Kikwete akae na Kagame wazungumze wayamalize...

Kikwete akae na Kagame wazungumze wayamalize...

Kwelii JK simpendi bt kwa hili hapana aysee he is ryt ILA AACHE KUINGILIA YASIYOMUHUSU.....then kama ugomv bac uwe wa JK na KAGAME na sio TANZANIA NA RWANDA.

kama ni ugomvi binafsi basi angemsubiri atoke madarakani, kikwete ndiyo watanzania. Akitukanwa tumetukanwa wote uwe umempa kura au haujampa. Nakereka sana na kejeli za slim boy, pindi vita rasmi itakapotangazwa nitakuwa wa kwanza kwenda kigali kukileta kichwa cha kagame
 
mkuu inaonyesha ww nisehem yatatizo,naunatumika kutengeneza propaganda za Rwanda,hivi mh.kikwete anakosa gani kwa ushauri alio utoa?acha ujinga,kama ww unagombana namkewako kila siku,majirani wakakushauri utawajiaju? ama unaweza kkubali ama kukataa ushauri wao.

Hakuna popote niliposema kuwa Kikwete ana makosa, ndipo akaongee na Kagame. Na hata Kikwete alipomshauri Kagame akaongee na FDLR hakumaanisha kuwa Kagame ana makosa. Maana hizi hasira tunazozionyesha hapa kuhusu Kikwete kukaa na Kagame na kuongea, ndizo hizo hizo alizozionyesha Kagame aliposhauriwa na Kikwete.
Diplomasia ni somo...
 
Chokochoko kati ya Tanzania na Rwanda zinazidi kuongezeka
Tunawahitaji majirani zetu zaidi ya tunavyowahitaji wachina na wamarekani
Jana tulikuwa tunajibizana na Malawi, leo Rwanda; Kesho itakuwa Kenya, na keshokutwa Uganda...
Hatutafika mahali...

Kama vile Kikwete alivyomshauri Kagame, kwa roho safi na kwa nia njema kabisa kuwa akae na FDLR waongee, nami basi napenda kumshauri Kikwete, kwa roho safi na kwa nia njema, akae na Kagame waongee, wayamalize, tuendelee kuwa na ujirani mwema...

Upuuzi gani huu, mtu akikushauri upatane na mke wako naye anakuwa adui yako? kama hautaki ushauri si upotezee.
 
Haijawahi tokea duniani mtoa ushauri aombe radhi au asuruhishwe kwa ugomvi wa kutoa ushauri

Suala sio kuombana radhi, bali ni kueleweshana pale ambapo hawakuelewana... then ujirani mwema uka-resume...
 
dharau za wanyarwanda,dhidi ya kiongozi wetu.wajinga hawakumbuki mzigo wa wakimbizi na uvunjivu wa sheria za nchi zilizotokana na wakimbizi hao toka rwanda.huku wakiharibu uoto wa asili na viumbe hai walioishi kwenye mapori ya nyakanazi ,mtabira,makere na eneo zima la uvinza.mkoani kigoma.NAUNGA MKONO KAULI YA RAISI WETU,AKAE KIMYA WALA ASIONGEE NA WAJINGA KAMA KAGAME.TANZANIA HATUTARAJII KUPOKEA TENA LUNDO LA WAKIMBIZI TOKA HUKO.

Mtoto akikunyea mkono huukati na kumbuka mwenzio akinyolewa wewe tia maji.
Kama majirani zetu, tunahitaji mahusiano mema na Wanyarwanda in one way or another...
 
Hakuna popote niliposema kuwa Kikwete ana makosa, ndipo akaongee na Kagame. Na hata Kikwete alipomshauri Kagame akaongee na FDLR hakumaanisha kuwa Kagame ana makosa. Maana hizi hasira tunazozionyesha hapa kuhusu Kikwete kukaa na Kagame na kuongea, ndizo hizo hizo alizozionyesha Kagame aliposhauriwa na Kikwete.
Diplomasia ni somo...

Mbona unajikanyaga kanyaga sana wewe? Utatafutaje suluhu na mtu kwa sababu tu eti umempa ushauri na akakuona adui? ushauri ukitolewa kuna mambo mawili tu kuukubali au kuukataa sasa haya ya JK akaye na Kagame yanatoka wapi? huoni unatafuta ugomviusiyo na maana? Hebu tujaribu kushughuisha vichwa vyetu badala kukurupuka tu na mada ambazo hazina kichwa wala miguu.
 
matusi wanayotutukana wanyarwanda na kagame huyaoni? au ndiyo yale yale mkuki kwa nguruwe mtamu lakini kwa binadamu mchungu.

Na ndiyo maana nasema kuna umuhimu hii hali ya kutukanana na majirani zetu ikamalizwa kidiplomasia... Tutatukanana weee, alafu iweje...
 
kama ni ugomvi binafsi basi angemsubiri atoke madarakani, kikwete ndiyo watanzania. Akitukanwa tumetukanwa wote uwe umempa kura au haujampa. Nakereka sana na kejeli za slim boy, pindi vita rasmi itakapotangazwa nitakuwa wa kwanza kwenda kigali kukileta kichwa cha kagame

Kwa lipi tupigane... kama tunaweza kupatana?...
 
Chanzo cha ugomvi wao hakina maana kabisa!

Watakuwa wana mambo yao Binafsi, .............eheee nimekumbuka jambo!!! hivi Nguza Vicking anaendeleaje? kitambo sana sijasikia tena habari zake kama watakata rufani au la!!
 
Rais Kagame ni lazima atalipa kwa kitendo chake alichokifanya huko Darfur!

Damu za Wanajeshi/ndugu wetu haziwezi kupotea bure, kitendo alichokifanya ni chakinyama na kauli zake za kwamba atatuchapa haziwezi kufumbiwa macho zikapita hivi hivi!

Nilazima kuhahkikisha haya mambo hayatokei tena, na wanajeshi wetu wakulinda amani wawe salama dhidi ya adui yoyote yule!

Kagame wewe ni shetani, na unastahili moto!
 
Chokochoko kati ya Tanzania na Rwanda zinazidi kuongezeka
Tunawahitaji majirani zetu zaidi ya tunavyowahitaji wachina na wamarekani
Jana tulikuwa tunajibizana na Malawi, leo Rwanda; Kesho itakuwa Kenya, na keshokutwa Uganda...
Hatutafika mahali...

Kama vile Kikwete alivyomshauri Kagame, kwa roho safi na kwa nia njema kabisa kuwa akae na FDLR waongee, nami basi napenda kumshauri Kikwete, kwa roho safi na kwa nia njema, akae na Kagame waongee, wayamalize, tuendelee kuwa na ujirani mwema...
Ni hatari sana mtu anapewa ushauri anaukataa halafu eti wakae waongee, ili iweje kwani TAnzania na RWanda tuna ugomvi kama hata ushauri si aache.
 
Rais Kagame ni lazima atalipa kwa kitendo chake alichokifanya huko Darfur!

Damu za Wanajeshi/ndugu wetu haziwezi kupotea bure, kitendo alichokifanya ni chakinyama na kauli zake za kwamba atatuchapa haziwezi kufumbiwa macho zikapita hivi hivi!

Nilazima kuhahkikisha haya mambo hayatokei tena, na wanajeshi wetu wakulinda amani wawe salama dhidi ya adui yoyote yule!

Kagame wewe ni shetani, na unastahili moto!

Darfur tena?!!!
 
Me nashindwa kuelewa diplomats kazi yake nn, kagame kamtukana sana kikwete, na hakuna aliyeinua mdomo hata kusema chochote, hata waziri wa mabmo ya nje yupo kimya au ndio kuepusha mengine?? hapana upole uliopitiliza ni ujinga, huyu kagame tumuonyeshe sisi ni nani, tuna marafiki wengi, tumewasidia wengi (hata wanyarwanda) kikwete simpendi na wala simkubali(kwa sababu ya udhaifu wake kiuongozi) lakini anapotukanwa na kudharilishwa na kagame ni sisi sote kama nchi tumedharauliwa
 
Darfur tena?!!!

Unashangaa nini Tuko?!!

Huo ndio ukweli mkuu, inawezekana wewe ujui kilichotokea huko? hakuna waasi wala nini? ni mipango ya Kagame hiyo!
 
Last edited by a moderator:
kwani nani kagombana na Rwanda kama siyo wendawazimu wa KAGAME.

Unajua tunavyomwona Kagame kuwa Mwendawazimu, ndivyo naye anavyowaona FDLR kuwa ni wendawazimu...
 
Me nashindwa kuelewa diplomats kazi yake nn, kagame kamtukana sana kikwete, na hakuna aliyeinua mdomo hata kusema chochote, hata waziri wa mabmo ya nje yupo kimya au ndio kuepusha mengine?? hapana upole uliopitiliza ni ujinga, huyu kagame tumuonyeshe sisi ni nani, tuna marafiki wengi, tumewasidia wengi (hata wanyarwanda) kikwete simpendi na wala simkubali(kwa sababu ya udhaifu wake kiuongozi) lakini anapotukanwa na kudharilishwa na kagame ni sisi sote kama nchi tumedharauliwa

Diplomacy kazi yake ni kudumisha mahusiano kwa njia ya amani... Kama vile kurudisha kumuelewesha Kagame kwa mazungumzo, bila kwaza kugombana nae...
 
Back
Top Bottom