KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 86
Kwanza kabisa mtu akinipa heshima ya ukada mimi naipokea kwa taadhima kabisa sina noma wala nini, enzi za Nyerere jamaa mmoja alisema Nampendekeza Julius kuwa Raisi wa jamhuri anayepinga anyooshe mkono, hakuna aliyenyoosha mkono basi Nyerere akawa raisi wa jamuhuri
Aisee kwamba jua ndio limewachosha mimi sikubaliani kabisa, mbona wanene wa CCM hawajachoka?wakati wao wapo kwenye nchi hii pia na jua si linawamulika wao pia? mbona California jua linapiga mwaka mzima lakini watu hawajachoka? mwenye njaa huchoka, mwenye shibe hunawiri.
Maneno yako yana msingi wa kujilinda lakini naona kipindi cha kumpima hakijafika wala hajatimiza nusu ya awamu ya kwanza,huyu mtu ndio kwanza ameanza kujenga si kweli hakuna mabadiliko katika uwajibikaji wa ahadi zake.lakini waswahili wanasema akutukanae hakuchagulii tusi,mnavyotaka nyinyi kuwa mkisema tu basi achukue hatua za kuwakamata na kuwapeleka jela,hilo halipo isipokuwa kwenye nchi za kidikiteta.Muungwana ni kiongozi muadilifu na ni binadamu kama binadamu wengine ,hakuna asiekosea na kila unapokosea ndipo unapojifunza mbinu mpya za kukabiliana na matatizo Tanzania mkae mkijua si kisiwa kama kama kisiwa cha Shelisheli,hivyo kinachotakiwa ni subira ya miaka mitano,hapo Watanzania ndio watampima uwezo wake wapi aliahidi na wapi amefikia na kipi kimekamilika.Haraka haraka haina baraka.
...can you believe jengo la BOT cost 350m USD? hata California lisingecost hivyo ni wizi tuu na rushwa imejaa
Bongo rhumba kali.........
Kuku wa kienyeji hashikiki kwa sasa Jogoo soko la buguruni anauzwa 13,000 - 16,000
kada acha mchezo wewe bongo watu wana njaa ile mbaya mpaka wanatia huruma,does it make sense to you makada wenzako wanatanua na landcruisers za milioni mia mia huku wengine hata hawajui watoto wao watakula nini? na ubaya hizo pesa ni za walipa kodi ndio zinanunua hayo magari ...fikiria vizuri kuna umafia mbaya sana unaendelea nchi ile sio kushabikia tuu,kada najua unakaa nchi za watu ulishawahi kuona seriakli huko ina matumizi ya kununulia maofisa wake magari,mafuta,madereva na nyumba kama Tanzania...its unheard kwa wenzetu na kila mtu aende finance gari lake na mafuta yake na apige gear mwenyewe,lazima ukubali umaskini mwingi umesababishwa na serikali ya CCM inabidi waondoke tuu maana kwa mwendo huu umaskini utazidi...can you believe jengo la BOT cost 350m USD? hata California lisingecost hivyo ni wizi tuu na rushwa imejaa
Maneno yako yana msingi wa kujilinda lakini naona kipindi cha kumpima hakijafika wala hajatimiza nusu ya awamu ya kwanza,huyu mtu ndio kwanza ameanza kujenga si kweli hakuna mabadiliko katika uwajibikaji wa ahadi zake.
Kikwete aliahidi ajira milioni moja, aliahidi kupitia mikataba upya, aliahidi kuboresha maisha, aliahidi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu, aliahidi ujenzi wa miundo mbinu, aliahidi kusaidia michezo nchini, aliahidi kufanya vingi sana...
...
Hali ya wananchi ikazidi kuwa mbaya, mfumuko wa bei zaidi ya asilimia mia mbili kwa bidhaa muhimu, nk /quote]
Zipi? Acha kamba za kitoto!
mkate kutoka 300 alipoingia hadi 600 kwa sasa au unataka zaidi. halafu inawezekana hujui jinsi ya kutafuta inflation wewe. ndio ninyi maodhani inflation ni % ya original bei la sivyo usingeuliza hilo swali
hapana, SIJAUNGA MKONO, bali nimetoa mshangao, niwaunge tela lenu hilo linalosuasua bana msije mkaniacha njiani ! acheni tu nimalizie safari yangu na hao mnaowaita Mafisadi, kwanza kila mtu akibase upande mmoja (haipendezi) nyie kaeni huko huko mlipo, na sie tukae huku tulipo (au nyie mje huku tulipo maana binfasi sina hata chembe ya kusikia kampeni zenu chafu zilizojaa chuki na uwongo,angalau saa nyingine mnakuwa na hoja nzuri)!! hehe ehheeee, lakini ukweli !
Kwa wale ambao wanafuatilia siasa za marekani watakumbuka kuwa miaka ya 90, serikali ya Clinton ilifanikiwa kuweka makubaliano na Korea kaskazini ili wamarekani wawapatie wakorea mafuta na chakula kwa uhakikisho kuwa wakorea wataachana na mipango ya kujenga nyuklia.
Joji Kichaka (ambaye alipondea sana alichofanya Clinton na democrats) alivyoingia madarakani alitishia kuwa angetumia nguvu ili wakorea waache nyuklia na vitisho vingine kibao. Haya, hata miaka haijapita, kichaka amedhihirisha kuwa mtu wa vitisho tu kwani wakorea wamejaribu kwa mafanikio nyuklia yao na pia Kichaka imebidi tu atume watu wakafanye mazungumzo na wakorea.
Mfano huu wa Kichaka na vitisho vya maneno ya democrats ni kitu ambacho Kikwete amejifunza toka kwa rafiki yake joji kichaka na sasa anakitumia Tanzania. Nilifuatilia sana maneno na ahadi za Kikwete wakati wa kampeni za kugombea uraisi. Maneno mengine sio tu yalikuwa kama ahadi za Joji Kichaka bali yalikuwa kama ahadi za mama anayebembeleza na kuhadaa mwanaye ili anyamaze na kulala.
Kikwete aliahidi ajira milioni moja, aliahidi kupitia mikataba upya, aliahidi kuboresha maisha, aliahidi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu, aliahidi ujenzi wa miundo mbinu, aliahidi kusaidia michezo nchini, aliahidi kufanya vingi sana...
Baada ya kuwa raisi, akaomba apelekewe majina wa mafisadi na wauzaji wa madawa ya kulevya, akaanzisha website ili kupokea maoni ya wananchi, akatoa namba za simu ili kupokea maoni ya watu na ahadi kibao.
Wakati watu wakisubiria sera zitekelezwe, waziri wake akasaini mkataba wa Richmonduli, buzwagi, mikataba kibao ya uchunguzi wa madini, nakadhalika. Wakati huo huo ikajulikana kuwa kuna upotevu mkubwa sana wa pesa BOT, akiba kubwa ya pesa za kigeni iliyoachwa na Mkapa ilikuwa ikipotea, nk.
Wakati haya yakiendelea, Kikwete akaanza safari za nje ambazo zimetumia mabilioni ya shilingi za watanzania, ukaguzi wa fedha ukaonyesha kuwa kuna matumizi zaidi ya bilioni moja ambayo hayana uthibitisho wowote huko ikulu, nk.
Hali ya wananchi ikazidi kuwa mbaya, mfumuko wa bei zaidi ya asilimia mia mbili kwa bidhaa muhimu, nk wakati serikali na viongozi wakitumbua mabilioni kwa ufahari wa magari na serikali yenye watu wengi sana (moja ya baraza la mawaziri kubwa kabisa barani Afrika).
Wakati wananchi wakisubiri vitendo, Kikwete anaendeleza trik ya Joji Kichaka (ndio maana hawa ni marafiki) ya kutoa maneno tu ambayo hayana vitendo. Hotuba yake ya Dodoma imejaa ahadi nyingi kuliko hata zile alizotoa wakati wa kampeni.
Kwa mara nyingine tena Kikwete amewadanganya watanzani. Swali ni kwamba, mpaka lini ataendelea kuwahadaa watanzania?
People you are joking. Mnasema miaka miwili haitoshi, katika miaka hii miwili tungeona dalili nzuri lakini tumeone dalili mbaya, kama mkiendelea na hilo la kusema bado, mnaweza hata kusema miaka mitan haitoshi tumuongeze mingine mitano, na kumi ikiisha wendawazimu wanaweza kuanza kusema tubadilishe katiba tuongoeze vipindi vie vitatu. Let us face it people, JK ametudisappoint tuliomchagua, let us admit it. Tusipambe maneno na kujipendekeza nchi yetu inateketea.
"Richmonduli" your freakin azz, godammit!! Wewe kila mada ni kumlaumu tuu Kikwete na lawama hizohizo za kuruduiarudia kila siku. Huchoki?!!! KAMA HUNA JIPYA KAA KIMYA!! PERIOD!
Nani kakwambia rais akiwa kama "mere mortal" anaweza miujiza ya kubadilisha mfumo mzima wa jamii na uchumi katika nchi ya watu milioni 40 kwenye muda wa chini ya miaka miwili? Mwache baba wa watu afanye kazi yake kwa amani.
Folks like you need a regular dose of reality. Nenda soma na kutafakari busara zilizomo kwenye "amri 6" alizoandika Padri Karugendo. If doesn´t help then nashauri urudi Bongo "for genuine reality check" badala ya kukandia serikali huku mmejichimbia Ughaibuni mkivuta muda mpate uraia wa kigeni.
,hivyo kinachotakiwa ni subira ya miaka mitano,hapo Watanzania ndio watampima uwezo wake wapi aliahidi na wapi amefikia na kipi kimekamilika.Haraka haraka haina baraka.
Folks like you need a regular dose of reality. Nenda soma na kutafakari busara zilizomo kwenye "amri 6" alizoandika Padri Karugendo. If doesn´t help then nashauri urudi Bongo "for genuine reality check" badala ya kukandia serikali huku mmejichimbia Ughaibuni mkivuta muda mpate uraia wa kigeni.
hivi wewe ndiyo muda mwingine huwa unajiita kada mpinzani? nataka kujua ili nione kama nikae au nitoke kwenye hii mada