Kikwete atembelea City Hall, apewa barabara

Kikwete atembelea City Hall, apewa barabara

Siasa bwana!!!! Tunafurahi jila la barabara kubadirishwa na kuwa la Rais wetu, je mapato yatokanayo na baranara hiyo ni ya kwetu? Acha hizo hata ningekuwa raisi nisingetaka jina langu litumike ovyo
 
Mtu unaonaje ukizungumza lugha ya mtu mwingine, ambaye hamhusiani si kitamaduni wala kirangi, na ndugu yako mnayefanana naye?
Kuna wengine wanaoa ni ufundi na kuonesha umesoma. Kuna sisi wengine twajing'ata vidole kwa kuudhika kuona kuwa hata hicho kitu rahisi hatuwezi kuktamalaki! Halafu eti tumepigania 'kujitawala'
 
sidhani kama kuna faida yoyote kumtukana baba yako mbele ya watu kisa ugali hautoshi wakati ww ni mtu mzima .huu muda woote unaotumia kumtukana hapa na muda mwingine unapoteza kwenye facebook na whatsap unatosha sana kujishughulisha ili angalau upate rizki
 
Watanzania tuna sifa mbaya ya kutothamini vitu vyetu na watu wetu, tujivunie Raisi wetu..najua tutamkumbuka kwa mengi mazuri tu,,,,,,,shida hata wasanii wetu pia wanaheshimika nje kuliko nchini, hebu mabadiliko yaanze na sisi kujikubali na kijithamini..
 
Jamani mmesahau alipowasuluhisha enzi za mwai kibaki
 
Uzalendo hata kama unampinga Kikwete ni kuhakikisha una support heshima anayopewa nje
ni kwa faida ya Tanzania

Wamarekani woote walilaani pale Bush alipopigwa na kiatu Iraq..
bila kujali ni democrats au Republican

Kikwete kawasaidia sana wakenya...wakimpa heshima ni kitu kizuri kwa kila mtanzania

Watanzania wengi bado hawajui siasa, ubinadamu na uzalendo.

Nakumbuka wakati Rais Reagan alipoigwa risasi Nyerere alionyesha masikitiko yake na kumpelekea salamu za kumwombea apone haraka. Kuna watu walilalamika kwa nini Nyerere alifanya hivyo ikizingatiwa kwamba uhusiano kati ya Tanzania na Marekani wakati ule ulikuwa mbaya sana. Ilibidi Nyerere awaeleze wananchi kuwa Reagan ni binadamu kama binadamu yeyote yule.
 
Huyu gavana Evance Kidero ni mchapakazi sana,natamani angepewa uraia awe gavana wa Dar au Dodoma,tofauti na wapiga dili kina silaa..
 
Wakenya wamemuweza. Kapewa Barabara? Basi yeye atatoa almasi! Ukitaka kumweza JK msifie, atatoa kisichotolewa hata bila ya mashauriano na experts, nalijua hili, mtakuja kuniambia!
 
Watanzania wengi bado hawajui siasa, ubinadamu na uzalendo.

Nakumbuka wakati Rais Reagan alipoigwa risasi Nyerere alionyesha masikitiko yake na kumpelekea salamu za kumwombea apone haraka. Kuna watu walilalamika kwa nini Nyerere alifanya hivyo ikizingatiwa kwamba uhusiano kati ya Tanzania na Marekani wakati ule ulikuwa mbaya sana. Ilibidi Nyerere awaeleze wananchi kuwa Reagan ni binadamu kama binadamu yeyote yule.

Viongozi wa marekani muwalinganishe na wazee wa vibakuri!!!
 
Back
Top Bottom