GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

Status
Not open for further replies.

Baada ya kupewa taarifa hizi, aliitisha kikao cha familia, na kuwapa taarifa hizi mbaya kwake, na kikao cha familia kiliamua yafuatayo:

1) Ridhiwani aende mikoa ya kusini kupiga debe la nguvu

2) Salma aende mikoa ya ziwa kupiga debe la nguvu

3) Kikwete alibadilisha ratiba yake ya kampeni na siku alizopangiwa kupumzika zikaondolewa.

Wakuu wa mikoa na wilaya ambazo familia yake watatembelea, walitakiwa kutoa ushirikiano wa hali na mali, ndiyo maana watendaji wa serikali wanadaiwa taarifa za kiserikali na familia kwenye mikoa na wilaya wanapotembelea, wakitumia magari ya serikali yaliyobadilishwa namba.


 
1) Ridhiwani aende mikoa ya kusini kupiga debe la nguvu

2) Salma aende mikoa ya ziwa kupiga debe la nguvu

3) Kikwete alibadilisha ratiba yake ya kampeni na siku alizopangiwa kupumzika zikaondolewa.

This is what we call 'division of labour'....go go go Dr. Slaa
 
Hata kama hizi taarifa siyo za kweli (authentic) lakini inaonekana kuna jambo siyo la kawaida mwaka huu. Ngoja tuendelee kusubiri. Binafsi siziamini 100% ila huyo mleta taarifa nampatia "a benefit of doubt".

Mwaka 2010 unaweza kuingia kwenye historia ya Tanzania,.. as a turning point. Actually not anything but everything is possible! I for one has no reason to doubt 31 10 2010.
 
Habari zilizopatikana ndani ya kikao cha siri kati ya vigogo waandamizi wa usalama wa taifa,Kikwete na Kinana wiki iliyopita zimedokeza kwamba JK amepokea report inayoonyesha kura za Dk Slaa atakazopata october 31 2010.

Mpashaji wa habari amebainisha ya kwamba baada ya JK kupewa tathimini hiyo hakuamini alichoambiwa, zaidi aliongea kwa kiingereza maneno mawili '' Is it?''.

Hii ni taarifa fupi iliyotolewa wiki tatu zilizopita ikulu jijini dar es salaam ikiwa ni mpango wa usalama wa taifa kukamilisha awamu ya kwanza ya utafiti wao kwa baadhi ya mikoa ya kanda ya ziwa, kati, pwani na kaskazini. Machache yameibwa kwenye taarifa hiyo:

Mara: Dr Slaa 59.7%
Mwanza😀r Slaa 58.3%
Kigoma😀r Slaa 52.7%
Singida: Dr slaa 34.7%
Shinyanga: Dr Slaa 43.2%
Kilimanjaro: Dr Slaa 51.7%
Arusha: Dr Slaa 47.1%
Manyara: Dr Slaa 53.8%
Tanga😀r Slaa 46.2%
Dar es Salaam: Dr Slaa 66.4%
Geita: Dr Slaa: 62.7%
Kagera: Dr Slaa 48.2%
Dodoma: Dr slaa 42.4%
Tabora: Dr Slaa 57.6%


Yaani wewe post yako ya kwanza unakuja na habari ambazo sorce yake haijatulia!... wafurahishe wanachadema..
 
Yaani wewe post yako ya kwanza unakuja na habari ambazo sorce yake haijatulia!... wafurahishe wanachadema..
heheheheheheheheh!

Ah na Nape kapewa U DC huko Masasi kwa baba zake
lol, makubwa haya tena! Nape si alipelekwa na serikali ya ccm kusoma? Naona wanamuandaa kuja kuwa Rais wa TZ miaka hiyooo ijayo!
 
Haihitaji tathimini ya USALAMA kujua matokeo ya uchaguzi wa Rais na wabunge Mwaka huu 2010.

Jakaya anajua fika kuwa atashinda kwa kura chache mno ikiwa wafanyakazi watakuwa wamekubali hongo kiduchu ya kuongezewa mishahara hivyo wakatoa kura zao kwa CCM.

Vinginevyo, bado hakuna anayeweza kusimama ndani ya CCM kutamka kuwa mwaka huu wanatakuwa na ushindi wa "SUNAMI" kwa staili ile ile ya chaguzi zilizopita.
 
Ukweli ni kuwa JK ana hali mbaya sana; ndani ya CCM kwenyewe wanaomuunga mkono wengi wao ni wale WACHAFU kisiasa (wahindi wengi na wasio watanzania + watanzania wapenda sifa). JK kanunuliwa helicopter na mhindi (Tanil Somaiya). Kaamua kumtumia Kinana ambaye pia si Mtanzania. Familia imeona hali imekuwa tete ikabidi waanze utawala wa kibabe kwa kumtumia Makamba ambapo mke wake na mwanae wanafuja pesa vibaya sana.

Baadhi ya watu ndani ya TISS wanamuunga mkono Slaa bila kificho, wanakiri JK ni mzigo. Ikitokea akarudi madarakani ajihesabu ana wakati mgumu sana.

Kama ana akili timamu asingesimama na kudai Mramba na Lowassa ni wasafi na tuhuma dhidi yao ni za kinafiki, hii inamaanisha nini wakuu? Nasita kumtukana vibaya kwa maandishi tu, kura yangu ni dawa tosha. Nipo hai, nipo Musoma na nitamnyonga kwa kura tu
 
Kutawala kwa ghariba na uongo huwa umamwisho wake! Mie katika viwango vyangu nimewapa CCM mpaka 2020.
 
Lisemwalo lipo, kama halipo laja. Eee mungu waangazie watanzania waweze kuona mbele wafanye chaguo sahihi.
 
hizi ndizo habari nilizopewa na vyanzo vya ndani kabisa toka usalama wa taifa asilia!
 
hizi ndizo habari nilizopewa na vyanzo vya ndani kabisa toka usalama wa taifa asilia
Kuna usalama wa Taifa aina mbili, nyingine ni hii usalama wa Taifa asilia, patamu hapo! Mbona hukuja na data hizi mapema?
 
Acha kutudanganya, unatuambia usalama wa taifa ili tuamini. Tupe ushahidi bwana hatutaki kuongelea vitu hewa.

Nyie ndo mijitu ya kuchapa viboko 12 kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi.:welcome: Sasa huamini sasa hapo? Hutaki unaacha.
 
Nafikiri cha msingi sana ni kucampaign like never before, inahitajika nguvu ya ziada kumtoa huyu bwana kwenye hicho kiti vinginevyo Tanzania itatumbukia shimoni. We can't afford to have him for another 5 years!!

Jamani wale wote wenye mapenzi na CCM and yet mnaipenda nchi yenu tafadhalini angalieni maslahi ya nchi yenu, watoto wenu na vizazi vya baadae, hawa wanahitaji nchi ambayo ni prosperous na sio ufukara tunaopewa na serikali ya Kikwete. Amkeni leo tuweke uongozi mpya wenye maono ya neema chini ya mwanamapinduzi ya kweli Dr. W. Slaa.

Mtanzania geuka leo tufanye mabadiliko ya kweli, kumbuka waweza kuibadilisha Tanzania kwa kura yako na kuweka historia ya uhuru no.2.
 
Baada ya kupewa taarifa hizi, aliitisha kikao cha familia, na kuwapa taarifa hizi mbaya kwake, na kikao cha familia kiliamua yafuatayo:

1) Ridhiwani aende mikoa ya kusini kupiga debe la nguvu

2) Salma aende mikoa ya ziwa kupiga debe la nguvu

3) Kikwete alibadilisha ratiba yake ya kampeni na siku alizopangiwa kupumzika zikaondolewa.

Wakuu wa mikoa na wilaya ambazo familia yake watatembelea, walitakiwa kutoa ushirikiano wa hali na mali, ndiyo maana watendaji wa serikali wanadaiwa taarifa za kiserikali na familia kwenye mikoa na wilaya wanapotembelea, wakitumia magari ya serikali yaliyobadilishwa namba.

Hii habari ina ukweli kwa sababu katika siku za karibuni ...hasa wiki iliyopita nguvu ya kubandika mabango imeongezwa maradufu ...inaashiria confidence inaendelea kupungua....
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom