hapana the boss, kikwete binafsi ameshindwa kabisa kuonyesha utaifa na uzalendo, alipopewa nafasi ya kuutubia bunge la kenya nimemsikia akisema kuwa uhusiana wa kenya na tanzania utaendelea kuwa imara na rais atakayemfuatia amemtuma akawaambie hivyo wakenya kuwa ataendelea kusimamia misingi ya mahusiano, na akaendelea kusema huyo aliynituma leo atakua anaunguluma arusha na ataongelea kuhusu mahusiano yake na nchi nyingine. wabunge wa kenya nilipwaangalia walipigwa butwaa na kauli hii.
kilichowashangaza ni kwamba wanatambua zahiri kuwa tanzania kwa hivi sasa ipo katika kampeni za uchaguzi mkuu na kuna wagombea kutoka vyama tofauti, haikutarajiwa kikwete aseme eti rais anayefuata amenituma niwahakikishie na pia leo atakua anaunguluma arusha....hapa alikua akimnadi magufuli. mimi nilitarajia aseme kuwa pamoja na ukinzani wa mawazo tulio nao nawahakikishieni kuwa rais awaye yeyote ajaye atasimamia misingi hii ya mahusiano kati ya kenya na tanzania na majirani wengine, maana ndiyo matakwa ya watanzania. lakini yeye kashindwa kufanya jambo la kizalendo kama hilo, kashindwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa na kidemokrasia na kuishia kujipunguza kabisa mbele ya jumuia za kimataifa.
hebu hapo uniambie wewe the boss watanzania tufanye nini ikiwa rais kasahau nafasi yake kwa ajili ya kuendekeza ushabiki binafsi.
Nakumbuka kipindi cha kampeni marekani wakati joji bush anamaliza term yake ya uongozi wa miaka kum alikwenda nchi kadhaa na yeye akaulizwa msimamo wa marekani kuhusiana na mahusiano na mataifa mengine baada ya uchaguzi mkuu, Joji BUSHI alijibu kuwa wasiwe na wasiwasi wamerekani wanatambua umuhimu wa mahusiano hayo na ni jukumu la yeyote atakayeshinda kuyasimamia.
mimi nadhani ungemkosoa kwanza kikwete kwa kitendo cha kutumia jukwaa la kimataifa kufanya kampeni za kumnadi mtu amtakaye na ungemuonya kwa kauli hiyo na athari zake iwapo nchi itaelekea katika machafuko.