangaa anawafanya watu wote bado watoto na hatujui tunachokifanya...kwa ujumla hajui kuongoza nchi.....zaidi hana jipya hata moja....
 
Jamani aibu meli ya mv liemba kumbe iletwa na mkoloni mjerumani mpaka leo inadunda ziwa tanganyika!naona mjerumani alikua na uchungu sana na hii nchi kuliko hawa watawala wa tanu na ccm!
 
Huyu changa la macho tu, Hana lolote. anatafuta mbuzi mwingine wa kafara ili aonekane msafi. kama alivyofanya kwa Dani yona na Mramba! ila mi namuona ni kama mtu anayenuka jasho afu anajipulizia pafyum, wakati dawa yake ni kuoga tu!!


AU KUJIVUA GAMBA!
:brushteeth:
 
Siasa bwana "Akifanya OOooh Msanii"
Asipofanya mnaandamana
Binafsi siwaelewi watanzania wa JF maana wamejaa uchama kuliko u Taifa.
Upupu mtupu.
 
Watanzania wenzangu tafadhali mnyonge mnyongeni lakini haki yake mwachieni. Kwa hili jambo alifanyalo Jakaya la kupita mawizarani na kuangalia ufanisi wa kazi anastahili pongezi kubwa sana. Watendaji ndiyo wamekuwa wakimuangusha JK na sasa kaamua kuwavalia njuga, nina imani kubwa kwamba hali ya utendaji na uwajibikaji itabadilika kwa kiasi kikubwa.
 
Ni usanii tupu. Labda zaidi kujikosha.
Ishu za kuwakoromea mawaziri wake zilitakiwa ziwe zimefanyika kwenye vikao vya baraza la mawaziri. Hapa anawadanganya wasioelewa utendaji wa serikali. Istoshe angeliwafukuza kazi mawaziri wanaochemsha. Anaendelea kuuonesha ulimwengu kuwa ameimudu sanaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom