Kikwete atembelea City Hall, apewa barabara

Kikwete atembelea City Hall, apewa barabara

Magazetini

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
593
Reaction score
1,713

Kikwete City Hall.JPG
Katika mwendelezo wa ziara ya Jakaya Kikwete nchini Kenya, leo Rais Jakaya Kikwete ametembelea City Hall Nairobi na kukutana na gavana wa Nairobi, Evans Kidero. Rais Kikwete amesema anaamini ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya utaimarika zaidi kama matokeo ya ziara yake.

Pia Rais Kikwete ameahidi kuendelea kuzuru nchini Kenya hata baada ya kustaafu kwake, Rais Kikwete alifanyiwa sherehe ya kukabidhiwa funguo za kuingilia mji wa Nairobi kama ishara ya upendo. Katika hatua nyingine barabara ya milimani(Milimani road) imebadilishwa jina na sasa itaitwa Jakaya Kikwete Road.

Baada ya hapo, Rais Kikwete alitembelea kiwanda cha magari nchini Kenya, General Motors(GM). Kiwanda hicho kimelalamikia Tanzania kuiwekea vikwazo kwa madai kuwa ni kiwanda cha uunganishaji na sio kutengeneza magari hivyo kutopata nafuu iliyopo kwenye ushirikiano wa Afrika Mashariki. Rais Kikwete akijibu hilo amesema ameona na atarudi kuwaambia watanzania ili kuona jinsi gani watasonga nalo mbele.


 
Last edited by a moderator:
Baada ya OCT 25, hiyo barabara itabadilishwa tena jina na kurudia jina lake la zamani...
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Vema, wametambua mchango wake kwa lipi hadi kumpa heshima kubwa hivyo?
 
Huyu jamaa anapenda sifa sijawahi kuona..... bora anaondoka..angekua wakujifunza tungeua mbali mno maana hakuna anachojifunzaga pamoja na kuzurula kote huko.....
.
.
 
Jamani hilo barabara Wakenya kwani nini wasiandike Ng'wanapagi Highway!!!
 
Kenya wanapata nafasi nzuri ya kuuza bidhaa wanazozalisha Tanzania baada ya ccm kuua viwanda

Big up Kenya!!

Na rais wetu kaenda kutalii viwanda vyao...katembelea kiwanda cha kutengeneza magari kasema akirudi atatuelewesha vizuri watuuziage kirahisi
 
Uzalendo hata kama unampinga Kikwete ni kuhakikisha una support heshima anayopewa nje
ni kwa faida ya Tanzania

Wamarekani woote walilaani pale Bush alipopigwa na kiatu Iraq..
bila kujali ni democrats au Republican

Kikwete kawasaidia sana wakenya...wakimpa heshima ni kitu kizuri kwa kila mtanzania
 
Mchango mmoja wapo ni ule wa kuhakikisha majizi hayapati nafasi ya kuwania urais kupitia ccm

Hapo nadhani kulikuwa na maslahi kidogo, ila ni jambo poa pia. Mimi ni mmoja wa waliochafukwa na Obama, shoga mtarajiwa kupewa jina la barabara ya Ikulu... Ndio maana nahoji na hili pia.

Nina imani na Kikwete though!
 
Huyu jamaa anapenda sifa sijawahi kuona..... bora anaondoka..angekua wakujifunza tungeua mbali mno maana hakuna anachojifunzaga pamoja na kuzurula kote huko.....
.
.
Umesema kweli. Kwa mtu aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nchi za Nje kwa zaidi ya miaka kumi, kutumikia serikali tatu kwa viwango vya juu.....halafu utendaji wake ukawa hivi......kwa kweli hajifunzi.
Halafu...anawazungumzia Kiingereza Wakenya? Speak of exporting Mercedes Benz to Germany!
 
Uzalendo hata kama unampinga Kikwete ni kuhakikisha una support heshima anayopewa nje
ni kwa faida ya Tanzania

Wamarekani woote walilaani pale Bush alipopigwa na kiatu Iraq..
bila kujali ni democrats au Republican

Kikwete kawasaidia sana wakenya...wakimpa heshima ni kitu kizuri kwa kila mtanzania

Humu wengi ni watoto na vichwa moto, hawajui where and when to vomit their frustrations.
 
Mbona uhuru yuko kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi marekani, huyu mwenyeji wake ni nani?
 


... Katika hatua nyingine barabara ya milimani(Milimani road) imebadilishwa jina na sasa itaitwa Jakaya Kikwete Road....

Naona Wakenya wamepitiwa kidogo ... hii barabara ilitakiwa iitwe Prof. Dr. Col. Jakaya Kikwete Road
 
Wamarekani woote walilaani pale Bush alipopigwa na kiatu Iraq..
bila kujali ni democrats au Republican

Hiyo ya 'Wamarekani woote' kwamba walilaani Bush aliporushiwa [vile viatu havikumpata hivyo hakupigwa] vile viatu si kweli.

Kuna idadi kubwa tu ya Wamarekani waliofurahishwa na lile tukio ingawa pia kuna idadi kubwa ya Wamarekani, bila kujalisha itikadi zao za kisiasa, waliolaani kitendo hicho.

 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka aliwapatanisha wakati wa kibaki na raila km sjakosea
 
Duh....ni "revenge"?

Old Bagamoyo road - Mwai Kibaki road, Milimani road - Jakaya Kikwete road,

Ocean road - Barack Obama road

........aende akaage Marekani tuone nako atapewa kitu gani kwa 'heshima' aliyojijengea!
 
Uzalendo hata kama unampinga Kikwete ni kuhakikisha una support heshima anayopewa nje
ni kwa faida ya Tanzania

Wamarekani woote walilaani pale Bush alipopigwa na kiatu Iraq..
bila kujali ni democrats au Republican

Kikwete kawasaidia sana wakenya...wakimpa heshima ni kitu kizuri kwa kila mtanzania
Hii mijitu ya chadema imelewa konyagi saa hizi unadhani kuna anae kuelewa mkuu.
 
Kwa Kenya, hiyo barabara itabadilishwa tena jina muda si mrefu.

But kabla ya huko, milimani rd inawakilisha nini?
 
Back
Top Bottom