Kikwete amenitukana....

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Nasikitika kusema kwamba Rais wangu wa Tanzania amenitusi.Hii imetokea siku ya Ijumaa alipokuwa akihutubia Wazee wa Dar es Salaam.Alinitusi kwa kuniambia uongo huku akiwa anaujua ukweli.Aliniona mimi zuzu.

Alidai kuwa eti mimi nanunua sukari kwa bei chee baada ya Serikali sikivu kushusha bei ya bidhaa hiyo.Ukweli ni kwamba kila uchwao,bei ya sukari inazidi kupaa.Niishipo mimi,kilo moja ni shilingi 2300.

Je,matusi haya kwangu ni kwakuwa amepotoshwa na wasaidizi wake? Je,amewatukana pia na Wazee waliokuwa wakimsikiliza?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
katutukana pia kwa kusema anayeishi nyumba za tembe ni kwa kupenda tuuu!
wakati ukipita kwao msoga zipo kibao! JAMAA HATA HAFIKILIII (ZEZETE TUU!)
 
Wazee nao bana, si wangemuuliza imeshuka wapi?....inawezekana kuwa ni kweli imeshuka lakini Magogoni
 
Kama bei ya sukari ni matusi, na yale ya David Cameron nayo utayaitaje? Au kwa sababu yametamkwa na Mzungu?
 
JK anatumia udhaifu wa watanzania walio wengi, umbumbumbu! eti wanaambiwa hii nchi a.k.a kisiwa cha amani, eti uchumi wetu unakua, eti JK anasafiri nje kila uchao kututafuta wafadhili, eti tumefaulu kutokomeza malaria nk nk.
 
Nasikitika kusema kwamba Rais wangu wa iTanzania amenitusi.Hii imetokea siku ya Ijumaa alipokuwa akihutubia Wazee wa Dar es Salaam.Alinitusi kwa kuniambia uongo huku akiwa anaujua ukweli.Aliniona mimi zuzu.Alidai kuwa eti mimi nanunua sukari kwa bei chee baada ya Serikali sikivu. kushusha bei ya bidhaa hiyo.Ukweli ni kwamba kila uchwao,bei ya sukari inazidi kupaa.Niishipo mimi,kilo moja ni shilingi 2300.Je,matusi haya kwangu ni kwakuwa amepotoshwa na wasaidizi wake? Je,amewatukana pia na Wazee waliokuwa wakimsiliza?

Inabidi tunaofatilia hotuba za Kikwete tukuone wewe kama ulivyoandika mwenyewe hapo juu. Hii hapa ni hotuba ya Kikwete ilippongelea Sukari ni wapi umeyatowa hayo unayosema wewe? au ndi unanihii wenyewe huo?:

Hali ya Uchumi
Ndugu Wananchi;
Katika kuelezea hali uchumi nchini, naomba nianze kwa kuelezea hali ya uchumi duniani kwani yanayotokea nchini yana uhusiano mkubwa na yanayotokea duniani. Hali ya uchumi duniani siyo shwari. Ukweli ni kwamba hali katika uchumi wa mataifa ya Marekani, Ulaya Magharibi na Japan haijatengemaa kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na mdororo wa uchumi wa miaka miwili iliyopita. Hivi sasa uchumi wa mataifa tajiri ya Ulaya , wanachama wa Umoja wa Ulaya na hasa wanachama wa Umoja wa Sarafu ya Euro unapita katika kipindi kigumu na mashaka. Thamani ya sarafu hiyo inashuka na hata kuaminika kwake ni kwa mashaka. Mfumuko wa bei umepanda, ukosefu wa ajira umeongezeka na ipo hofu kubwa ya uchumi wa nchi hizo kudorora tena. Lakini nchi hizi ndiyo masoko makubwa ya bidhaa zetu, watalii na bidhaa za viwandani. Hivyo, athari zao zinatugusa na sisi. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kunaongeza bei ya bidhaa tunazonunua kutoka kwao. Aidha, kutetereka kwa uchumi wao nako kumepunguza masoko ya bidhaa zetu.
Lakini kulegalega kwa sarafu ya Euro kumesaidia kuimarika kwa sarafu ya dola ambayo kabla ya hapo ilikuwa imepungua nguvu. Kwa sababu hiyo thamani ya sarafu ya dola imepanda duniani ikilinganishwa karibu na sarafu nyingine zote pamoja na yetu. Wakati huo huo bei ya mafuta imeendelea kupanda duniani kutoka dola 76.1 kwa pipa Septemba,, 2010 hadi dola 100.5 Septemba, 2011. Jumla ya yote haya ni kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka asilimia 4.2 Oktoba, 2010 hadi asilimia 17.9 Oktoba, 2011.
Ndugu Wananchi;
Serikali na vyombo husika vimekuwa vinachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matatizo ya kushuka kwa thamani ya shilingi, bei ya mafuta, bei ya sukari na matatizo ya umeme. Kuhusu kushuka kwa thamani ya shilingi Benki Kuu imeendelea kuchukua hatua zilizopo ndani ya mamlaka yake hususan kubana ulanguzi wa fedha za kigeni, kudhibiti matumizi ya fedha kigeni kufanyia malipo hapa nchini na kuongeza fedha za kigeni katika masoko ya fedha. Kwa kweli uwezo wao una ukomo. Jawabu la uhakika lipo kwenye uchumi wa mataifa makubwa kuchukua hatua thabiti kuimarisha uchumi wao ili thamani ya dola irejee mahali pake stahiki na bidhaa zetu zipate masoko ya uhakika na bei nzuri ili mapato yetu ya fedha za kigeni yaongezeke.
Kwa upande wa mfumuko wa bei, ni vyema tukatambua kuwa Asilimia 75 ya ongezeko hili imetokana na kupanda kwa bei ya chakula na mafuta. Asilimia 25 iliyobaki imechangiwa na sera za fedha. Kwa upande wa mafuta, tunaamini utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja utasaidia kudhibiti bei za ndani za bidhaa hiyo. Aidha, itsaidia kupunguza makali ya athari ya bei za dunia zinazopanda. Kwa upande wa bei za vyakula, tatizo kubwa ni uhaba wa chakula katika nchi jirani unaosababisha wote kututegema sisi na hivyo kupandisha bei nchini. Tunaendelea kudhibiti magendo ya chakula na wakati huo kutengeneza taratibu rasmi za kuziuzia chakula nchi jirani.
Kwa upande wa sukari tumeamua kuruhusu tani 120,000 ziagizwe ili kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo na kushusha bei yake.


Hatuko Peke Yetu

Ndugu Wananchi;
Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu. Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya. Kwa mfano, mfumuko wa bei kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5. Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa wastani karibu asilimia 5. Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika. Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4. Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7.
 
avatar39905_1.gif
hawa nao wamepanda bei sana hawa....kilo buku saba>!!!
Inabidi tunaofatilia hotuba za Kikwete tukuone wewe kama ulivyoandika mwenyewe hapo juu. Hii hapa ni hotuba ya Kikwete ilippongelea Sukari ni wapi umeyatowa hayo unayosema wewe? au ndi unanihii wenyewe huo?:

Hali ya Uchumi
Ndugu Wananchi;
Katika kuelezea hali uchumi nchini, naomba nianze kwa kuelezea hali ya uchumi duniani kwani yanayotokea nchini yana uhusiano mkubwa na yanayotokea duniani. Hali ya uchumi duniani siyo shwari. Ukweli ni kwamba hali katika uchumi wa mataifa ya Marekani, Ulaya Magharibi na Japan haijatengemaa kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na mdororo wa uchumi wa miaka miwili iliyopita. Hivi sasa uchumi wa mataifa tajiri ya Ulaya , wanachama wa Umoja wa Ulaya na hasa wanachama wa Umoja wa Sarafu ya Euro unapita katika kipindi kigumu na mashaka. Thamani ya sarafu hiyo inashuka na hata kuaminika kwake ni kwa mashaka. Mfumuko wa bei umepanda, ukosefu wa ajira umeongezeka na ipo hofu kubwa ya uchumi wa nchi hizo kudorora tena. Lakini nchi hizi ndiyo masoko makubwa ya bidhaa zetu, watalii na bidhaa za viwandani. Hivyo, athari zao zinatugusa na sisi. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kunaongeza bei ya bidhaa tunazonunua kutoka kwao. Aidha, kutetereka kwa uchumi wao nako kumepunguza masoko ya bidhaa zetu.
Lakini kulegalega kwa sarafu ya Euro kumesaidia kuimarika kwa sarafu ya dola ambayo kabla ya hapo ilikuwa imepungua nguvu. Kwa sababu hiyo thamani ya sarafu ya dola imepanda duniani ikilinganishwa karibu na sarafu nyingine zote pamoja na yetu. Wakati huo huo bei ya mafuta imeendelea kupanda duniani kutoka dola 76.1 kwa pipa Septemba,, 2010 hadi dola 100.5 Septemba, 2011. Jumla ya yote haya ni kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka asilimia 4.2 Oktoba, 2010 hadi asilimia 17.9 Oktoba, 2011.
Ndugu Wananchi;
Serikali na vyombo husika vimekuwa vinachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matatizo ya kushuka kwa thamani ya shilingi, bei ya mafuta, bei ya sukari na matatizo ya umeme. Kuhusu kushuka kwa thamani ya shilingi Benki Kuu imeendelea kuchukua hatua zilizopo ndani ya mamlaka yake hususan kubana ulanguzi wa fedha za kigeni, kudhibiti matumizi ya fedha kigeni kufanyia malipo hapa nchini na kuongeza fedha za kigeni katika masoko ya fedha. Kwa kweli uwezo wao una ukomo. Jawabu la uhakika lipo kwenye uchumi wa mataifa makubwa kuchukua hatua thabiti kuimarisha uchumi wao ili thamani ya dola irejee mahali pake stahiki na bidhaa zetu zipate masoko ya uhakika na bei nzuri ili mapato yetu ya fedha za kigeni yaongezeke.
Kwa upande wa mfumuko wa bei, ni vyema tukatambua kuwa Asilimia 75 ya ongezeko hili imetokana na kupanda kwa bei ya chakula na mafuta. Asilimia 25 iliyobaki imechangiwa na sera za fedha. Kwa upande wa mafuta, tunaamini utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja utasaidia kudhibiti bei za ndani za bidhaa hiyo. Aidha, itsaidia kupunguza makali ya athari ya bei za dunia zinazopanda. Kwa upande wa bei za vyakula, tatizo kubwa ni uhaba wa chakula katika nchi jirani unaosababisha wote kututegema sisi na hivyo kupandisha bei nchini. Tunaendelea kudhibiti magendo ya chakula na wakati huo kutengeneza taratibu rasmi za kuziuzia chakula nchi jirani.
Kwa upande wa sukari tumeamua kuruhusu tani 120,000 ziagizwe ili kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo na kushusha bei yake.


Hatuko Peke Yetu

Ndugu Wananchi;
Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu. Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya. Kwa mfano, mfumuko wa bei kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5. Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa wastani karibu asilimia 5. Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika. Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4. Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7.
 

Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu. Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya. Kwa mfano, mfumuko wa bei kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5. Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa wastani karibu asilimia 5. Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika. Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4. Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7.
Sijui kama Kikwete anajua kuwa hapa alichemka
 


Sijui kama Kikwete anajua kuwa hapa alichemka

Ndio maana hawezi kuwaita ninyi vijana....tatizo watukutu sana halafu "mnajidai" mnajua sana hivyo mtabana kumuuliza

Hivi ukiangalia vile vizee kuna hata mmoja ambae angeweza kuona na kuuliza hilo unaloliona na kuliuliza?

Inabidi angalau mara moja ajitutumue (sijui kama ataweza, labda ataishia wale vijana wa "mashina" ambao wakishavaa kijani wanasahau kila kitu) atuite na sisi vijana hasa kwa kuzingatia kuwa under 35 wanatengeneza karibu zaidi ya 70 % ya population ya Tanzania....hili ndilo kundi la kuongea nalo
 
Back
Top Bottom